Sijawaelewa nhif na tangazo lao la interview,,,!

MR.LEO

Senior Member
Jun 10, 2012
129
24
Jamani,naombeni ufafanuzi wa tangazo la interview za NHIF la tarehe 8 juzi.
Wametoa ratiba na venue za interview bila kutoa shortlist ya majina!
SASA MIMI NITAJUAJE NA HUKU ZIMEBAKI SIKU CHACHE,,?
Na kuna haja gani ya kueleza vigezo vinavyomzuia mtu asiende kwenye interview wakati barua za maombi wanazo,,,?
Naombeni ufafanuzi kwa wenye uelewa jaman!
 
Kama unajijua uliomba wewe beba vyeti vyako nenda.
Mengine yatajulikanaga hukohuko.
Wanadhani mtu anafanya application moja kwa mwezi hadi akumbuke hiyo barua yake ilikua na nini au ilikosa nini?
Jiamini, nenda ila kwa walio nje ya Dar ni mtihani mgumu.
 
nenda tu ndugu kwenye hiyo interview wakizingua faitia hata jwtz,polic,magereza utapata
 
uyui panda nbs au treni au hamia dsm kama una ndugu ili kupunguza gharama ya kusafiri marakwamara
 
Hawa NHIF naona hawana HR kabsa,kwanini wanashindwa kufanya kazi zao??? au ndo ufisadi wao wa ajabu??Najuta sana kukatwa pesa zangu kwenda huku. Nadhani kwenye katiba mpya tuweke maoni yetu kwamba kuchangia kwenye hii mifuko kuwe kwa hiari na sio lazima kama sasa.
 
  • Thanks
Reactions: CAY
mi nadhan ingekuwa vyema kama wangetoa shortlist ya watu watakaofanya hiyo interview na si kuwaita wote walioapply,huu ni uzembe mkubwa sana!!!!!
 
samahani mkuu! kwani nssf,ssra na pssf ilikuwaje? mana na mimi nataka kwenda kufanya interview ila niko mbali

we nenda kajaribu hawa wanaweza kuwa fair, huwez jua. Ila nssf waliita watu weng ila walopata kaz hata interview hawakufanya.
 
we nenda kajaribu hawa wanaweza kuwa fair, huwez jua. Ila nssf waliita watu weng ila walopata kaz hata interview hawakufanya.

mkuu! mbona mimi nana jamaa zangu wamepata nssf! na walifanya interview tena mbili, written na oral ila wao nasikia walichukuwa watu kama 147 nadhani, ila wa kuchakachua lazima walikuwepo, sasa sijui huku nhif mana walioomba wengi wanaohitajika kulingana na tangazo la kazi hawazidi 30 nadhani hapa ndo kutakuwa na kuchakachuliwa 100% mana itaishia written interview tu. afu wahusika wataingia zao kazini, we acha tu! sisi wa huku mbali tunajifikiria kufunga safari kuja huko
 
hii kali usafiri kutoka kigomakwa ajiri ya usaili kati tayari wanawatu wao, polen wapendwa,

mkuu watu kama 10000 kwa hesabu la tangazo na ninauhakika wamepunguza idadi ya walioomba kwa kukadiria tu hizo namba! alafu wanaohitajika mkuu hata 30 nadhani hawazidi, sasa huu si mtihani kwelikweli mkuu! yani hapo inamaana wale walioshikwa mkono arua zao ziko tayari! watafanya watu interview afu wale wahusika wataitwa baada ya wiki mbili tatu kuanza mzigo, mie ngoja nibaki tu huku namtumbo
 
Back
Top Bottom