ChipeTungi Jr
Senior Member
- Sep 21, 2018
- 104
- 251
Habari wakuu.. Katika harakati za hapa na pale nikakutana na huyu mrembo wa kitanga kabila mzigua. Tumekutana kwenye site ya ujenzi yeye ni chief cooker hapa na mimi ni electrician. She's so cute, mpole na mtu wa dini sana (Muslim).
Kiukweli ukiachilia uzuri alionao nimevutiwa pia na maadili yake. Mtu wa stara muda wote, mchangamfu anacheka na kila mtu na ikifika time ya swala ataacha shughuli zake na kwenda kufanya ibada "I love that"
Mwanzoni sikuwa na ukaribu nae sana zaidi ya salamu tu. Mimi nimepita Madrassa kidogo ingawa si mtu wa dini kivile. Ijumaa moja kama leo baada ya swala sikuwa na kazi hivyo nikaenda eneo tunalolitumia kwa ajili ya chakula nikawa natwarihi Qur'an basi kuna aya nikawa nimekosea ghafla nikasikia sauti nzuri ya kike ikinisahihisha kugeuka nikamkuta ni yeye. Nikatabasamu na kumshukuru basi ukaribu ukaanzia hapo.
Tulizungumza mawili matatu then tukabadilishana namba za simu in case kama kuna changamoto yoyote kwenye chakula basi naweza kumcheck.
Kiukweli si mimi tu niliyekuwa na namba zake ni wafanyakazi wengi tu kwa kuwa utaratibu wa ofisi uko hivyo endapo ikitokea kuna malalamiko yoyote kwenye huduma ya chakula basi hupigiwa chief cooker moja kwa moja. Binafsi mwanzo sikuwa nayo kwa kuwa sikuona tatizo lolote kwenye chakula tangu nifike hapo pia bado nilikuwa mgeni hapo site.
Basi kwa kuwa nilishaanza kuvutiwa nae nikaamua nianze kujenga mazoea nae. Nilianza kwa kumjulia hali mara kwa mara naye akawa anarespond vizuri tu kisha story mbili tatu hasa zinazohusiana na dini then tungeishia hapo. Nilikuwa namvutia timing siku ajae kwenye kumi na nane zangu niyamwage ya moyoni maana nilishamuelewa huyu shombe wa kitanga.
Siku moja nimeingia job najaribu kumcheki oustadhat naambiwa amesafiri kwao Tanga. Wengine wanasema alikosana na boss bibie akaamua aache kazi basi ilimradi tu kila mtu anasema lake kwa masikitiko maana walimzoea sana.
Nilivurugwa nikaamua kumcheck muda ule ule akapokea kisha akaniomba radhi kwa kuchelewa kuniambia sababu safari ilikuwa ya ghafla sana. Akaniambia karudi Tanga ameamua kufungua restaurant yake huko hivyo hakuona haja ya kuendelea kuajiriwa tena.
Nilimuelewa zikapita wiki kadhaa tukiendelea kuwasiliana kawaida. Sasa siku moja nikaamua kumfungukia ukweli. Binti akashangaa kidogo kwa kuwa anadai yeye alinichukulia kama swahiba wa kawaida tu. Nilipomuuliza kama ana mtu akasema hana hivyo nimpe muda ajifikirie.
Baada ya siku kadhaa kupita usiku mmoja akanipigia simu baada salamu za hapa na pale akanikumbushia kuhusu lile ombi langu na kuwa amenikubalia isipokuwa akaniambia yeye ni single mother ana mtoto mmoja. Kuhusu baba wa mtoto alishafariki miaka miwili nyuma hivyo anaishi yeye mwenyewe na mwanawe wa kiume.
Sasa kilichonifanya niandike humu kuomba ushauri ni kuwa jana Alhamisi kanipigia simu anataka niende kwake Tanga. Yeye alijenga pamoja na mumewe na ndio anaishi humo hadi sasa.
