Siasa: April 2020 imebeba ujumbe mzito!

Nguruvi3

Platinum Member
Jun 21, 2010
15,407
31,392
Katika aliyofanya Rais SSH tangu achukue madaraka ni 'kuacha watu waonge' .

Rais alisema watu wakiongea viongozi wanaelewa nini kinaongelewa.
Katika kufungua uhuru wa maoni/habari uliofinyangwa miaka sita amefanya vizuri.

Kwa hatua hiyo Rais anapata faida ya ziada ya kuelewa kilichopo akilini na miyooni mwa jamii anayoisimamia kama kiongozi mkuu.

Mwezi April una matukio kadhaa yanayohitaji tuyaangalie kwa jicho pana kuyaelewa

Mkutano Mkuu wa CCM:
Uliandaliwa kumchagua makamu Tanzania Bara baada ya mzee Mangula kung'atuka. Komredi Kinana alichukua nafasi akitoka kwenye maumivu makali ya awamu ya tano ya kudhalilishwa illiyoshindwa kujali , kuthamini au kuheshimu kazi za Wazee na wanachama

Wazee wengi sana wa Chama walihudhuria mkutano wakiwa na furaha ikieleza jambo.

Kubwa ni kwa katibu mkuu wa zamani Yusuf Makamba kutema nyongo akisema ''.... wasamehe wewe ndio bosi wao sasa''
Makamba anamwambia Kinana awasamehe 'Timu JPM' iliyoongoza kwa mkono wa chuma

Komredi Kinana akishukuru wajumbe aliwaasa viongozi kutokuwa na majigambo, kuwa wanyenyekevu na kuwa watumishi. Ujumbe ulilenga JPM na timu yake ''inner circle''

Mkutano wa TCD:
Ni mkutano wa wadau wa Demokrasia. Katika yaliyojiri ni kusemwa wazi kwa utawala wa JPM, likifanywa na viongozi wa siasa, dini. wazee Wastaafu na Wasomi

Ni ujumbe ulioashiria nchi haikuwa katika mstakabali mzuri miaka michache iliyopita.

Ufunguzi wa Chuo cha CCM:
Tukio hilo limeambatana na uzinduzi wa vitabu vilivyomhusu Mwalimu Nyerere.

Washiriki walimweleza Mwalimu Nyerere kadri walivyomfahamu

Tukio moja ambalo wengi hawakuliona kwa urahisi au kulielewa kama lilivyotokea ni la mchangia mada mwandishi Aboubakar Lyongo aliyeongea kwa niaba ya vijana

Katika kuchangia Bw Lyongo alizungumzia udini, ukabila na ukanda akisema miaka ya karibuni tumerudi nyuma. Hakuna shaka Bw Lyongo alizunguzia utawala wa JPM

Mtoto wa Mwalimu Nyerere Bwa Makongoro (RC Manyara) alieleza kwamba Nyerere alipendwa kwasababu ya ''Ubinadamu'' .

Reactions (mwitikio) wa Wananchi ni makofi mazito ya dhati ya kukubaliana na Makongoro. Hapa palikuwa na ujumbe pia Katika yaliyolalamikiwa utawala wa JPM ni haki za binadamu

Rais SSH alipo ongea alipita kule kule alikoanzia Bw Lyongo tena akimnukuu.
Rais alisema tuna kazi ya kufanya kufuta mambo ya udini, ukanda na ukabila yaliyojitokeza miaka ya karibuni. JPM ananyooshewa vidole na aliyekuwa Msaidizi wake.

Je, bado kuna shaka ya tuhuma Udini, Ukanda na Ukabila?

