Siasa safi ni zao la watu safi wenye dhamira safi

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Siasa safi ndio msingi Wa maendeleo ya kweli kwenye nchi yoyote. Bila Siasa safi; jamii haiwezi kupiga hatua yoyote ya maana.

Hata hivyo Siasa safi ni zao la watu safi, wenye dhamira safi na matendo safi.

Ni kwa vipi tunaweza kuwa watu safi ili toka kwetu tuwe na Siasa safi na hivyo kufikia Tanzania tunayoitaka?

Usiwaze kupata vitu ambavyo huna eti ili ndio utoe mchango wako kusaidia watu na kuibadili nchi yako au hata dunia. Tumia kile ulichonacho na kile unachopata kwa kadiri kinavyojitokeza.

Mungu kamjalia kila mtu kitu Fulani, wengine wana fedha, wengine wana vyeo, wengine wana Mali, wengine wana vipaji mbalimbali ila hata kwa yule ambaye kakosa vyote hivyo, angalau ana akili. Tumia chochote ulicho nacho bila kujali ni nini na cha ukubwa gani kusaidia kujenga ustaarabu, utu na ustawi Wa mwanadamu kwenye nchi yako. Wakati ni sasa, hakuna wakati mwafaka zaidi ambao utajitokeza. Ni pale ambapo kila mtu atatia jitihada za kufanya hivyo: tutaweza kujenga nchi yenye ustawi Wa kweli.

Fikra, malengo na matendo yoyote yasiyolenga kwenye kusaidia kujenga ustaarabu na utu; hutokana na fikra za kishetani, na hakuna nchi wala jamii yoyote inayoweza kustawi kwa mawazo hayo.

Sisi watanzania ndio tutaamua hatma ya Tanzania tukianza na wewe unayesoma hapa. Anzia ulipo kwa kile ulichonacho kutoa mchango wako kuhakikisha Tanzania unayoitaka inakuwa.
 
'Nanliu hole' countries ni adimu sana kua na siasa safi
Inawezekana kuwa na siasa safi sana kama tukiweza. Tunaweza kufanya zaidi ya sasa kama tukiamua.Mkuu mtu yoyote akiamua kuwa mtu safi wanaweza, na akiamua kila siku awe bora kuliko Jana anaweza.

Tatizo sisi watanzania kila mmoja huhisi mwenzake ndio tatizo na ndio Mwenye wajibu wakati nchi zilizoendelea kila mtu hujihisi yeye ndiye hasa hupaswa kuubadili ulimwengu.
 
Wanasiasa ni wanafki tu by nature!

Ova
Mkuu hapo ndipo tunapokosea. Mwanadamu yeyote ni mwanasiasa by nature. Ilikuwa hivyo tangu kuumbwa kwa ulimwengu, iko hivyo na itakuwa hivyo hata milele.

Suala tu ni kutofautiana viwango, mazingira na majukumu. Sasa suala la unafiki ni kweli lipo sana tu lakini unapoona hivyo, ujue cases unazozizungumzia ni zao la jamii nafiki.

Suala ni ikiwa unafiki ni maumbile au ni tabia na mtu anaweza kuongeza au kupunguza unafiki akiamua? Duniani kuna vitu viwili viwili. Kila kitu kina mbadala wake. Kwa mfano ukiona mtu kamchagua kuwa na chuki, haimaanishi kuwa hawezi kuchagua kuwa na upendo.
 
Mmea huanzia chini kwenye ardhi, baadae hutengeneza mizizi, kisha huchomoza ardhini, hukuwa, hutoa maua kisha matunda.

Tatizo letu watanzania wengi tuna papara, tunataka tuibuke na kuanza kuchuma matunda.
 
Mkuu hapo ndipo tunapokosea. Mwanadamu yeyote ni mwanasiasa by nature. Ilikuwa hivyo tangu kuumbwa kwa ulimwengu, iko hivyo na itakuwa hivyo hata milele.

Suala tu ni kutofautiana viwango, mazingira na majukumu. Sasa suala la unafiki ni kweli lipo sana tu lakini unapoona hivyo, ujue cases unazozizungumzia ni zao la jamii nafiki.

Suala ni ikiwa unafiki ni maumbile au ni tabia na mtu anaweza kuongeza au kupunguza unafiki akiamua? Duniani kuna vitu viwili viwili. Kila kitu kina mbadala wake. Kwa mfano ukiona mtu kamchagua kuwa na chuki, haimaanishi kuwa hawezi kuchagua kuwa na upendo.
Wanasiasa hawana tofauti na wale madada wa kona bar pale
Mwanasiasa unaweza mnunua kwa njia yoyote ile!

Ova
 
Kitu kinachotusumbua ni unafiki tulionao watanzania hili tatizo likitutoka tutafanya kama ulivyotaka mkuuu.ila kikubwa ni kuwajibika kwa mmoja mmoja ili kuacha alama kwa vizazi vijavyo.
 
Usikae ukasema ipo siku, hiyo siku haitafika! Siku ndio Leo. Amua kuwa badala ya kutykana sasa angalau utakuwa unashauri, badala ya kulalamika angalau utafanya kile kilichoko ndani ya uwezo wako kuchangia kuboresha hali ya mambo.Angalau kwa kuanzia itakuwa sio mbaya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom