Kwanza nashukuru ndugu yangu kwamba tumetoka kubishana hadi sasa kujadiliana, hayo ndiyo mabadiliko ya kweli na Uhuru wa Kweli ambao CHADEMA inaupigania.
Igunga hoja kubwa ilikuwa kama Igunga ni maskini au si maskini na kama ni maskini ni nani kausababisha huo umaskini. Kwa hoja hii CDM walishinda kwani wananchi wenyewe wa Igunga wanajua umaskini wao. Pia Igunga walikuwa hawawachagui hao niliowaorodhesha bali walikuwa wanataka kuchagua Kashindye mwana Igunga mwenzao na mwalimu maarufu anayefahamika na wengi.
CUF hawakuchaguliwa kwa sababu wenyewe waliwekeza kidogo kwenye upelekaji wa ujumbe wao kwa wananchi hadi wakashindwa kujitofautisha wao na CCM ambao wananchi wa Igunga walishaamini ndiyo wezi wa rasirimali zao na ndiyo waliosababisha wao wawe maskini.
Hakuna anayejua kwenye suala la kura ni za nani zilikwenda CDM. Kwa nini usifikiri kwamba za CUF zilikwenda CCM na CDM wao walichota za CCM?
Kura za CUF zilipungua kwa sababu walikuwa hawana hoja mahsusis inayokubalika kwa wananchi. Halafu kumbuka ndoa ya CCM na CUF ni mzigo unaowatesa CUF huku Tanzania Bara.
Hivi vyama vyote ulivyovitaja uwekezaje wake wa kifedha na rasirimali watu huwezi kuufananisha na CCM na CDM. CDM walikuwa na Helkopta moja wenzao wa CCM walikuwa nazo mbili. Igunga kuna kata 26 hivi vyama vingine hata magari walifanya kukodisha au walikuw nayo chakavu. kwa mantiki hiyo utaona ni kwa nini mvutano ulikuwa ni kwa CCM na CDM na CUF kwa Mbaaali.
Wabunge wa CCM na CDM walikuwa wanapishana mbugani na magari yao huku wengine wa vyama hivi hata kuzindua kampeni zao walikuwa na Horn speakers tu. heri yule wa UPDP alituburudisha kwa Mayenu.
TAFAKARI CHUKUA HATUA. Ujumbe umefika maana hakuna ata mtu anayepinga kwa ushahidi kama ulivyofanya wewe.
hata wakiwa wote pilipili usiyoila yakuwasha nini? Buku 2 ya lunch imekutoa leo.
migwanda bwana sasa nape anahisika nn hapo au kawashika sana.. mbona hamkanushi kama ni uongo huo ulioandikwa...nepi kakupa hela ya kula mchana huu?
Unashangaza. Yaani suala la chama cha siasa ambacho ni taasisi ya umma kupachikana madarakani kwa upendeleo unaita pilipili usiyoila! Kweli wewe umepauka kichwani.
migwanda bwana sasa nape anahisika nn hapo au kawashika sana.. mbona hamkanushi kama ni uongo huo ulioandikwa...
hata wakiwa wote pilipili usiyoila yakuwasha nini? Buku 2 ya lunch imekutoa leo.
migwanda bwana sasa nape anahisika nn hapo au kawashika sana.. mbona hamkanushi kama ni uongo huo ulioandikwa...
Sasa wewe kila siku kelele tu kama una pesa kajenge Makao Makuu ya CDM pale Manyanya.
Makao Makuu utadhani ofisi ya Saccos ya Tandale.
Mimi kwa siku tu natumia all most $60 kwa ajili ya Internet tu, Laptop, Desktop, BlackBerry Touch.
Nakushauri fanya kazi acha kukaa kwenye vijiwe vya mbege na komoni
Huyu jamaa kila post yake lazima amtaje nape, sijui kwa nini lakini uwezi kujua asifie mvua imemnyea...Ha! Ha! Ha! Ha!
migwanda bwana sasa nape anahisika nn hapo au kawashika sana.. mbona hamkanushi kama ni uongo huo ulioandikwa...
Sasa wewe kila siku kelele tu kama una pesa kajenge Makao Makuu ya CDM pale Manyanya.
Makao Makuu utadhani ofisi ya Saccos ya Tandale.
Mimi kwa siku tu natumia all most $60 kwa ajili ya Internet tu, Laptop, Desktop, BlackBerry Touch.
Nakushauri fanya kazi acha kukaa kwenye vijiwe vya mbege na komoni
Aliyekuwa diwani wa kata ya kaloleni kupitia CHADEMA inasemekana anatafutwa na Polisi kwa tuhumu za kumtapeli mwekezaji mwenza kwenye biashara yao ya utalii. Charles David Mpanda (Rasta) anadaiwa kumtapeli Margaret Lema kiasi cha Dola 16,400 kutoka kwenye akaunti yao ya pamoja.
