NAKUMBUKA nilipokua shule ya msingi na sekondari nili imba sana tena kwa shangwe na hamsa kubwa . nili imba TANZANIA TANZANIA NAKUPENDA KWA MOYO WOTE, NA NILALAPO NAKUWAZA WEWE PIA NIAMKKAPO NI HERI MAMA WEE......................... LAKINI kwa hali hii iliyonikuta sidhani kama kweli nitakuimbia wimbo huu eeeeweeh TANZANIA kwa moyo wangu. Ntakua mnafiki na mzandiki kuimba nakupenda wakati moyo wangu umejawa na simanzi kubwa, maswali mengi yasiyo na majibu. umebeba visasi na risasi umebeba ujumbe wa dhiki na shida. sina furaha tena na wewe TANZANIA. NAINGIA MWAKA 2012 NIKIWA NA FUNDO KUBWA MOYONI NIKIKUMBUKA YALIYO NIKUTA TAREHE ZA ISHIRINI. SIJUI KAMA NTASAHAU TUKIO LA MAJI KUINGIA NDANI MPAKA KUBOMOA UKUTA WANGU. SITA SAHAU JINSI NLIVYO JITAHIDI KUOKOA MAISHA YANGU NA MAISHA YA JAMAA ZANGU, SITASAHAU KUMPOTEZA MTOTO WANGU NA KUJIKUTA MIMI NA MAMA WA MTOTO TUKIWA TUMESHIKILIA MTI AMBAO UMEBAKI KIDOGO TU KUFUNIKWA NA MAJI. SITASAHAU NYOKA NA KENGE TULIOKUA NAO KARIBU WAKIJITAHIDI NA WAO KUOKOA MAISHA YAO. SITA SAHUA SAUTI YA SPIKA ZA POLISI INYOTAMKA TULIENI NA MUWE WAVUMILIVU TUNAJITAHIDI KUTAFUTA LIFE JACKETS ZA KUWAKOA.SITA SAHAU KUONA VIONGOZI WETU WAKITABASAMU NA KULA KRISMASS KWA BASHASHA WAKATI TULIOWACHAGUA TUKI TAABIKA KWA DHIKI ISIYO MFANO.. SITA SAHAU NAINGIA MWAKA WA 2011 NIKIWA NA KAPTULA 1 NA TISHET NA YEBOYEBO CHINI, HUKU MKE WANGU AKISHINDIA DERA MOJA. SITASAHAU.... HAKIKA..... SITASAHAU UPWEKE NILIONAO NA KUKOSA TUMAINI...SIDHANI KAMA BADO NAIPENDA NCHI YANGU