Ukichukua matukio matatu ya mwezi huu, hadhra na watu walioongelea hakuna shaka miaka awamu ya tano ilipanda mbegu mbaya nchini

Jamii inaonyesha kutoridhishwana Taifa lilipopitia katika utawala wa Rais JPM kijamii

Serikali ya JPM imeonyooshewa vidole siyo na Wapinzani ambao huonekana kama 'wasema hovyo'' bali Wanachama wa CCM, viongozi wa Dini, Wazee Wastaafu na Wasomi

Kazi ya kuturudisha katika mstari si rahisi kwani 'mbegu' ilishapandwa na kuchanua.
Ingawa mbegu bado ni changa kuiondoa itachukua muda na jitihada za dhati kwetu sote

Rais SSH aungwe mkono, tuondoe na kuwazomea waliotaka kutupoteza

Tukemee yasijirudie tena kama yale ya 'kueleza kanda fulani itusubiri''

Hatuwezi kuponya majeraha kwa kukaa kimya au kusingizia mtu.

Jambo muhimu ni kuweka rekodi sawa na zisemwe wazi ili tujue ni akina nani , kwa njia gani wakifanya nini na kusaidiwa na nani walitaka taifa letu ligawanyike kwa misingi mibaya

Tusemezane
 
Ujumbe wa April : CAG , CCM

April imeendelea kuwa mwezi wenye ujumbe kwa namna tofauti

Taarifa ya CAG ikigonganisha vichwa kwa 'madudu' yanayochefua
Ripoti haina tofauti na zile za wakati wa CAG Assad Musa kwa uwazi wake

Ujumbe unaopatikana ni kuwa miaka iliyopita baada ya CAG kuondolewa uhaguzi ulifanywa kwa kutazama 'mkubwa' alitaka kuona nini , kipi kismwe na kipi kiwekwe chini ya Zulia

Kuna uwezekano kabisa taarifa imewekwa wazi Wananchi waone mchwa wanavyosakata gunia la rasilimali za Taifa kukiwa hakuna uhaba wa nyongeza za kodi na tozo.

Wapo wanaosema 'mchwa' wamerudi kazini. Hilo si kweli, awamu ya JPM mengi yalifichwa

CCM
Katika hali isiyokuwa ya kawaida ujumbe wa April unazidi kubeba mithili ya kokoro

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza amenukuliwa akiwaasa CCM waache wizi wa kura

Mwenyekiti amesema CCM haiwezi kuendelea kutegemea Polisi katika kupata ushindi
Alikwenda mbali na kutaja maeneo CCM waliposhindwa lakini wakashinda kwa nguvu ya Polisi

Mwenyekiti aliwahi kuingia matatani kwa kauli ya kutaka ''viongozi wachunguzwe kwani wapo waliokuwa na mafaili Mirembe''

Duru zinabainisha Mwenyekiti alikuwa mwathirika wa kibiashara miaka 6 iliyopita

Pamoja na yote alichosema Mwenyekiti kina ukwel

Uchaguzi wa 2020 haukuwa uchaguiz kwa maana ya uchaguzi.

Kule Hai Polisi alimwambia mgombea ''wewe hushindi atashinda wa CC'' .

Jambo la kushangaza ni Polisi kabakia kazini licha ya kukiuka taratibu za kazi na sheria.

Tulishuhudia uchaguzi wa serikali za mitaa ulivyochafuliwa na CCM.

Tukashuhudia Mahakama kuu ikitoa hukumu ya kutetea Wakurugenzi kusimamia uchaguzi.

Hukumu hiyo tata ilisema kuwa '' Wakurugenzi wanaapishwa '' na hivyo watatenda haki!

Ni hukumu iliyotia simanzi Taifa kwa kuelewa hakuna pa kukimbilia na haki ipo njia panda

Ni kwa kuelewa hivyo uchaguzi wa 2020 Mahakama kuu haikupata lalamiko, si kwasababu hayakuwepo bali ilionekana haki ya uchaguzi haitapatikana Mahakamani.

Jambo hilo limeondoa shaka kuhusu 'uhuru' wa mahakama. Mahakama imeonyooshewa vidole kama sehemu inayotakiwa kufumuliwa na kusukwa isiingiliwe katika katiba mpya

Imani kwa mhimili huo wa sheria imeshuka na kufikia kiwango cha chini sana

Alichosema Mwenyekiti wa mkoa wa Mwanza aliwahi pia kusema Rais Kikwete

Tofauti iliyopo sasa ni kwamba watu wanatema nyongo zao! ili wapumue baada ya miaka 6

Tusemezane
 
Wazee wengi sana wa Chama walihudhuria mkutano wakiwa na furaha ikieleza jambo.



