Siasa zimezidi The Law School of Tanzania. Hiki chuo kimulikwe!

Mada yako kuihusianisha na siasa nakubaliana nawe, namfahamu mwalimu mmoja hapo Law School aliwahi kupewa shavu na JPM enzi zile, akawa wakili wa serikali, hivyo tabia za kisiasa kuwepo kwenye utendaji wa hicho chuo sishangai.

Hii elimu ya Law School huwa naona kama imelazimishwa kuwa ngumu kwa manufaa ya wachache, siku hizi imegeuzwa kufaulu mitihani yao kuwa kama kushinda bahati nasibu.

Huo mfano uliotoa wa idadi ya wanafunzi wanaofaulu huku wengi wa wanaofeli wakiwa wametoka vyuo vile vile vinavyofundishwa na walimu walewale, ni jambo la kushangaza zaidi, nieleweke; sio kwamba nalazimisha wafaulishe wengi ili kuturidhisha, lakini kwa trend ilivyo ya ufaulu kila mwaka hairidhishi.

Wale jamaa zangu ni kama wamejigeuza "miungu watu" wanajua wao ndio wameshika funguo zenu kuwa mawakili, hivyo lazima wafanye namna ya kuwapunguza kwa kila njia ilimradi siku ya mwisho viwango vya wafaulu viwe chini.

Lakini hawajui kwa kufanya kwao hivyo, wanaitia jamii mashaka juu ya uwezo wao wa kiufundishaji, kwanini wanafunzi wengi wanafeli kila mwaka zaidi ya wanaofaulu? sasa "Law School" imegeuka kuwa "School of Failures"?!

Huwa nahisi kama wana mpango maalumu wa kuhakikisha wana "regulate" idadi ya mawakili Tanzania, kwamba isiwe kubwa na kupunguza soko lao, hasa ukizingatia "unyeti" wa fani yao [wakili msomi].

Huo mfano wa kuingia kwenye chumba cha mtihani na kitabu OG uliotoa, huku wenye photocopy wakibanwa, nao ni kielelezo cha ujanja ujanja wanaofanya hao walimu, lakini niwape angalizo tu...

Hata hao wanaoingia kwenye chumba cha mtihani na kitabu OG, bado wasijiamini, wajiandae kwa lolote, hapo kinachoangaliwa na muuza kitabu ni biashara yake pekee, ufaulu wako haumuhusu, matokeo ya hilo somo yakitoka mtu akafeli licha ya kuwa na kitabu kwenye chumba cha mtihani msishangae, maisha yenu sio mepesi hivyo.
nchi hii ngumu sana kila eneo lina vikwazo kibao pia kwa wahasibu ndo kabisa kuipata hiyo CPA (T) ujue si chini ya miaka 7 hata wanaosomea udaktari ni cha mtoto.wenzetu ulaya na marekani vitu kama hiyo ni rahisi sana kuvipata na wanafunzi wakifeli huyo mwalimu anajisikia vibaya sana kwani kufeli kwake ni sawa na kufeli kwa huyo mwalimu.
 
Kwa hakika hii nchi ni ngumu sana. Mambo yote hata yasiyopaswa yamegeuzwa kuwa siasa siasa tu.

Hili la law school nalo kwa hakika ni shida.

Examination Results

Hiyo ni "site' yenye matokeo yaliyotoka tangia jumatano 5/10 lakini hayafunguki.

Waliofeli, watatakiwa kwenye supplementary zitakazoanza jumatatu 10/10.

"Watajua vipi wanafunzi waliofeli kuwa wamefeli na kujiandaa tokea kokote waliko Tanzania, kufika kwenye mtihani Dar kwa wakati?"

Hayupo anayejali ila kukusanya pesa za ada tu.

Mass failures ni jambo la kawaida kwenye chuo hiki. Takwimu zinaonyesha si nadra wanafunzi 30 tu kufaulu baina ya wanafunzi 400. Kwa uhalali upi?

Wanafunzi hawa huwa ni wahitimu wa shahada za kwanza, wengine wakiwa na shahada za uzamili na hata za uzamivu. Walimu Law School ni hawa hawa wanaofundisha UDSM na vyuo vingine.

