great 2012
Member
- Jun 27, 2012
- 23
- 8
Nilikuwa na mpenzi ambaye tulianza uhusiano mnamo mwaka 2010 kipindi hicho yeye alikuwa anasoma lakini wakaja wakakosana na wazazi wake hivyo akawa ni mtu wa kutanga tanga, mimi nikaona sio vizuri aendelee kuhangaika so nikachukua jukumu la kumsaidia kwa kumsomesha huku nikiwa na matumaini kwamba siku moja Mungu akijalia atakuja kuwa mke wangu,nilimlipia school fees tsh 600,000/= na kila wiki nilikuwa nampatia elfu 40,000/= ya matumizi lakini siku zilivyozidi kwenda mbele nikaja kugundua kuwa kumbe alikikuwa hasomi wala shule alikuw haendi, nilipo muuliza akakataa kata kata.
So mimi nikaona huyu mwanamke hanifai nikaamua kumwambia ukweli kuwa mimi na yeye basi lkn akaendelea kuning'ang'ania na kunitishia kuwa endapo nitamuacha ataniua, mimi nikaamua kutafuata mpenzi mwingine ambaye nilimpeleka kwa wazazi wangu, na wote walimfurahia na ndipo tukaanza process zote za kutoa mahali, hadi ninavyoandika post hii tayari vikao vya ndoa vimeshaanza na ndoa itafungwa mwezi ujao, cha kushangaza yule mwanamke wangu wa kwanza alipopata habari za mimi kuoa alinijia juu na kuniambia kuwa ana ujauzito wangu na tayari ameshawaambia wazazi wangu, na anapanga kupinga ndoa kanisani. JAMANI HAPA NILIPO MWENZENU NIMECHANGANYIKIWA HATA SIJUI NIFANYEJE?
So mimi nikaona huyu mwanamke hanifai nikaamua kumwambia ukweli kuwa mimi na yeye basi lkn akaendelea kuning'ang'ania na kunitishia kuwa endapo nitamuacha ataniua, mimi nikaamua kutafuata mpenzi mwingine ambaye nilimpeleka kwa wazazi wangu, na wote walimfurahia na ndipo tukaanza process zote za kutoa mahali, hadi ninavyoandika post hii tayari vikao vya ndoa vimeshaanza na ndoa itafungwa mwezi ujao, cha kushangaza yule mwanamke wangu wa kwanza alipopata habari za mimi kuoa alinijia juu na kuniambia kuwa ana ujauzito wangu na tayari ameshawaambia wazazi wangu, na anapanga kupinga ndoa kanisani. JAMANI HAPA NILIPO MWENZENU NIMECHANGANYIKIWA HATA SIJUI NIFANYEJE?