SIKIKA: Taarifa kwa vyombo vya habari

n00b

JF-Expert Member
Apr 10, 2008
1,006
2,667
[h=2]Taarifa hii ni muhimu sana
Taarifa kwa vyombo vya habari, Jumanne, Novemba 29, 2011 Wananchi walioarifiwa – Bajeti iliyoarifiwa

Taarifa kuhusu bajeti zilizotolewa hivi karibuni katika tovuti ya Wizara ya Fedha na Uchumi zimesaidia kuwawezesha wananchi kufuatilia mjadala wa bajeti na kuishauri serikali jinsi ya kutatua kero zinazowakabili.


Vitabu vya bajeti ni nyaraka muhimu inayo fafanua jinsi fedha za walipa kodi zinavyotumika katika taasisi mbalimbali za umma. Pamoja na umuhimu wake kwa umma, kwaki pindi cha miaka iliyopita, vilikuwa havitolewi kwa wananchi.


Kwa miaka kadhaa, Sikika pamoja na mashirika mengine ya kijamii kwa pamoja tumekuwa tukitoa rai kwa serikali kuchapisha vitabu vya bajeti hususan katika toleo la lugha rahisi na kuviweka kwenye tovuti.Wizaraya Fedha na Uchumi imeitikia rai yetu na kuweka matoleo ya

Lugha rahisi ya kitabu cha pili, cha tatu na cha nne katikat ovuti yake
www.mof.go.tzhttp://www.mof.go.tz

Sikika inahimiza wananchi wote kutembelea tovuti ya Wizara ya Fedha na Uchumi na kutumia fursa hii kutafakari kuhusu maswali yafuatayo:



  • Je, serikali imeweka kipaumbele katika elimu na afya?
  • Je, kiasi gani cha fedha kimeelekezwa katika serikali za mitaa?
  • Je,kuna mgawanyo sahihi warasilimali za umma?

Bajeti itakuwa na msaada kw awananchi pale tu itakapolenga kutatua kero na mahitaji yanayotoka kwa wananchi. Hivyo, Sikika inatoa rai kwa wananchi, kuhakikisha sauti zao zinasikika kwa kuwaagiza wawakilishi na wabunge wao kuhakikisha yafuatayo yanazingatiwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2012/13:



  • Bajeti ina akisi lengo la kutokomeza ujinga na maradhi, kwa
  • Kuwawezesha watoa huduma ili waweze kutoa huduma bora, na kwamba
  • Rasilimali zilizopo zinagawanywa kwa usawa.

Sikika inakumbusha serikali na wabunge kusikiliza na kuzingatia kwa umakini maoni ya wananchi kwa kuwa wanawajibika kwao na pia wananchi wana kauli ya mwisho katika sanduku la kura.


Ili kuifanya bajeti ya 2012/13 ya wananchi zaidi, serikali inapaswa kukumbuka kuweka taarifa mpya za kibajeti katika tovuti siku 21 kabla ya kuanza kwa bunge lijalo la bajeti. Kwa kufanya hivyo wananchi na wabunge watakuwa na muda wa kutosha kutoa ushauri katika maeneo mbalimbali na ushauri wao kuwafanyiwa kazi ndani ya muda sahihi.


Bw. Irenei Kiria
MkurugenziMtendaji, Sikika, S. L. P 12183 Dar es Salaam,

Simu: +255 222 666355/57, Nukushi: 2668015, Baruapepe: info@sikika.or.tz, Tovuti:
www.sikika.or.tz
[/h][h=2]
Tujiulize kuhusu utekelezaji wake. Pia kuna lile suala la taarifa za vifungu vya kasma kutofautiana linapokuja suala la implementation.

Download documents kamili hapa

[/h][h=2][/h]
 

Attachments

  • Press release_Informed citizens_informed budgets.docx
    77.4 KB · Views: 30
  • Taarifa Kwa umma-Informed budgets.docx
    78.1 KB · Views: 30
thanks.

but kuna ishu mbili: kuweka vitabu au kuweka vitabu vyenye taarifa genuine.
 
kwa budget zinavyobadilishwa na makatibu wakuu na wakuu wa idara............budget ya Tz haina maana kabisa. haionyeshi ukweli wa yatakayotokea.