Tusemezane
Leo tunataka tutumie FURAHA ya wastafu wa CCM kutambua Ustawi wa Taifa uko salama, na hudhuni yao ni Taifa liko hatarini.

Ni mpaka siku tutapotambua Gharama Sahihi za Matamanio Yetu, na kuwa tayari kuzilipa.

Wengine tutasubiri bado nafasi nyingine, Nanyi mjipongeze kwa Taifa kurudi kwenye mikono salama. Hongereni sana.
 
Leo tunataka tutumie FURAHA ya wastafu wa CCM kutambua Ustawi wa Taifa uko salama, na hudhuni yao ni Taifa liko hatarini.

Ni mpaka siku tutapotambua Gharama Sahihi za Matamanio Yetu, na kuwa tayari kuzilipa.

Wengine tutasubiri bado nafasi nyingine, Nanyi mjipongeze kwa Taifa kurudi kwenye mikono salama. Hongereni sana.
Kuna kueleza jambo kama unavyoliona halafu kuna kueleza jambo kwa maana iliyokusudiwa
Nimeeleza kama nilivyoona, kwamba, Wastaafu na Wazee wa CCM walikuwa na furaha
Sijaeleza furaha yao ni ya nini lakini kwa aliyeangalia mkutano ule walikuwa na furaha

Hata hivyo una haki ya maoni,hakuna maoni sahihi au potofu na siwezi kujibu maoni yako
Ninachoweza kufanya ni kueleza kilichoandikwa
 
Kuna kueleza jambo kama unavyoliona halafu kuna kueleza jambo kwa maana iliyokusudiwa
Nimeeleza kama nilivyoona, kwamba, Wastaafu na Wazee wa CCM walikuwa na furaha
Sijaeleza furaha yao ni ya nini lakini kwa aliyeangalia mkutano ule walikuwa na furaha

Hata hivyo una haki ya maoni,hakuna maoni sahihi au potofu na siwezi kujibu maoni yako
Ninachoweza kufanya ni kueleza kilichoandikwa
Mpaka unauliza wanajamvi kama kuna yeyote mwenye shaka juu ya Tuhuma za Udini, Ukanda na Ukabila, bado tu unataka kujitoa miongoni mwa wale wenye FURAHA sawa na wazee wa CCM?

Mbali zaidi ukahitimisha kwa kusema Hakuna Shaka kuwa awamu ya tano ilipanda mbegu mbaya nchini. Bado unadai hu miongoni mwao wakenuao meno wakati huu?

Tunajua in Upinzani+CCM Vs Magufuli. Jamii haikuwahi kuwa kinyume na Magufuli, ila ni huo muungano wa TimuMaslahi.

JIPONGEZENI, KWA MAANA MMESHINDA. Nasi tutaendelea kuomboleza na labda sauti yetu Itasikika Tena. Tumaini lipo.
 
Mpaka unauliza wanajamvi kama kuna yeyote mwenye shaka juu ya Tuhuma za Udini, Ukanda na Ukabila, bado tu unataka kujitoa miongoni mwa wale wenye FURAHA sawa na wazee wa CCM?
Kuna hoja mbili, usichanganye. Moja, kuhusu Wazee niliwaona wanafuraha!

Pili, kuhusu tuhuma za udini, ukanda na ukabila nilisema na majuzi makundi mbali mbali ya viongozi akiwemo Mh Rais walikemea hali hiyo miaka ya karibuni.
Sasa kama unataka tuwe na mjadala wa hili nipo tayari kutetea hoja yangu
Mbali zaidi ukahitimisha kwa kusema Hakuna Shaka kuwa awamu ya tano ilipanda mbegu mbaya nchini. Bado unadai hu miongoni mwao wakenuao meno wakati huu?
Hili nalo kama unataka mjadala tafadhali jenga hoja nami nitatetea zangu
Tunajua in Upinzani+CCM Vs Magufuli. Jamii haikuwahi kuwa kinyume na Magufuli, ila ni huo muungano wa TimuMaslahi.
Jamii ni neno pana, hao Wapinzani na CCM ni jamii pia , jamii unayozungumzia ni ipi?
JIPONGEZENI, KWA MAANA MMESHINDA. Nasi tutaendelea kuomboleza na labda sauti yetu Itasikika Tena. Tumaini lipo.
Maoni yako tunayaheshimu
 
Kuna hoja mbili, usichanganye. Moja, kuhusu Wazee niliwaona wanafuraha!

