Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Taarifa ya GAG juu ya ufisadi wa uniform za polisi ulifanyika lini? Ni wazi ni kabla ya Lugola kuwa waziri wa Mambo ya Ndani. Taarifa ya CAG inasema malipo ya uniform za polisi yalifanywa mwaka 2015, na tunaelewa mwaka wa mwisho wa ukaguzi wa CAG ni 2016.
Sasa leo Kangi Lugola, miaka zaidi ya mitatu baada ya GAC kufanya ukaguzi na kukuta fedha za uniform zimetumika lakini uniform hakuna, anasema CAG aende kwenye maghala ya Polisi akaonyweshe uniform
Sasa jiulize - uniform zilizonunuliwa miaka mitatu iliyopita zinafanya nini ghalani au kwenye container hadi leo? Si zitakuwa zimevunda na kuoza? Lugola angekuwa na hata chembe ya busara, angesema uniform zilifika baada ya ukaguzi wa CAG. Lakini sasa kaamua kujifanya kikaragosi (puppet) wa Ndugai. Nimemtoa kabisa heshima kwa hili.
Kwa kweli sijawahi kuona mtu mwongo kama Kangi Lugola! Halafu eti ni waziri anaesimamia jeshi la polisi. Kama kweli Magufuli yuko serious na nchi hii Lugola aondolewe mara moja. Kumbuka juzi tu hapa Magufuli mwenyewe alitamka kwamba kuna ufisadi wa sare za polisi, kuwa hela zimelipwa sare hazipo na alitoa maagizo kwa Lugola, IGP, PS Meja Generali Rwegasira na makamishna wa polisi. Lugola si tu ni muongo, bali ni mwepesi kuongea na mzito kukumbuka, na kamtukana CAG na Magufuli kwa pamoja.
Sasa leo Kangi Lugola, miaka zaidi ya mitatu baada ya GAC kufanya ukaguzi na kukuta fedha za uniform zimetumika lakini uniform hakuna, anasema CAG aende kwenye maghala ya Polisi akaonyweshe uniform
Sasa jiulize - uniform zilizonunuliwa miaka mitatu iliyopita zinafanya nini ghalani au kwenye container hadi leo? Si zitakuwa zimevunda na kuoza? Lugola angekuwa na hata chembe ya busara, angesema uniform zilifika baada ya ukaguzi wa CAG. Lakini sasa kaamua kujifanya kikaragosi (puppet) wa Ndugai. Nimemtoa kabisa heshima kwa hili.
Kwa kweli sijawahi kuona mtu mwongo kama Kangi Lugola! Halafu eti ni waziri anaesimamia jeshi la polisi. Kama kweli Magufuli yuko serious na nchi hii Lugola aondolewe mara moja. Kumbuka juzi tu hapa Magufuli mwenyewe alitamka kwamba kuna ufisadi wa sare za polisi, kuwa hela zimelipwa sare hazipo na alitoa maagizo kwa Lugola, IGP, PS Meja Generali Rwegasira na makamishna wa polisi. Lugola si tu ni muongo, bali ni mwepesi kuongea na mzito kukumbuka, na kamtukana CAG na Magufuli kwa pamoja.