Sijui Ndio Kupishana na Bahati Huku?

Sijui Ndio Kupishana na Bahati Huku?

Hongera kwa kununua gari, ila chukua tahadhari. Ukiendelea na tabia ya kutamani kila mwanamke na hasa kama hutatumia kinga, basi ujue HIV/UKIMWI itakutembelea. Vilevile hii tabia ya kuendesha gari huku macho yakisaka vimwana, basi kuna siku utaokotwa chini ya lori ukiwa hoi au tayari RIP.
 
Mi nilidhani unasema umepishana na Bahati Bukuku! Angalia ajali kaka, usipende kuangalia pembeni!
 
Mkuu hizo gari roho ya paka kama vipi tuongee dili nilkodi kusombea mkaa kwenye matanuri yangu ya igindu kusogeza pale chalinze make izo rover zinapitika hata majurubani.

Ha haaa! Yani mkuu unataka unitoe bara barani? No nimekataa. Kutembelea makalio raha!
 
Yani siku nikiwa kwa mguu au nikpanda dala dala huwa sibahatiki kukutana na 'watoto wazuri' tabu nikiwa kwenye private Car, ndio nawaona waleee! Na hivi breki zenyewe za kupampu pampu, mpaka nisimame unakuta mtoto keshapotea. Sasa sijui ndio kupishana na bahati kwenyewe huku?​

ndio umeandika ugoro gani hapo juu?
 
Back
Top Bottom