Sijui nianzie wapi?

Sijui nianzie wapi?

Kahema

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2010
Posts
202
Reaction score
43
Wanajamvi, natumaini muwazima wa Afya,
Nimeona nije kwenu walau mujue yanayonisibu, sio kitu kipya hapana, ila kimeniweka kwenye mazingira magumu sana, japo najitahidi kufanya kila linalowezekana walau upepo huu upite.

kifupi ni hivi Mama wa Watoto wangu (Mke) nimeamua kumrudisha kwao baada ya kugundua hakua mwaminifu kwangu ie niligundua anamahusiano ya Kimapenzi na Watu wengine Nje ya Ndoa, nilifanya uchunguzi wa kina nakugundua uchafu huo, baada ya mikimiki ya hapa na pale alikiri mbele ya wazazi wake kua yote niliyowaeleza ni ukweli mtupu. baada ya mashauriano ya muda mrefu nilifikia uamuzi wa yeye aondoke kwangu. hili halikua gumu sana kuamua kwa kila kitu kilikua wazi

So issue yangu kubwa ni nini nifanye baada ya hapa, ukizingatia yafuatayo:

1. tuna watoto watatu , mdogo kabisa ana miezi 9

2. hawa watoto nawapenda sana na mpaka sasa naishi nao

3.mimi mwenyewe umri umekimbia am 35 yrs now

4. mama watoto kila siku anapiga simu kuomba msamaha( japo najua kabisa jasiri haachi asili)

5. najiuliza hata kama nikitaka kuoa tena, will it be fair to my children?

6. nina watoto 3, will it suit me kuoa mwanamke ambaye hajazaa? ataweza kulea kwa upendo hawa watoto?

7.je nikioa mwanamke mwenye mtoto/watoto tayari si atataka naye awalete waishi kwangu? huu mzigo utaniua

8.je ni haki niwapeleke boarding hawa watoto ili mi niishi peke yangu?
kiukweli nipo njia panda, tafadharini yeyote anayeweza nisaidia kimawazo nitashukuru
asanteni!
 
Mi naona hiyo choice ya kuwapeleka watoto boarding ni nzuri wakati unatafakari nini cha kufanya..
 
msamehe tu anaweza kubadilika ila kama unaona uwezi peleka watoto boarding anza kutafuta ubavu wako
 
mkuu,nakushauri urudishe moyo nyuma,wafikirie watoto.unawatesa kwa dhambi ya mama yao.watoto huwa wana lose sana wasipomuona mama.ni bora uishi na huyo mwanamke hata kama mapenzi hakuna.hakuna kuduu au hata mtengane vitanda.lakini watoto wawe wanawaona mko pamoja.wanamuona mama na pia baba.hata darasani zitachaji sana.lakini kama unataka uwaharibu watoto basi wasiwe wanamuona mama yao around.
ni hayo tu mkuu,mengineyo kichwani mwako.
 
Ukisikia changamoto ndio hizo..dalili zote za kumsamehe naziona hapo...haya mrudishe nyumbani mlee watoto kuliko kwenda kuitafuta shida zaidi.. hao ndio wanawake...ukiviendekeza hivyo viumbe utakufa kwa ugonjwa wa moyo huku ukiwaacha wanaponda raha.,pole sana.
 
Mkuu pole sana msamehe yaishe mrudi katika hali ya furaha kama zaman mlee watoto na mungu awasimamie katika hili..
 
mkuu,nakushauri urudishe moyo nyuma,wafikirie watoto.unawatesa kwa dhambi ya mama yao.watoto huwa wana lose sana wasipomuona mama.ni bora uishi na huyo mwanamke hata kama mapenzi hakuna.hakuna kuduu au hata mtengane vitanda.lakini watoto wawe wanawaona mko pamoja.wanamuona mama na pia baba.hata darasani zitachaji sana.lakini kama unataka uwaharibu watoto basi wasiwe wanamuona mama yao around.
ni hayo tu mkuu,mengineyo kichwani mwako.

Mbaya zaidi kiongozi, wakati wa purukushani hii, huyu wife alishawahi kuwakimbia hawa watoto sio chini ya mara tatu. alidiriki kuondoka nyumbani zaidi ya siku sita, hiki hasa ndo kilichonifanya nisiwaze hata mara moja kumwambia aondoke kwangu. haikua rahisi na ni mengi sana nimeyaona sijayaweka hapa. najuta kumfahamu huyu mwanamke
 
Msamehe tu.

msamehe tu anaweza kubadilika ila kama unaona uwezi peleka watoto boarding anza kutafuta ubavu wako

mkuu,nakushauri urudishe moyo nyuma,wafikirie watoto.unawatesa kwa dhambi ya mama yao.watoto huwa wana lose sana wasipomuona mama.ni bora uishi na huyo mwanamke hata kama mapenzi hakuna.hakuna kuduu au hata mtengane vitanda.lakini watoto wawe wanawaona mko pamoja.wanamuona mama na pia baba.hata darasani zitachaji sana.lakini kama unataka uwaharibu watoto basi wasiwe wanamuona mama yao around.
ni hayo tu mkuu,mengineyo kichwani mwako.

Msamehe tu.........,

wanaume wana mioyo migumu ya kusamehe tofauti na wanawake

CC mahondaw tunahitaji busara zako hapa dada'angu. kuja haraka!!
 
Last edited by a moderator:
Peleka watoto boarding wakati unaendelea kutafakari.Baada ya muda msamehe mkeo arudi home.Ila watoto wasijue kama mmetengana,waambie mama kasafiri.

Ninavyowajua wanawake,hawezi tena kurudia kosa hilo hilo unless otherwise ndio tabia yake hata kabla hujamuoa(Neo maana tunashauriwa kujua background ya mume/mke kabla haujaoa/olewa).

Hata hivyo pole sana mkuu,nahisi maumivu unayoyapata!
 
Back
Top Bottom