Amefika mbali zaidi anasema amenitafutia kazi kwenye kampuni nzuri huko huko Tanga na kwamba nikifika mambo yasiwe mengi nipeleke barua ya posa haraka then ndoa ifungwe. Kiukweli naona imekuwa ghafla sana na nimeanza kuingiwa na wasiwasi kwa kweli.
Kiukweli ukiachilia uzuri alionao nimevutiwa pia na maadili yake. Mtu wa stara muda wote, mchangamfu anacheka na kila mtu na ikifika time ya swala ataacha shughuli zake na kwenda kufanya ibada "I love that"
Mwanzoni sikuwa na ukaribu nae sana zaidi ya salamu tu. Mimi nimepita Madrassa kidogo ingawa si mtu wa dini kivile. Ijumaa moja kama leo baada ya swala sikuwa na kazi hivyo nikaenda eneo tunalolitumia kwa ajili ya chakula nikawa natwarihi Qur'an basi kuna aya nikawa nimekosea ghafla nikasikia sauti nzuri ya kike ikinisahihisha kugeuka nikamkuta ni yeye. Nikatabasamu na kumshukuru basi ukaribu ukaanzia hapo.
Tulizungumza mawili matatu then tukabadilishana namba za simu in case kama kuna changamoto yoyote kwenye chakula basi naweza kumcheck.
Kiukweli si mimi tu niliyekuwa na namba zake ni wafanyakazi wengi tu kwa kuwa utaratibu wa ofisi uko hivyo endapo ikitokea kuna malalamiko yoyote kwenye huduma ya chakula basi hupigiwa chief cooker moja kwa moja. Binafsi mwanzo sikuwa nayo kwa kuwa sikuona tatizo lolote kwenye chakula tangu nifike hapo pia bado nilikuwa mgeni hapo site.
Basi kwa kuwa nilishaanza kuvutiwa nae nikaamua nianze kujenga mazoea nae. Nilianza kwa kumjulia hali mara kwa mara naye akawa anarespond vizuri tu kisha story mbili tatu hasa zinazohusiana na dini then tungeishia hapo. Nilikuwa namvutia timing siku ajae kwenye kumi na nane zangu niyamwage ya moyoni maana nilishamuelewa huyu shombe wa kitanga.
Siku moja nimeingia job najaribu kumcheki oustadhat naambiwa amesafiri kwao Tanga. Wengine wanasema alikosana na boss bibie akaamua aache kazi basi ilimradi tu kila mtu anasema lake kwa masikitiko maana walimzoea sana.
Nilivurugwa nikaamua kumcheck muda ule ule akapokea kisha akaniomba radhi kwa kuchelewa kuniambia sababu safari ilikuwa ya ghafla sana. Akaniambia karudi Tanga ameamua kufungua restaurant yake huko hivyo hakuona haja ya kuendelea kuajiriwa tena.
Nilimuelewa zikapita wiki kadhaa tukiendelea kuwasiliana kawaida. Sasa siku moja nikaamua kumfungukia ukweli. Binti akashangaa kidogo kwa kuwa anadai yeye alinichukulia kama swahiba wa kawaida tu. Nilipomuuliza kama ana mtu akasema hana hivyo nimpe muda ajifikirie.
Baada ya siku kadhaa kupita usiku mmoja akanipigia simu baada salamu za hapa na pale akanikumbushia kuhusu lile ombi langu na kuwa amenikubalia isipokuwa akaniambia yeye ni single mother ana mtoto mmoja. Kuhusu baba wa mtoto alishafariki miaka miwili nyuma hivyo anaishi yeye mwenyewe na mwanawe wa kiume.
Sasa kilichonifanya niandike humu kuomba ushauri ni kuwa jana Alhamisi kanipigia simu anataka niende kwake Tanga. Yeye alijenga pamoja na mumewe na ndio anaishi humo hadi sasa.
Amefika mbali zaidi anasema amenitafutia kazi kwenye kampuni nzuri huko huko Tanga na kwamba nikifika mambo yasiwe mengi nipeleke barua ya posa haraka then ndoa ifungwe. Kiukweli naona imekuwa ghafla sana na nimeanza kuingiwa na wasiwasi kwa kweli.