Inaweza kutumika ufanya tracking....lakini kiuhalisia zoezi zima ni utapeli mtupu.

Bunge limepata wapi hela ya kupandisha posho kiasi hicho??? ina maana wamechukua hela kwenye budget line gani??

Kama mkurugenzi anaweza kuandikiwa barua na mkuu wa wilaya achangie gharama za mbio za mwenge, na mkurugenzi huyo akatoa hela kwenye budget line ya capitation grants to secondary schools, na kutoa magari mawili, kuyajaza mafuta na kutoa posho za wafanyakazi 10 ili washiriki kwenye mbio za mwenge.............budget ina maana gani???
 
Sikika inahimiza wananchi wote kutembelea tovuti ya Wizara ya Fedha na Uchumi na kutumia fursa hii kutafakari kuhusu maswali yafuatayo:

Je, serikali imeweka kipaumbele katika elimu na afya? Je, kiasi gani cha fedha kimeelekezwa katika serikali za mitaa? Je,kuna mgawanyo sahihi warasilimali za umma?
Labda hapa tuseme moja kwa moja kuwa wananchi wa mijini!....huh!
 
Bajeti ya Tanzania inapitishwa bungeni kutimiza wajibu tu. Lakini expenditure ni unrealistic, na kibaya zaidi ni kwamba kasma zinazowekwa kwa shughuli za maendeleo zinapotea hewani, hakuna mrejesho zaidi ya kutolewa hati chafu chini ya angalizo la wahusika kujitahidi kupata hati safi next ktk next count.

Seems hata wabunge wenyewe wana kifua cha kufuatilia kama taarifa na usahihi wa taarifa za bajeti zinawafikia wahusika (wananchi).. Ukifanikiwa kupata hilo lijikabrasha la taarifa za bajeti limejaa terminologies ambazo kama hujapitia madarasa ya uchumi unatoka kapa.
 
Bajeti ya Tanzania inapitishwa bungeni kutimiza wajibu tu. Lakini expenditure ni unrealistic, na kibaya zaidi ni kwamba kasma zinazowekwa kwa shughuli za maendeleo zinapotea hewani, hakuna mrejesho zaidi ya kutolewa hati chafu chini ya angalizo la wahusika kujitahidi kupata hati safi next ktk next count.

Seems hata wabunge wenyewe wana kifua cha kufuatilia kama taarifa na usahihi wa taarifa za bajeti zinawafikia wahusika (wananchi).. Ukifanikiwa kupata hilo lijikabrasha la taarifa za bajeti limejaa terminologies ambazo kama hujapitia madarasa ya uchumi unatoka kapa.

Tukubaliane kwamba kwa hatua ambayo wizara imeichukua ni nzuri japo bado kuna mapungufu mengi sana. lazima tuanzie mahali fulani kuelekea tunakokutaka. Ni kweli kwamba mara nyingi bajeti iliyoko kwenye vitabu ni tofauti kabisa na ile iliyopo kwenye taasisi husika. Pia kwa kuangalia taarifa zilizopo kwenye hivi vitabu ni vigumu kujua kuhalisia kwamba fedha zilizotengwa zinaenda kufanya shughuli gani. Kuna kitu kinachoitwa Medium Term Expenditure Framework (MTEF), humu ndimo kunakuwa na breakdown ya kila fedha iliyopangwa kwa maana ya shughuli gani zimetengewa kiasi gani haswa. Na hapa ndipo tunapoweza kuona kwa undani jinsi serikali inavyoelekeza rasilimali zake.

Hata hivyo, katika hivi vitabu viliyowekwa bado wananchi wanaweza kuona kwa ujumla wake utengaji wa fedha za bajeti haswa lile fungu la posho ukilinganisha na fedha za maendeleo.

Binaafsi ninaipongeza wizara ila bado safari ni ndefu maana hata lugha iliyotumika kwenye hivi vitabu ni ngeni kwetu wengi.
 
We bibi na babu kule kijijini kwetu mmesikia? mtembelee hiyo tovuti piga *148*01# mchague kifurushi
 
bajeti zitakuja kuleta maana pale ambapo mawaziri watakuwa sio wabunge
 
Back
Top Bottom