Si kila wanachofanya CHADEMA kiko sahihi

Si kila wanachofanya CHADEMA kiko sahihi

IKIRIRI

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2018
Posts
2,734
Reaction score
3,027
Jamii forum naamini ni platform inayotumiwa na wasomi kutoa mawazo yao kuliko sehemu yoyote ile.

Sisi wengine tunadandia tu ingawa ni haki yetu..BT wengi humu ni graduate+ wachache sana, sisi wa form IV na STD7 wachache.. Kinachonishangaza ni kwann kila jambo wakifanya CHADEMA hata kama sio sahihi linasapotiwa sana. Na yeyote atakayetoa mawazo mbadala atatukanwa na kukejeliwa sana..

Hii tafsiri yake nini?

Ukitoa mada kuhusu CCM ni kejeli tupu hata km ni jambo jema. Kwangu Mimi hii haiko sawa. Kila upande unafanya makosa kwa namna yake. Pia makosa ya wengine wasibebeshwe wengine. MTU anasema hao CCM wanaua...hii si kweli sababu kama kosa limefanywa na dola yaani polisi chama kinausikaje...?

Tusikilize mawazo ya wengine sio kukashifu kwa kejeli....
 
Naomba nikuweke sawa,waliopo wengi jamii forum ni std 7 pamoja na form 4. pili unavozungumzia dola unatakiwa kujua dola inaongozwa na chama gani ndio utajua kwann watu wanailamu ccm kwa kila kosa linalofanywa na dola.
Sina fact juu idadi ya member jamii forum ni wa elimu gani BT kwa mda nilionao humu nikisoma comments nahisi wengi ni wasomi graduate+...km usemalo ndio iko hivyo thanks kwa kunielewesha....then km unawalaumu CCM unawaacha VP CHADEMA chanzo cha hizo mambo?
 
kama ni msomaji wa comment utagundua watu wengi huwa wanachangia nje ya mada hii inatikana na uelewa mdogo juu ya mada (elimu). Chadema nao wanastahili lawama kwa upande flani lkn kabla ya kuwalaumu unatakiwa kujua sababu ya wao kuwa chanzo cha matatizo.
 
Uko sahihi mkuu, kuna watu humu wanatamani majanga kama, ukame, magonjwa, vifo, kunyimwa misaada ya nje, nchi yetu kuvamiwa kijeshi, n.k kwa kuwa tu ni wapinzani wa CCM ( serikali), wanatukana wakuu wa nchi kisa tu wao ni chadema.

Inashangaza sana
 
kama ni msomaji wa comment utagundua watu wengi huwa wanachangia nje ya mada hii inatikana na uelewa mdogo juu ya mada (elimu). Chadema nao wanastahili lawama kwa upande flani lkn kabla ya kuwalaumu unatakiwa kujua sababu ya wao kuwa chanzo cha matatizo.
Sikia ndugu....kutoka nje ya mada haimanishi sio msomi...wengi humu wasomi mkuu...then km CHADEMA wanapaswa kulaumiwa kwann MTU akitoa hoja anatukanwa?
 
Sina fact juu idadi ya member jamii forum ni wa elimu gani BT kwa mda nilionao humu nikisoma comments nahisi wengi ni wasomi graduate+...km usemalo ndio iko hivyo thanks kwa kunielewesha....then km unawalaumu CCM unawaacha VP CHADEMA chanzo cha hizo mambo?

Chadema wanaweza kuwa na shida sawa but why ni wao kila siku inawezekana kuna sehemu ni kweli wanaonewa so ni muhimu kusikilizwa

Mfano ishu za form za mkurugenzi kuwapa mawakala wa uchaguzi nadhan kama tume ingekuwa inawapa mapema kusingekuwa na magomvi sasa mkurugenzi anazima simu au hapokei simu mpaka watu waandamane ndio atoe sidhani kama ni sawa
 
Sikia ndugu....kutoka nje ya mada haimanishi sio msomi...wengi humu wasomi mkuu...then km CHADEMA wanapaswa kulaumiwa kwann MTU akitoa hoja anatukanwa?
kama wapo wasomi wanaotukana katika asilimia mia moja basi 25 ndio watukanaji iliobakia wanajua wanachokifanya mtandaoni.


Hoja nyingi zinazotolewa ambazo zinahitaji majibu kutoka chadema zimekuwa zikiwagandamiza ndio maana yote hayo yanatokea unayoyasema.
 
