Siipendi democracy

the-true-wash

Senior Member
Oct 14, 2012
142
106
Wadau wenzangu naamini kabisa umasikini wetu woote huu ni kwa sababu ya democracy, tangu tukubali na kuanza kuiiishi democracy ndivyo umasikini unavyotuumiza aliye nacho atabaki kuwa nacho na asiyekuwa nacho atabaki masikini daima labda aibe au apate wadhifa fulani serikalini utaomfanya awe fisadi. Tanzania tuna kila kitu cha kuifanya iwe nchi tajiri saana.

Kwa kupitia democracy wawekezaji (wa nje hasa wazungu) tuliowafukuza kwa kutunyonya na kututawala tunawaleta tena ili waendelee kuiba mali zetu huku sisi tunaangalia tu! Hii sera wameanzisha wao kwa manufaa yao, walivyokuwa masikini hawakuwa na democracy kumbukeni nchi kama italy, germany,england zimetajirika bila kupitia democracy.

Kwa nini sisi na umasikini wetu tuikumbatie democracy? Wakati wake bado sana naamini tungeendeleza sera za Nyerere za ujamaa kama walivyofanya china tungekuwa mbaali sana hata viwanda vyetu vya wakati ule visingekufa. Democracy ni mbaya mbaya saana., wazungu wanaweka viongozi wao wanavyotaka, wanafanya wanavyotaka yote haya ni kwa sababu democracy inaruhuru RUSHWA kwa hali ya juu sana. Naishia hapo.
 
Nakubaliana na wewe. Tuanhitaji Rais amae ni Benevolent Dictator.i.e a kind, caring and compasionate dictator.

Benevolent dictatorship is a form of government in which an authoritarian leader exercises political power for the benefit of the whole population rather than exclusively for the benefit of himself or herself or only a small portion of the population. A benevolent dictator may allow for some democratic decision-making to exist, such as through public referendum ( from encyclopedia)
 
Tatizo si democracy bali mfumo wa kipuuzi ukisimamiwa na watawala vipofu na walafi. Kuna nchi nyingi zimeendelea pamoja na kuwa na democracy mfano Botswana kwa hapa Afrika. Hivyo tubadili mfumo wa kutawaliwa na miungu watu tena vipofu na majuha na koo zao.
 
Back
Top Bottom