Pili, kuhusu tuhuma za udini, ukanda na ukabila nilisema na majuzi makundi mbali mbali ya viongozi akiwemo Mh Rais walikemea hali hiyo miaka ya karibuni.
Sasa kama unataka tuwe na mjadala wa hili nipo tayari kutetea hoja yangu

Hili nalo kama unataka mjadala tafadhali jenga hoja nami nitatetea zangu

Jamii ni neno pana, hao Wapinzani na CCM ni jamii pia , jamii unayozungumzia ni ipi?

Maoni yako tunayaheshimu
Hoja ni Moja tu Mkuu, kwamba Taifa limerejea kuwa na FURAHA baada ya kipindi kibaya cha Magufuli; Ufisadi, Wizi, Udini, Udini, Uminywaji wa Demokrasia, Inhumanity, Uhuru,nk...
Hiyo ndiyo Hoja yako Kuu. Ni kutuambia kuwa sasa Taifa lipo kwenye Mikono Salama, na Tujivunie hasa kwa hilo.

Umeitaja jamii yako, kuwa ni Wasomi, wanaCCM, wapinzani, viongozi wa dini, nk.. Kama ni hayo basi uko Sahihi kwa upande wako.

Ila, Jamii nayoisemea mimi ni ile inayohudumiwa na hayo makundi ya mchwa uliyoyataja. WATEJA wa hayo makundi yako. Kundi hili hatuna Kinyongo na Magufuli, na Tutamkumbuka sana na Hatutaacha Kuomboleza. Haijalishi ninyi wasomi, wanaCCM, wapinzani, na wanadini mtasemaje.
 
Awali ya yote napenda nikuase yafuatayo
1. Ukiingia katika mjadala kwa ghadhabu utapoteza ulichokusudia kusema ghadhabu zitatawala fikra

2. Kuna maoni (opinion) na facts (ukweli) ambavyo ni vitu tofauti.
Maoni yako tunayaheshimu lakini siyo facts.
Na facts zinabaki kuwa hivyo iwe iwavyo haiangalii mtu anapenda nini

Usichukue maoni yako ukayafanya maoni yangu kwasababu unadhani ni hivyo.

Tafsri ipo kwa msomaji na usijaribu ku-construe maana iliyokusudiwa ku fit narrative yako.
Hoja ni Moja tu Mkuu,
Ni hoja yako unayojadili si yangu
kwamba Taifa limerejea kuwa na FURAHA baada ya kipindi kibaya cha Magufuli; Ufisadi, Wizi, Udini, Udini, Uminywaji wa Demokrasia, Inhumanity, Uhuru,nk...Hiyo ndiyo Hoja yako Kuu.
Hakuna mahali nimeandika maneno hayo na kama ipo lete nukuu.
Kama huna nukuu acha kuzua mambo kwa vile tu unataka. Narudia hakuna mahali nimeandika hayo maneno
Ni kutuambia kuwa sasa Taifa lipo kwenye Mikono Salama, na Tujivunie hasa kwa hilo.
Hakuna mahali nimeandika hayo maneno. Kama ni maana yako sema ni maoni yako
Sijasema hata neno moja, lete nukuu kama ipo. Maana yako ni tafsiri yako
Umeitaja jamii yako, kuwa ni Wasomi, wanaCCM, wapinzani, viongozi wa dini, nk.. Kama ni hayo basi uko Sahihi kwa upande wako.
Sijataja jamii kwasababu naiangalia jamii kwa ukubwa wake.

