Si riziki

Si riziki

akohi

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2012
Posts
787
Reaction score
527
Salaama wana jf?
Nimepanda mipapai ile ya muda mfupi na nimejitahidi kuhakikisha inapata maji na mbole ya kutosha Ila cha kushngaza naona asilimia kubwa yote ni midume yaani ni ile isiyotoa matunda na nimepanda zaidi ya mashina 50.

Naombeni ushauri wa namna ya kuifanya itoe matunda

AsAnteni!
 
mkuu wala usiumize kichwa.mtafute bwana shamba au afisa kilimo hilo tatizo lako limekwisha.iku hizi science ya kupandikia mbegu inafanyika tena kirahisi tu.nakuhakikishia tena utavuna matunda mengi na matamu sana.wanaokubeza wapotezee,jukwaa huru hili.
 
Ng'oa panda mipapai jike maana hakuna namna ya kuifanya hiyo mipapai itoe matunda ya aina nyingine.

 
Funga gunzi la mahindi tehe tehe niliona kwa bibi hiyo ila nikakosa muda wa kuchunguza kama kweli inafanya kazi hiyo science ya bibi.KWELI MAISHA YA WABONGO KAMA VIDEO.

Umenikumbusha mbali sana....
 
Hiyo iliyokuwa dume imeshakula kwako mkuu haiwezi badilika
 
Ipake pafyumu ili uvutie wadudu wachavushe au kama vipi panda maua yanayonukia kuwavutia wadudu.
 
Funga gunzi la mahindi tehe tehe niliona kwa bibi hiyo ila nikakosa muda wa kuchunguza kama kweli inafanya kazi hiyo science ya bibi.KWELI MAISHA YA WABONGO KAMA VIDEO.

hii kitu ya gunzi nimeisikia tena. Sijajua pana uhusiano gani
 
Back
Top Bottom