"Iweje wanafunzi hao kufeli law school wanapokuja kusoma kwa mwaka mmoja tu, kwa walimu hao hao?"

Mazingira wezeshi kabisa kwenye zile rushwa zetu pendwa za ngono na mauzo batili ya notes.

"Iweje kitabu 'original' kilichoandikwa na mwalimu husika kuruhisiwa kuingia nacho kwenye mtihani, lakini siyo photocopy ya kitabu hicho hicho?"

Kwa hakika kuna mengi ya kuangaliwa kwenye vyuo hivi vinavyoendeshwa na walimu miungu watu.
Pole mkuu kwa supp
 
Mkuu kukubali kutishwa na miungu watu siyo suluhu. Haya ya kuhofia kulipiziwa visasi ndiyo yanayoukomaza ubaradhuli.

Woga na hofu nyingi zilizotujaa watanzania ndizo zilizotufikisha hapa tulipo. Kila mtu anaogopa kuchuma janga asije kula na wa kwao.

Nchi imejaa opportunists.
Hatari sn
 
Hatari sn

Si kidogo. Utaratibu wa utahini vyuo vikuu ndiyo chanzo cha haya. Utaratibu wa utahini shule za msingi na sekondari ni muafaka zaidi.

Mtunga mtihani hapaswi kumfahamu mtahiniwa, hali kadhallika msahishaji hapaswi kuwa ndiye mtahini.

Imekuwa kusema hadi uvuke mto. Wa kumfunga paka kengele hayupo hadi mtu avuke mto kwanza.
Mtu ukivuka mto ya nini kujihusisha na yasiyomhusu?

Vicious cycle inaendelea.
 
nchi hii ngumu sana kila eneo lina vikwazo kibao pia kwa wahasibu ndo kabisa kuipata hiyo CPA (T) ujue si chini ya miaka 7 hata wanaosomea udaktari ni cha mtoto.wenzetu ulaya na marekani vitu kama hiyo ni rahisi sana kuvipata na wanafunzi wakifeli huyo mwalimu anajisikia vibaya sana kwani kufeli kwake ni sawa na kufeli kwa huyo mwalimu.

Kupigania haki za watahiniwa ni jambo la msingi.

Mtunga mtihani, msahishaji na mtahiniwa zinapaswa kuwa pande tatu zisizofahamiana.

Vinginevyo u Mungu mtu itabakia kuwa ni matokeo tu.
 
Je kwa Tanzania mitihani ya law school ifutwe au iboreshwe ili tupate fursa ndani na nje ya nchi

2 February 2019
Kampala, Uganda

Legal experts disagree on removing LDC pre-entry exams



Over the years, scores of people have failed the pre-entry exams for the Law Development Centre bar course. Last year, the debate in many circles on whether these exams are a necessity raged on after Parliament passed a resolution to have the examinations suspended. The President of the Uganda Law society Simon Peter Kinobe does not agree with the call to scrap the pre-entry exams.

Source: NTVUganda


Waungwana wanasema:

The way to hell is paved with good intentions.

Tatizo si mitihani. Tatizo ni mode ya examinations.

Gone are the days at MUCHS when barely 2 doctors could hardly pass, out of a batch of 40.

Walitanzua vipi utata kama huu pale?
 

THE LAW SCHOOL OF TANZANIA : Taasisi ya Uanasheria kwa Vitendo



Kuandikishwa ktk daftari kama mawakili binafsi walioonesha umahiri kupitia mitihani yao hivyo wanaweza kuwawakilishi wateja katika mahakama za wilaya na mahakama kuu mahakama ya rufaa....


Kwamba mtu kasoma sheria Hadi Ph.D lakini kafeli LST haya ni Tanzania tu no wonder:

"Ways to hell are paved with good intentions."
 
Umeandika ukweli sana yaani !! hongera kwa kuwasemea watu hawa

Hata website ya matokeo haIfanyi kazi. Ole wako ujitie kimbele mbele kuuliza.

Kwamba kuwa na Ph.D ni bure ila kuwa na cheti Cha TLS, na watu wote wameufyata?

Hii nchi ni ngumu sana.

Si bora watu wakasome law school peke yake waachane na yasiyokuwa na faida?
 
Mazingira wezeshi kabisa kwenye zile rushwa zetu pendwa za ngono na mauzo batili ya notes.

