Siamini ninachokiona sasa hivi ITV

Siamini ninachokiona sasa hivi ITV

Nchimbi na Warioba ni sawa na machinga..
biashara zao huangalia upepo unakovumia..
 
Ameoneshwa pia TBC ila sioni kwanini mtukane kwani aliko ni chama chake na amefika hapo alipo kwa kupitia hicho chama, huo ndo ukomavu wa kisiasa ..hongera sana nchimbi kwa kuonesha ukomavu na subira, usiwe kama wataka yote kwa pupa
 
MNANSO, usishangae sana relax kabisaaa.Siasa zetu ndivyo zilivyo. Wengi wao wanasiasa wetu wanaweka matumbo mbele akili nyuma. Hakuna cha kushangaa, ndivyo ilivyo, kwanza ni mwanaccm mwache ni haki yake kumnadi mgombea wa chama chake. Mengine waachie wanasiasa, siku zote wanajiangalia wao halafu wananchi na nchi baadae. Hakuna uadui wala urafiki wa kudumu katika siasa. Tanzania aslimia kubwa ya wanasiasa wana misimamo feki. Usiamini na kuwaamini sana.utakuwa unapoteza kani. Hakuna namna na hana namna. Tumbo kwanza, mengine baadae.
 
Last edited by a moderator:
Nchimbi ni mpuuzi alikuwa jasiri kuonesha tofauti wazi wazi. Anapobadilika overnight kila mtu anamshangaa. Anaomba nafasi lkn he is hopeless....ndiyo alikuwa waziri wetu tena Home Affairs!!!
Chama kwanza mtu baadaye ,alikuwa anamuunga mkono Lowassa alipokuwa CCM,akiamini kuwa ni haki yake kumuunga mkono anayemtaka,lakini si kuwa kama tuxedo ya Lowassa eti kwa kuwa Lowassa kaondokaCCM basi nae Nchimbi amfuate huko alikoenda,Uwezo wa Nchimbi ni tofauti na uwezo wa akina Mngeja,Mahanga,Ole Medei,Msindai ambao ni chooni tu ndio wanashindwa kumfuata mheshimiwa,au mlidhani ndio atakuwa kati ya wabunge 50 ambao mlidanganywa na aliyekatwa kuwa atahama nao.
 
Nchimbi ni mwaminifu kwa chama chake cio kama wale wanaokatwa majina na kuhama ili wapate madaraka

Ukiona uliyemkosea kakimbia jua uko salama lakini akikaa karibu na wewe anatafuta njia sahihi ya kikumaliza kabisa
 
hayo tumuachie mwenyewe..
ninachotaka CCM walipe mahindi waliyotukopa..
hatuhitaji kingine kwa sasa.
 
Hiyo ITV ni yako oeke yako ,maana mimi nimeangalia itv cjaona sehem nchimbi kamnadi magufuli

We nae...labda ulipata tangazo toka studio za macho yako ndugu huo muda wanaonesha.
 
Yeye alipinga Lowassa kukatwa akijua Membe angepeta, baada ya Membe kushindwa karidhika.
 
Aisee mh Emanuel Nchimbi anamnadi Magufuli na kusema hakuna rais atakae faa kama magufuli.nimeshangaa sana

Emanuel Nchimbi ni mtu anayependa madaraka mno,kwa wale waliosoma Sangu Secondary, Mzumbe university ktk vipindi alivyokuwepo Nchimbi watanielewa.Mzumbe university aliwahi kuwa Waziri wa elimu ktk Serikali ya wanachuo chini ya Raisi Mr Mbwasi,Kipindi cha Mbwasi kilivyoisha Nchimbi aligombea Uraisi kwa kumkejeri na kumdharau Mbwasi mnoo,ili apate Uraisi.Alikosa Uraisi ila alitupa fundisho kuwa ni kigeugeu,Mnafiki na atafanya lolote kupata madaraka! That is Nchimbi that I know.
 
Aisee mh Emanuel Nchimbi anamnadi Magufuli na kusema hakuna rais atakae faa kama magufuli.nimeshangaa sana

Unashangaa nini.
Mbona hushangai waliokuwa wanamwita Lowassa fisadi na kumtukana matusi mabaya hadharani sasa hivi wanamnyenyekea na kumwita mwokozi..mtume...yesu..mussa...etc?
 
Unashangaa nini.
Mbona hushangai waliokuwa wanamwita Lowassa fisadi na kumtukana matusi mabaya hadharani sasa hivi wanamnyenyekea na kumwita mwokozi..mtume...yesu..mussa...etc?

hawa wenzetu bavicha akili sijui wamepeleka wapi?
 
Back
Top Bottom