karv
JF-Expert Member
- Dec 26, 2019
- 1,799
- 3,221
Habari zenu mabibi na mabwana
Baada ya kupitia vitabu baadhi nikapata kitu ambacho nimeona nilete kwa ajili ya kujifunza na kuongezeana ujuzi
Kitu chenyewe ni NDOA
=>Ndoa ni muunganiko wa hiyari kati ya mwanaume na mwanamke unaokusudiwa kudumu katika maisha yao yote.
SIFA ZA NDOA HALALI NI ZIPI
=>Ndoa lazima iwe ya hiyari kati ya mwanamke na mwanaume. Udanganyifu, kurubuniwa na ulaghai kunafanya ndoa isiwe halali. Ndoa za kuchaguliwa wenza na ndoa za mikeka hazitambuliwi kisheria.
=>Ndoa ni lazima iwe ya kudumu, ndoa ni lazima iwe ya kudumu vinginevyo kikatokea kifo ama talaka. Ndoa za mikataba hazitambuliwi.
=>Ndoa ni lazima iwe ya jinsia mbili tofauti. Ndoa za jinsia moja hazina uhalali kisheria.
=>Ndugu wa damu au ndugu wa karibu hawaruhusiwi kuoana.
=>Watu wanaotakiwa kufunga ndoa lazima wawe na umri kuanzia miaka 18 na zaidi. Lakini mwanamke mwenye umri wa chini ya miaka 18 anaruhusiwa kuolewa kwa idhini ya baba yake.
=>Kama wafunga ndoa mmoja wao ana ndoa ya mke mmoja basi hawezi kufunga ndoa nyingine. Mtu mwenye ndoa ya wake wengi hawezi kufunga ndoa ya mke mmoja.
=>Kusiwe na pingamizi la aina yeyote na ndoa itangazwe siku 21 kabla ya kufungwa.
=>Mfungisha ndoa lazima awe na mamlaka ya kufungisha ndoa.
=>Lazima wakati wa kufungisha ndoa kuwe na mashahidi wasiopungua wawili.
=>Wafunga ndoa wote lazima wawepo siku ya kufunga ndoa.
MAMBO YATAKAYOFANYA NDOA KUWA BATILI
● Kutoweza kufanya tendo la ndoa.
● Mke kudhihirika kuwa alikuwa na mimba ya mwanaume mwingine.
● Mmoja wa wanandoa kudhihirika kuwa na kichaa au kifafa.
● Mmoja wa wanandoa kudhihirika kuwa alikuwa ana magonjwa ya zinaa.
● Mwanandoa mmoja kukataa kwa makusudi kufanya tendo
la ndoa tangu ndoa kufungwa.
Naomba kuwasilisha.
Baada ya kupitia vitabu baadhi nikapata kitu ambacho nimeona nilete kwa ajili ya kujifunza na kuongezeana ujuzi
Kitu chenyewe ni NDOA
=>Ndoa ni muunganiko wa hiyari kati ya mwanaume na mwanamke unaokusudiwa kudumu katika maisha yao yote.
SIFA ZA NDOA HALALI NI ZIPI
=>Ndoa lazima iwe ya hiyari kati ya mwanamke na mwanaume. Udanganyifu, kurubuniwa na ulaghai kunafanya ndoa isiwe halali. Ndoa za kuchaguliwa wenza na ndoa za mikeka hazitambuliwi kisheria.
=>Ndoa ni lazima iwe ya kudumu, ndoa ni lazima iwe ya kudumu vinginevyo kikatokea kifo ama talaka. Ndoa za mikataba hazitambuliwi.
=>Ndoa ni lazima iwe ya jinsia mbili tofauti. Ndoa za jinsia moja hazina uhalali kisheria.
=>Ndugu wa damu au ndugu wa karibu hawaruhusiwi kuoana.
=>Watu wanaotakiwa kufunga ndoa lazima wawe na umri kuanzia miaka 18 na zaidi. Lakini mwanamke mwenye umri wa chini ya miaka 18 anaruhusiwa kuolewa kwa idhini ya baba yake.
=>Kama wafunga ndoa mmoja wao ana ndoa ya mke mmoja basi hawezi kufunga ndoa nyingine. Mtu mwenye ndoa ya wake wengi hawezi kufunga ndoa ya mke mmoja.
=>Kusiwe na pingamizi la aina yeyote na ndoa itangazwe siku 21 kabla ya kufungwa.
=>Mfungisha ndoa lazima awe na mamlaka ya kufungisha ndoa.
=>Lazima wakati wa kufungisha ndoa kuwe na mashahidi wasiopungua wawili.
=>Wafunga ndoa wote lazima wawepo siku ya kufunga ndoa.
MAMBO YATAKAYOFANYA NDOA KUWA BATILI
● Kutoweza kufanya tendo la ndoa.
● Mke kudhihirika kuwa alikuwa na mimba ya mwanaume mwingine.
● Mmoja wa wanandoa kudhihirika kuwa na kichaa au kifafa.
● Mmoja wa wanandoa kudhihirika kuwa alikuwa ana magonjwa ya zinaa.
● Mwanandoa mmoja kukataa kwa makusudi kufanya tendo
la ndoa tangu ndoa kufungwa.
Naomba kuwasilisha.