"Iweje kitabu 'original' kilichoandikwa na mwalimu husika kuruhisiwa kuingia nacho kwenye mtihani, lakini siyo photocopy ya kitabu hicho hicho?"
Mkuu, Africa has it's own ways of running things. Usiumize sana kichwa chako kwa watu ambao hawataki positive changes.

All in all, tungepata fursa ya kusikia upande wa mlalamikiwa ingekuwa vema zaidi ili tuweze kutoa huku iliyo sahihi.
 
Kwa hakika hii nchi ni ngumu sana. Mambo yote hata yasiyopaswa yamegeuzwa kuwa siasa siasa tu.

Hili la law school nalo kwa hakika ni shida.

Examination Results

Hiyo ni "site' yenye matokeo yaliyotoka tangia jumatano 5/10 lakini hayafunguki.

Waliofeli, watatakiwa kwenye supplementary zitakazoanza jumatatu 10/10.

"Watajua vipi wanafunzi waliofeli kuwa wamefeli na kujiandaa tokea kokote waliko Tanzania, kufika kwenye mtihani Dar kwa wakati?"

Hayupo anayejali ila kukusanya pesa za ada tu.

Mass failures ni jambo la kawaida kwenye chuo hiki. Takwimu zinaonyesha si nadra wanafunzi 30 tu kufaulu baina ya wanafunzi 400. Kwa uhalali upi?

Wanafunzi hawa huwa ni wahitimu wa shahada za kwanza, wengine wakiwa na shahada za uzamili na hata za uzamivu. Walimu Law School ni hawa hawa wanaofundisha UDSM na vyuo vingine.

"Iweje wanafunzi hao kufeli law school wanapokuja kusoma kwa mwaka mmoja tu, kwa walimu hao hao?"

Mazingira wezeshi kabisa kwenye zile rushwa zetu pendwa za ngono na mauzo batili ya notes.

"Iweje kitabu 'original' kilichoandikwa na mwalimu husika kuruhisiwa kuingia nacho kwenye mtihani, lakini siyo photocopy ya kitabu hicho hicho?"

Kwa hakika kuna mengi ya kuangaliwa kwenye vyuo hivi vinavyoendeshwa na walimu miungu watu.
HATA MATOKEO YAO HAYA YALIYOTOKA JUMATANO YANA WALAKINI INABIDI WARUDIE KUYASAHIHISHA MAANA KUNA WATU WAMEFELISHWA MAKUSUDI
 
Mkuu, Africa has it's own way of running things. Usiumize sana kichwa chako kwa watu ambao hawataki positive changes.

All in all, tungepata fursa ya kusikia upande wa mlalamikiwa ingekuwa vema zaidi ili tuweze kutoa huku iliyo sahihi.

Ngoja tuwasubirie labda walikuwa wanashughulikia Ile website ya matokeo ilivyokuwa inazidi kuwatolea uvundo zaidi.

Kweli Africa Ina namna yake. No wonder we are poor.
 
Kama umeamua kusoma soma jamani elimu ya kupeana. Sio poa
Kwa maana iyo mnataka hata walio feli wafaulishwe? Big NO
 
Hayo ni matokeo ya kawaida kabisa mkuu.

Kufaulu 30 kati ya 400.

Toka hiyo shule imeanza matokeo yapo hivyo.
 
Hayo ni matokeo ya kawaida kabisa mkuu.

Kufaulu 30 kati ya 400.

Toka hiyo shule imeanza matokeo yapo hivyo.

30 kati ya 400 na hao LLB, LLM na Ph.D holders wewe waona ni kawaida?

Hata Muhimbili wakifaulu 2 au hamna kati ya 40 pana warusi wa pande za Buza hawakuchoka kudai ilikuwa ni kawaida hiyo. Hadi dua la kuku lilipomfika mwewe.
 
30 kati ya 400 na hao LLB, LLM na Ph.D holders wewe waona ni kawaida?

Hata Muhimbili wakifaulu 2 au hamna kati ya 40 pana warusi wa pande za Buza hawakuchoka kudai ilikuwa ni kawaida hiyo. Hadi dua la kuku lilipomfika mwewe.
Kawaida sana.
 
Back
Top Bottom