Wezi, wafungwa, wachawi , wasomi, wakulima, wafanyakazi, wazururaji, n.k. ni sehemu ya jamii. Hatuwezi kuwa na jamii ya makundi!uliyoandika ni maneno kwa maana yako si yangu
Ila, Jamii nayoisemea mimi ni ile inayohudumiwa na hayo makundi ya mchwa uliyoyataja.
OK kama una jamii hewala. Makundi mchwa ni yapi? again maoni na tafsiri yako maana yangu
WATEJA wa hayo makundi yako.
Hata sijui una maana gani, punguza ghadhabu ili tukuelewe.
Kundi hili hatuna Kinyongo na Magufuli, na Tutamkumbuka sana na Hatutaacha Kuomboleza.
Hiyo ni hiari ya kila mtu kumtazama JPM kwa jicho lake, hata hivyo mtazamo wako si lazima uwe sahihi na wala wa mwingine si lazima uwe sahihi kwako.

Kilicho muhimu ni kuheshimu mitazamo mingine hata kama inakwaza
Haijalishi ninyi wasomi, wanaCCM, wapinzani, na wanadini mtasemaje.
Haya ni maoini yako mazuri tu tunayaheshimu hatuhitaji kuyajadili
 
Awali ya yote napenda nikuase yafuatayo
1. Ukiingia katika mjadala kwa ghadhabu utapoteza ulichokusudia kusema ghadhabu zitatawala fikra

2. Kuna maoni (opinion) na facts (ukweli) ambavyo ni vitu tofauti.
Maoni yako tunayaheshimu lakini siyo facts.
Na facts zinabaki kuwa hivyo iwe iwavyo haiangalii mtu anapenda nini

Usichukue maoni yako ukayafanya maoni yangu kwasababu unadhani ni hivyo.

Tafsri ipo kwa msomaji na usijaribu ku-construe maana iliyokusudiwa ku fit narrative yako.

Ni hoja yako unayojadili si yangu

Hakuna mahali nimeandika maneno hayo na kama ipo lete nukuu.
Kama huna nukuu acha kuzua mambo kwa vile tu unataka. Narudia hakuna mahali nimeandika hayo maneno

Hakuna mahali nimeandika hayo maneno. Kama ni maana yako sema ni maoni yako
Sijasema hata neno moja, lete nukuu kama ipo. Maana yako ni tafsiri yako

Sijataja jamii kwasababu naiangalia jamii kwa ukubwa wake.

Wezi, wafungwa, wachawi , wasomi, wakulima, wafanyakazi, wazururaji, n.k. ni sehemu ya jamii. Hatuwezi kuwa na jamii ya makundi!uliyoandika ni maneno kwa maana yako si yangu

OK kama una jamii hewala. Makundi mchwa ni yapi? again maoni na tafsiri yako maana yangu

Hata sijui una maana gani, punguza ghadhabu ili tukuelewe.

Hiyo ni hiari ya kila mtu kumtazama JPM kwa jicho lake, hata hivyo mtazamo wako si lazima uwe sahihi na wala wa mwingine si lazima uwe sahihi kwako.

Kilicho muhimu ni kuheshimu mitazamo mingine hata kama inakwaza

Haya ni maoini yako mazuri tu tunayaheshimu hatuhitaji kuyajadili
1. Sijui ni nini kinakufanya uone kwamba nimeghadhibika katika hoja! Isije ikawa unasemea nafsi yako ilivyo huko. Ni mtazamo wako, na uheshimiwe pia.

2. Ndio, facts haziwezi kuwa manipulated na chochote... Iwe ni kundi la wasomi, viongozi wa dini au wanasiasa. Haijalishi ni nguvu gani wataitumia. Ndio maana tunawaambia Hongereni sana.

3. Wewe ni bingwa wa kukana matamshi yako, sikushangai. Umetoa wito wa Kumuunga Mkono Mama Samia baada ya tuhuma dhidi ya Awamu iliyopita. Sasa nikuulize, Kama Taifa haliko katika Mikono Salama unataka Tuunge Mkono nini? Kama hukumaanisha hivyo basi utusaidie kujua.

