Juliana Shonza
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 2,009
- 1,607
Siasa ni mtazamo / dhana za wanasiasa (ama vyama vyao) na mapokeo ya wananchi katika mitazamo na falsafa hizo, ambazo kimsingi ndizo zinatoa mwelekeo na njia za maisha ya watu husika.
Wanasiasa ama labda niseme vyama vya siasa, vinajibainisha na kujitanabaisha kwa watu ama kundi la watu katika taswira fulani ya kuwavutia ili vipate kuungwa mkono na watu hao.
Upinzani ama niweke bayana zaidi, CHADEMA walipoanza siasa walijibainisha kuwa ni Chama cha Vijana, kikasema ajenda za vijana na kutenda matendo yaliyopendwa na Vijana na kikaungwa mkono na Vijana wengi wakati huo.
Vijana wanaathirika zaidi (youth are more influenced na entertainment industry) burudani ni miongoni mwa hitaji la Vijana. Wanamichezo, waigizaji, wanamuziki etc wana influence kubwa kwa jamii, na matendo yao huchukuliwa na jamii hata kufikia kuitwa kioo cha jamii..kwa maana jamii inajigezea na kufuata taswira yao.
Kuelekea Octoba 2015, tayari kundi la wasanii wameendelea kujibainisha kuwa si tu wafuasi wa CCM bali wameweka bayana nia zao za kutaka kuwa viongozi kupitia Chama hiko..hii maana yake nini..? Ni kuwa hakuna tena namna upinzani wakapata kuungwa mkono na vijana ikiwa wamepoteza mafungamano yao na wasanii.
2010, wasanii wa muziki, maigizo etc wote waliibea CHADEMA, Roma Mkatoliki, Afande Sele, Sugu etc waliweka wazi misimamo yao, vijana wakavutiwa nao wakaiunga mkono chadema, 2015 hali ni tofauti kabisa.,wasanii wamehakikisha wanafukia kaburi la upinzani nchini...
Watu wakimuangalia Diamond wanaiona CCM, wakimuangalia Wema wanaiona CCM, wakimuangalia Uwoya and the rest of the team, hawaoni isipokuwa CCM. Followers wao kwenye mitandao wana repost kuhusu CCM, matokeo yake kila unapotazama ni CCM.,upinzani tupa kule na watu wameshaanza kusahau kuwa tuna vyama vingi...masikio yako Dodoma, hawapitwi na taarifa ya habari kujua yanayojiri..
Sio kwa bahati mbaya, SIASA ni CCM, wengine wasindikizaji.
Wanasiasa ama labda niseme vyama vya siasa, vinajibainisha na kujitanabaisha kwa watu ama kundi la watu katika taswira fulani ya kuwavutia ili vipate kuungwa mkono na watu hao.
Upinzani ama niweke bayana zaidi, CHADEMA walipoanza siasa walijibainisha kuwa ni Chama cha Vijana, kikasema ajenda za vijana na kutenda matendo yaliyopendwa na Vijana na kikaungwa mkono na Vijana wengi wakati huo.
Vijana wanaathirika zaidi (youth are more influenced na entertainment industry) burudani ni miongoni mwa hitaji la Vijana. Wanamichezo, waigizaji, wanamuziki etc wana influence kubwa kwa jamii, na matendo yao huchukuliwa na jamii hata kufikia kuitwa kioo cha jamii..kwa maana jamii inajigezea na kufuata taswira yao.
Kuelekea Octoba 2015, tayari kundi la wasanii wameendelea kujibainisha kuwa si tu wafuasi wa CCM bali wameweka bayana nia zao za kutaka kuwa viongozi kupitia Chama hiko..hii maana yake nini..? Ni kuwa hakuna tena namna upinzani wakapata kuungwa mkono na vijana ikiwa wamepoteza mafungamano yao na wasanii.
2010, wasanii wa muziki, maigizo etc wote waliibea CHADEMA, Roma Mkatoliki, Afande Sele, Sugu etc waliweka wazi misimamo yao, vijana wakavutiwa nao wakaiunga mkono chadema, 2015 hali ni tofauti kabisa.,wasanii wamehakikisha wanafukia kaburi la upinzani nchini...
Watu wakimuangalia Diamond wanaiona CCM, wakimuangalia Wema wanaiona CCM, wakimuangalia Uwoya and the rest of the team, hawaoni isipokuwa CCM. Followers wao kwenye mitandao wana repost kuhusu CCM, matokeo yake kila unapotazama ni CCM.,upinzani tupa kule na watu wameshaanza kusahau kuwa tuna vyama vingi...masikio yako Dodoma, hawapitwi na taarifa ya habari kujua yanayojiri..
Sio kwa bahati mbaya, SIASA ni CCM, wengine wasindikizaji.