Babu Kijiwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2010
- 4,845
- 4,776
Habari wanabodi,
Kwa muda mrefu nimekuwa nikisikia habari kuhusu idara ya Usalama wa Taifa, nilivutiwa kuwafahamu hawa watu, nimesoma vitabu vingi na makala nyingi kuhusiana na watu hawa ila sijawahi kukutana nao katika maisha yangu.
Namaanisha sijawahi kukutana nao ana kwa ana, nasikia wapo kila sehemu nimetembea sehemu nyingi ila sijawahi hata kuhisi kuwa fulani ni Afisa usalama wa taifa.
Kuna wachache nilisikia wakitambulishwa kuwa ni watumishi wa TISS ila ni wale wenye nyadhifa kubwa mf. Mh Diwani Athumani (inasemekana hata kamanda Siro alikuwa hajui kuwa huyu bwana ni TISS) hapo nikachanganyikiwa zaidi hii inakuwaje?
Hawa watu wapo kweli au ni nafasi za kusadikika ambazo zinafanya watu waishi kwa nidhamu na kuheshimiana sababu hatujui nani ni nani?
Kama kweli wapo kwenye nchi hii basi watakuwa na mafunzo ya hali ya juu na maadili maana nadhani kwa jinsi nilivyotafuta taarifa zao ningekuwa nimemfahamu hata mmoja tu bila kuambiwa na mtu, wewe unamfahamu?
Nani alikwambia? (Achana na wale tunaowaona wakimlinda Mh Rais, nataka kujua hawa tunaoishi nao)
Kwa muda mrefu nimekuwa nikisikia habari kuhusu idara ya Usalama wa Taifa, nilivutiwa kuwafahamu hawa watu, nimesoma vitabu vingi na makala nyingi kuhusiana na watu hawa ila sijawahi kukutana nao katika maisha yangu.
Namaanisha sijawahi kukutana nao ana kwa ana, nasikia wapo kila sehemu nimetembea sehemu nyingi ila sijawahi hata kuhisi kuwa fulani ni Afisa usalama wa taifa.
Kuna wachache nilisikia wakitambulishwa kuwa ni watumishi wa TISS ila ni wale wenye nyadhifa kubwa mf. Mh Diwani Athumani (inasemekana hata kamanda Siro alikuwa hajui kuwa huyu bwana ni TISS) hapo nikachanganyikiwa zaidi hii inakuwaje?
Hawa watu wapo kweli au ni nafasi za kusadikika ambazo zinafanya watu waishi kwa nidhamu na kuheshimiana sababu hatujui nani ni nani?
Kama kweli wapo kwenye nchi hii basi watakuwa na mafunzo ya hali ya juu na maadili maana nadhani kwa jinsi nilivyotafuta taarifa zao ningekuwa nimemfahamu hata mmoja tu bila kuambiwa na mtu, wewe unamfahamu?
Nani alikwambia? (Achana na wale tunaowaona wakimlinda Mh Rais, nataka kujua hawa tunaoishi nao)