4. Rudi kwenye post yako #1 aya ya 20 na 21 uzifute, halafu uandike tena kutuambia kutuambia hakuna sehemu umetaja jamii. Au utolee ufafanuzi kuwa kwanini huwa huoni aibu kukana matamshi yako.

5. Makundi Mchwa ni mtazamo wangu juu ya makundi uliyoyataja wewe kuwa wameoneshwa kutoridhishwa na awamu ya tank ;Wapinzani+CCM, Viongozi wa Dini na Wasomi. Hakika ni Mtazamo wangu, kama nawe ulivyo nao kwao.

6. Je, ni kweli hujui Mteja wa Mwanasiasa ni nani, Mteja wa Kiongozi wa Dini ni nani, Mteja wa Msomi ni Nani, Mteja Viongozi wa Umma ni nani? Punguza jazba kuelewa vizuri.

7. Ni we we ndio umetaja makundi, sio Mimi. Unataka na hili ukumbushwe? Mimi nimetaja neno moja tu kutafsiiri jamii, MTEJA/CUSTOMER.

8. Yap, kila mtu ana Uhuru wake juu ya kumtazama JPM. Na hicho ndicho kinachofanyika. Sifikiri kama nimetoka nje ya hilo. Nisahihishwe.

Sijajua kwanini umekuwa MTU wa kurudiarudia hoja ya kuheshimiwa mtazamo wako, nani amevunjia heshima mtazamo wako kwani? Ungetaja hili au hili limenivunjia heshima, binafsi ningekuomba radhi bila shaka.

Acha mchezo wa Ku act innocence katika mjadala.

SISI TUTAOMBOLEZA MPAKA PALE SAUTI YETU ITAKAPOSIKIKA TENA. NANYI HONGERENI SANA.
 
.

3. Umetoa wito wa Kumuunga Mkono Mama Samia baada ya tuhuma dhidi ya Awamu iliyopita. Sasa nikuulize, Kama Taifa haliko katika Mikono Salama unataka Tuunge Mkono nini? Kama hukumaanisha hivyo basi utusaidie kujua.
Ungechukua nukuu nzima ! unapotosha. Nilichosema ni kuhusu udini, ukanda na ukabila nikimnukuu Abubakar Lyongo na Rais SSH ambaye ni msaidizi wa JPM
Kwa kukemea ukabila , ukanda na udini tunapaswa kumuunga mkono! Yes aungwe mkono
5. Makundi Mchwa ni mtazamo wangu juu ya makundi uliyoyataja wewe kuwa wameoneshwa kutoridhishwa na awamu ya tank ;Wapinzani+CCM, Viongozi wa Dini na Wasomi. Hakika ni Mtazamo wangu, kama nawe ulivyo nao kwao.
Sina tatizo na mtazamo wako, naheshimu maoni yako
6. Je, ni kweli hujui Mteja wa Mwanasiasa ni nani, Mteja wa Kiongozi wa Dini ni nani, Mteja wa Msomi ni Nani, Mteja Viongozi wa Umma ni nani? Punguza jazba kuelewa vizuri.
Ni mtazamo wako, sina tatizo na tafsiri yako
8. Yap, kila mtu ana Uhuru wake juu ya kumtazama JPM. Na hicho ndicho kinachofanyika. Sifikiri kama nimetoka nje ya hilo. Nisahihishwe.
Basi panapokukera onyesha tujadili. Nime ku challenge kuwa tujadili unacholalamikia, umekimbi
SISI TUTAOMBOLEZA MPAKA PALE SAUTI YETU ITAKAPOSIKIKA TENA. NANYI HONGERENI SANA.
Kwanza pole sana , pili maoni yako hayajadiliwi ni yako
 
Ungechukua nukuu nzima ! unapotosha. Nilichosema ni kuhusu udini, ukanda na ukabila nikimnukuu Abubakar Lyongo na Rais SSH ambaye ni msaidizi wa JPM
Kwa kukemea ukabila , ukanda na udini tunapaswa kumuunga mkono!
Kwenye Ujumbe wako wa April-2022, Mimi nimeona Tuhuma dhidi ya Utawala wa Magufuli, na Matumaini mapya juu ya Utawala Samia.