Hili jambo limenifanya nifikirie upya siasa za bongo. Margaret ni Mdogo wake God bless Lema Mbunge wa Arusha Mjini kwa maana nyingine yale yanayotokea CCM kwa watu wa ukoo mmoja kumiliki chama yanatokea na CHADEMA pia. Mbowe kaoa mtoto wa Edwin Mtei Muasisi wa CHADEMA, Lucy Owenya mbunge wa viti maalum ni mtoto wa Philimon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini.
Ukikutana na Rose Kamili Mbunge wa viti maalum ujue ni mzazi mwenzie Dr. Wilbroad Slaa pia ujue kwamba ukikutana na Christina LIssu ni Mdogo wake na Tundu Lissu, na Moulida au Anna Komu Mbunge Viti maalum ni Mke wa mkuu wa Idara ya fedha Makao Makuu CHADEMA, Anthony Komu. Hawa ni wale wanaohusiana kimapenzi na kiukoo hatujui wale wanaohusiana kimaslahi kama vile kibiashara wako wangapi na kwenye ngazi zipi. Lakini jambo hili kwa sababu limetokea CDM basi litatetewa weeee hadi mijasho itukauke.
Aliyekuwa mkuu wa upelelezi Kanda Maalum ya Dar es salaam Abdalah Zombe alidai kwamba Godbless Lema alikuwa ni mwizi wa magari. Sijaona mcharuko mkubwa angalau wa kumshinikiza Zombe aseme anavyojua wizi wa magari wa Lema wala wa kumshinikiza Lema kueleza historia yake ya nyuma kabla hajawa Mbunge inahusiana vipi na wizi wa magari. Wote tuko kimyaa kwa sababu ni mtoto wa nyumbani. Rage kuonyesha Bastola ilikuwa nongwa lakini la Lema ni "Uzushi' wa magamba.
Sasa wewe kila siku kelele tu kama una pesa kajenge Makao Makuu ya CDM pale Manyanya.
Makao Makuu utadhani ofisi ya Saccos ya Tandale.
Mimi kwa siku tu natumia all most $60 kwa ajili ya Internet tu, Laptop, Desktop, BlackBerry Touch.
Nakushauri fanya kazi acha kukaa kwenye vijiwe vya mbege na komoni
Ukisubiri wamalize hoja itapotoshwa ,ni bora uchangie ingali moto. CHUMA KIKOLI MOTO. Nimewahi kuchangia kuhusu CDM kujipanga kufungua matawi mengi vijijini lakini nikatahadharisha kuwa vijana baadhi wa CDM hawana uwezo wa kujenga hoja kisayansi kuvutia hadhira hasa ya wenye umri wa miaka 50 hasa akina mama ambao ni mtaji mkubwa. Nimesoma michango hapa ni matusi, hoja hazishikiki, mtawapataje wanachama makini wanaotaka kushawishiwa taratibu? Watu wazima hawapokei mageuzi mara moja wanatafakari kwanza. Refer; CONSUMER BEHAVIOUR, hoja dhidi ya CDM hata zikiwa zinauma kiasi gani na ukweli ndani yake tusijibu kwa jazba as if CDM ni malaika,tunakosea.NGUVU YA NGUVU HAILETI TIJA EXCEPT HOJA YA NGUVU MAKES ALOT
Umemaliza mkuu? ukimaliza nijulishe ndio nichangie..............
Hao vijana ndiyo balaa kwa kuporomosha "mistari" bila vina wakiulizwa kulikoni wanajitetea eti ni wapiganaji. Kwa taarifa yao wanamtandao waliomweka Kikwete madarakani mwaka 2005 ndiyo walikuwa wanajiita wapiganaji labda hili la "makamanda" ndiyo jipya..... lakini nikatahadharisha kuwa vijana baadhi wa CDM hawana uwezo wa kujenga hoja kisayansi kuvutia hadhira hasa ya wenye umri wa miaka 50 hasa akina mama ambao ni mtaji mkubwa
Ni kweli kwa sababu watu wenye umri mkubwa wanajua mengi wanakumbuka tangu enzi za AMNUT mpaka Mtikila alipotuletea misamiati ya "walalahoi" na "magabachori" huku akituchombeza na kauli mbiu "Saa ya ukombozi ni sasa. tumeona mengi.Hasa akina mama ambao ni mtaji mkubwa. Nimesoma michango hapa ni matusi, hoja hazishikiki,mtawapataje wanachama makini wanaotaka kushawishiwa taratibu?
Watu wazima hawapokei mageuzi mara moja wanatafakari kwanza. hoja dhidi ya CDM hata zikiwa zinauma kiasi gani na ukweli ndani yake tusijibu kwa jazba as if CDM ni malaika,tunakosea.