Siku 100 za Edward Lowassa Madarakani

Siku 100 za Edward Lowassa Madarakani

Ocampo four

JF Senior Expert Member
Joined
Feb 28, 2014
Posts
5,789
Reaction score
2,159
1. Uhakika wa dawa na vifaa vya uzazi.

2. Umeme wa uhakika nchi nzima.

3. Kuanzisha mchakato wa katiba mpya.

4. Kupunguza foleni Dar-Es-Salaam na miji mikubwa.

5. Kuondoa kero kwa wafanya biashara ndogondogo (Machinga), Mamantilie na bodaboda.

6. Kuweka mipango kabambe ya Kumaliza tatizo la maji nchi nzima.

7. Mfumo bora na rafiki kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa.

8. Kufuta ada na michango kwa wanafunzi kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu.

9. Kupunguza kodi ya mshahara kwa wafanyakazi (PAYE).

10. Kufuta kodi zote za mazao kwa wakulima, wavuvi na wafugaji.

11. Mkakati wa kukuza michezo, sanaa na utamaduni.

12. Kuunda tume maalum ya kutatua migogoro ya wafugaji na wakulima.

13. Kuanzisha kituo kila wilaya kutoa huduma za serikali (one~stop centre).

14. Kuboresha maslahi ya watumishi wa vyombo vya usalama (polisi, wanajeshi, Takukuru). Kuboresha maslahi ya walimu, watumishi wa afya na watumishi wa serikali kwa ujumla.

15. Kuweka dira na mipango ya kuelekea katika uchumi wa kipato cha kati.
 
Mhhhh!! Hayo yote ndani ya siku 100. Nadhani hata baraza la mawaziri litakuwa bado halijaanza kazi.
 
Mhhhh!! Hayo yote ndani ya siku 100. Nadhani hata baraza la mawaziri litakuwa bado halijaanza kazi.

Ukiangalia yote hayo katibu 8 yanawezekana hata ndani ya siku 20.... Tatizo kubwa viongozi wa CCM wanakosa utashi wa kisiasa...

Kiongozi mzuri anapimwa ndani ya siku 100 duniani kote
 
1. Uhakika wa dawa na vifaa vya uzazi.

2. Umeme wa uhakika nchi nzima.

3. Kuanzisha mchakato wa katiba mpya.

4. Kupunguza foleni Dar-Es-Salaam na miji mikubwa.

5. Kuondoa kero kwa wafanya biashara ndogondogo (Machinga), Mamantilie na bodaboda.

6. Kuweka mipango kabambe ya Kumaliza tatizo la maji nchi nzima.

7. Mfumo bora na rafiki kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa.

8. Kufuta ada na michango kwa wanafunzi kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu.

9. Kupunguza kodi ya mshahara kwa wafanyakazi (PAYE).

10. Kufuta kodi zote za mazao kwa wakulima, wavuvi na wafugaji.

11. Mkakati wa kukuza michezo, sanaa na utamaduni.

12. Kuunda tume maalum ya kutatua migogoro ya wafugaji na wakulima.

13. Kuanzisha kituo kila wilaya kutoa huduma za serikali (one~stop centre).

14. Kuboresha maslahi ya watumishi wa vyombo vya usalama (polisi, wanajeshi, Takukuru). Kuboresha maslahi ya walimu, watumishi wa afya na watumishi wa serikali kwa ujumla.

15. Kuweka dira na mipango ya kuelekea katika uchumi wa kipato cha kati.

Baada ya hizo siku. Atuibie tena? # hapa ni kazi tu.
 
Sasa kama alikaa madarakani kwa muda wa siku 800 akiwa Waziri Mkuu na hakufanya hayo atawezaje ndani ya siku 100? Tumia akili. Lowasa ni sumu iliyojificha ndani ya asali
 
Ukiangalia yote hayo katibu 8 yanawezekana hata ndani ya siku 20.... Tatizo kubwa viongozi wa CCM wanakosa utashi wa kisiasa...

Kiongozi mzuri anapimwa ndani ya siku 100 duniani kote

All falls in short plan of about 2 (60 dys) 2 months. Kwanza hayo matatizo yote hayakupaswa kuwepo
 
Mzee wa pushup hajui atafanya nini ndani ya siku 100. Anasubiri maelekezo kutoka kwa WAMA Family
Hatuhitaji mtu ambaye utawala wake ni wa siku 100 tu. kiongozi mzuri ni yule anayepanga mikakati ya zaidi ya muongo mmoja
 
1. Magufuli ameshalisemea sana hili la madawa kwenye hospitali za serikali. Lowasa kacopy tu kwa mzee wa push up
 
Sasa kama alikaa madarakani kwa muda wa siku 800 akiwa Waziri Mkuu na hakufanya hayo atawezaje ndani ya siku 100? Tumia akili. Lowasa ni sumu iliyojificha ndani ya asali

Ujenzi wa shule za kata nchi nzima, ujenzi wa vyuo 2 vikubwa Tanzania, kupandisha watumishi madaraja na mishahara unafikiri ni jambo dogo?..... Na hapo hakuwa na full mandate kwenye utekelezaji.
 
2. Kuhusu uhakika wa umeme, hilo halihitaji kutekelezwa ndani ya siku 100. Tayari bomba la gesi toka Mtwara limekuja Dar na kuanza kuzalisha umeme pale kinyerezi na Ubungo. Baada ya tarehe 20 Oktoba, tatizo la umeme litakuwa limemalizika. Hizo siku 100 ni upuuzi mwingine
 
Tatizo mnadhani serikali inaendeshwa Kama saccos yake pale monduli.
 
3. Kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, hilo nalo si ajenda kwa sasa. Mchakato wa Katiba Mpya umekamilika na yeye alishiriki. Kilichobaki ni kura za maoni ambazo hazihitaji siku 100 kutekeleza
 
Lile jengo la bodi ya mikopi HESLB na wafanya kazi wake wataenda wapi?
 
4. Kuhusu kupunguza foleni ya Dar es Salaam, hilo tayari lipo kwenye utekelezaji. Miundombinu ya DART inaendelea kukamilishwa na zaidi ya mabasi 140 yameshaingia nchini. Mabasi hayo ni ya kisasa na makubwa ambayo yatapita kwenye njia rasmi na hivyo kuharakisha movement ya magari. Kweli Lowasa ni tapeli
 
na hiyo ndani ya siku 100 asisahau kutuwekea na treni za umeme(sub way) ili na sisi tuwaringishie Kenya.
maana uwezo anao
 
Back
Top Bottom