Tuhuma hizo ni juu ya Udini, Ukabila, Ukanda, Ubadhirifu, Ukiukwaji wa Haki, Uminywaji wa Uhuru, nk...

Nimeona Tumaini pia kwa Kutoa kwako Wito wa kuunga mkono awamu hii Leo. Namna ya rejea yako ya report ya CAG kushibisha Tuhuma zako. FURAHA za wastaafu na wanaCCM katika awamu hii ikiashiria Tumaini jipya.

Juu ya Tuhuma zako nimesema "Ni mpaka pale tutakapotambua Gharama halisi za Matamanio Yetu"

Na juu ya Tumaini mlilo nalo nimesema "Hongereni Sana, ila Sisi bado Tutaomboleza"

Bado nasimama katika hayo kwa sasa.
 
Tuhuma hizo ni juu ya Udini, Ukabila, Ukanda, Ubadhirifu, Ukiukwaji wa Haki, Uminywaji wa Uhuru, nk...
Kwa mtazamo wako ambao si lazima uwe na makosa au uwe sahihi
Nimeona Tumaini pia kwa Kutoa kwako Wito wa kuunga mkono awamu hii Leo.
YES, kuunga mkono jitihada za kupinga ukabila, ukanda na udini aliousema Rais SSH
Haya ni mambo yanayoligawa Taifa letu, na hakuna kuomba radhi katika kuyakemea!
Namna ya rejea yako ya report ya CAG kushibisha Tuhuma zako.
Kwa mtazamo na tafsiri yako , tunakubali maoni yako. Ni maoni yako
FURAHA za wastaafu na wanaCCM katika awamu hii ikiashiria Tumaini jipya.
Haikuwaepo shaka Wazee walikuwa na furaha, sasa kama hukuona wanafuraha hilo nalo ni mtazamo wako. Unaweza kueleza ikiwa walikuwa na huzuni ili nasi tufaidike na mtizamo wako
Juu ya Tuhuma zako nimesema "Ni mpaka pale tutakapotambua Gharama halisi za Matamanio Yetu"
Sijui una maana gani! sorry
Na juu ya Tumaini mlilo nalo nimesema "Hongereni Sana, ila Sisi bado Tutaomboleza"
Mlilo nalo akina nani hao! again kwanini tujibu maoni yako
Bado nasimama katika hayo kwa sasa.
Simama kwa yote unayodhani ni sahihi kwa mtazamo wako ni haki yako!
Mtazamo wako usifunge macho na mitazamo ya wengine
 
Sijui una maana gani! sorry
Kutokujua kwako, ndipo Tatizo linapoanzia, na mpo wengi sana. Kaeni Chini mfanye Tafakari vizuri, labda IPO siku tutaimba wimbo mmoja.

"MLILO NALO.... " Wewe si mtu wa kwanza kumsikia juu ya tuhuma hizi, hivyo tambua mko wengi sana. Wengine umewataja mwenyewe(Wastaafu, Wapinzani, wanaCCM, wasomi, nk)

Najua pia upande Wetu tu wachache mno.
 
Kutokujua kwako, ndipo Tatizo linapoanzia, na mpo wengi sana. Kaeni Chini mfanye Tafakari vizuri, labda IPO siku tutaimba wimbo mmoja.
Kauli yako nisiyoielewa hapo awali ni hii ''Juu ya Tuhuma zako nimesema "Ni mpaka pale tutakapotambua Gharama halisi za Matamanio Yetu''

Nauliza ndio kitu gani unazungumzia hapa?
"MLILO NALO.... " Wewe si mtu wa kwanza kumsikia juu ya tuhuma hizi, hivyo tambua mko wengi sana. Wengine umewataja mwenyewe(Wastaafu, Wapinzani, wanaCCM, wasomi, nk)
Najua pia upande Wetu tu wachache mno.
Rais SSH ametoa kauli kuhusu udini, ukanda na ukabila akishadidia kauli ya Abubakar Lyongo
Kumbuka Samia ni Rais wa JMT na VP wa JPM ambaye ni msaidizi mkuu.

Pili hatuwezi kuwa na mjadala usio na ''substance' nimesema hivi changua tuhuma moja baada ya nyingine tuidadavue, hutaki! unaujua ukweli na wewe ni wale wa ''marehemu' hasemwi!

Chagua tuhuma moja tu tuijadili tafadhali
 
Kauli yako nisiyoielewa hapo awali ni hii ''Juu ya Tuhuma zako nimesema "Ni mpaka pale tutakapotambua Gharama halisi za Matamanio Yetu''

Nauliza ndio kitu gani unazungumzia hapa?

Rais SSH ametoa kauli kuhusu udini, ukanda na ukabila akishadidia kauli ya Abubakar Lyongo
Kumbuka Samia ni Rais wa JMT na VP wa JPM ambaye ni msaidizi mkuu.

Pili hatuwezi kuwa na mjadala usio na ''substance' nimesema hivi changua tuhuma moja baada ya nyingine tuidadavue, hutaki! unaujua ukweli na wewe ni wale wa ''marehemu' hasemwi!

Chagua tuhuma moja tu tuijadili tafadhali
Kudadavua Tuhuma zako ni wajibu wako, Fanya vile inavyokufaa. Mimi nilikuja kutoa pongezi tu kwenu na kusemea maombolezo Yetu pia.

Ajabu ukapanic na kulalama nisizuie maoni ya watu, niheshimu maoni ya watu. Hakika hakuna mahali sijafanya hivyo.
Ibaki hivyo.
 
Kubwa ni kwa katibu mkuu wa zamani Yusuf Makamba kutema nyongo akisema ''.... wasamehe wewe ndio bosi wao sasa''
Makamba anamwambia Kinana awasamehe 'Timu JPM' iliyoongoza kwa mkono wa chuma
Makamba aliongeza kusema kwamba sasa wanalamba asali. Wakati anajua watanzania wengi sana maisha yamekuwa magumu. Yawezekana, ndiyo maana, labda siku hizi Chama kinafanya mikutano ya ndani akifanyi mikutano ya hadhara. Nawaza tu!
 
Mtoto wa Mwalimu Nyerere Bwa Makongoro (RC Manyara) alieleza kwamba Nyerere alipendwa kwasababu ya ''Ubinadamu'' .
Na aliongeza kusema watoto wengi wa viongonzi furusa zinawashukia Kwa sababu ya wazazi wao! Yawezekana hawana uwezo lakini wazazi wakawa kigezo kwa furusa hizo! Labda nilimsikiliza vibaya...nitarejea hotuba yake
 
Rais SSH aungwe mkono, tuondoe na kuwazomea waliotaka kutupoteza
Ndiyo mmefikia hatuna ya kuwaambia watanzania wenzenu kuwa kama walimpenda sana Hayati Magufuli waende Chato wakazikwe Naye? Kumbe Zitto anaweza kuwa amefuata ushauri wako. Na bado unasema kwa sasa mnaondoa mifarakano ndani ya Jamii. Nakushauri, msikilize sana ushauri wa Mh Lusinde alioutoa juzi Kati huko Bungeni Dodoma
 
Ujumbe unaopatikana ni kuwa miaka iliyopita baada ya CAG kuondolewa uhaguzi ulifanywa kwa kutazama 'mkubwa' alitaka kuona nini , kipi kismwe na kipi kiwekwe chini ya Zulia
Tunasubiri Report ya 2022- 2023 Kuona namna Rubi yetu ya thamani ya mamilioni ilivyoweza kufika soko la Dubai kwa kufuata taratibu zote za kifedha na taifa kupata inachostaili.

Hii ni baada ya CAG kutoona kosa lolote kwenye malipo yaliyofanywa na Wizara ya fedha katika mazingira ya kutatanisha kiasi cha Waziri Mkuu kuunda tume kuchunguza hilo. Mambo ni Mengi Ha ha haaaa!
 
Back
Top Bottom