Chadema wanaweza kuwa na shida sawa but why ni wao kila siku inawezekana kuna sehemu ni kweli wanaonewa so ni muhimu kusikilizwa

Mfano ishu za form za mkurugenzi kuwapa mawakala wa uchaguzi nadhan kama tume ingekuwa inawapa mapema kusingekuwa na magomvi sasa mkurugenzi anazima simu au hapokei simu mpaka watu waandamane ndio atoe sidhani kama ni sawa
Kwann uandamane bila kibali na CHADEMA uwa wanajinadi wanafuata utawala wa sheria? Inamaana hakuna njia mbadala hadi waandamane....OK yule diwani aliyekatwa mapanga unailamu VP polisi au CCM wao wamefanya nn? Tusiishi kwa dhana cz km tukienda kwa dhana CHADEMA wanalo la kujibu juu ya kifo cha CHACHA wangwe hadi Leo kimya....dhana zipuuzwe utaratibu ufuatwe...
 
Sina fact juu idadi ya member jamii forum ni wa elimu gani BT kwa mda nilionao humu nikisoma comments nahisi wengi ni wasomi graduate+...km usemalo ndio iko hivyo thanks kwa kunielewesha....then km unawalaumu CCM unawaacha VP CHADEMA chanzo cha hizo mambo?
Uchanzo cha chadema ni wapi?! Kwa mfano maandamano ya kinondoni, chadema wangefanya Je?! Mpaka siku ya mwisho jioni saa 12, bado Mkurugenzi amewanyima viapo vyao vya kuwatambulisha vituoni na kesho yake saa 12 kura zinapigwa, wamefanya Je?!! Wakati huo wenzao wana viapo zaidi ya wiki!!! Kwa nini usione tatizo lilipo?! .

Tundu Lissu alisababishaje kumiminiwa risasi kama chatu?! Na Je Mawazo alifanya nini mpaka acharangwe mashoka, kama nyama buchani?! Hebu eleza chanzo chao cha matatizo

Kuhusu ndege kukamatawa huko Canada Je kosa la CDM ni lipi?! Kwamba wewe hujui alieleteleza hilo deni?! Jibu maswali yangu
 
  • Thanks
Reactions: BAK
kama wapo wasomi wanaotukana katika asilimia mia moja basi 25 ndio watukanaji iliobakia wanajua wanachokifanya mtandaoni.


Hoja nyingi zinazotolewa ambazo zinahitaji majibu kutoka chadema zimekuwa zikiwagandamiza ndio maana yote hayo yanatokea unayoyasema.
Km hoja gani imekosa majibu ufikie kutukana?
 
Uchanzo cha chadema ni wapi?! Kwa mfano maandamano ya kinondoni, chadema wangefanya Je?! Mpaka siku ya mwisho jioni saa 12, bado Mkurugenzi amewanyima viapo vyao vya kuwatambulisha vituoni na kesho yake saa 12 kura zinapigwa, wamefanya Je?!! Wakati huo wenzao wana viapo zaidi ya wiki!!! Kwa nini usione tatizo lilipo?! .

Tundu Lissu alisababishaje kumiminiwa risasi kama chatu?! Na Je Mawazo alifanya nini mpaka acharangwe mashoka, kama nyama buchani?! Hebu eleza chanzo chao cha matatizo

Kuhusu ndege kukamatawa huko Canada Je kosa la CDM ni lipi?! Kwamba wewe hujui alieleteleza hilo deni?! Jibu maswali yangu
Sina tatizo na hoja ulizotoa OK....una uhakika gani km serikali imehusika ishu ya lisu? Hivi haujui km lisu wakili? Unajua anasimamia kesi ngapi zenye risk gani? Pia hoja yangu mbona mapungufu ya CHADEMA huyasemi? Kwann MTU akisema mnamkebei wakati kuna Uhuru wa mawazo...?
 
Kwann uandamane bila kibali na CHADEMA uwa wanajinadi wanafuata utawala wa sheria? Inamaana hakuna njia mbadala hadi waandamane....OK yule diwani aliyekatwa mapanga unailamu VP polisi au CCM wao wamefanya nn? Tusiishi kwa dhana cz km tukienda kwa dhana CHADEMA wanalo la kujibu juu ya kifo cha CHACHA wangwe hadi Leo kimya....dhana zipuuzwe utaratibu ufuatwe...

Na si unaona walipata baada ya kuandamana that's means labda wasingeandamana wasingepata kabisa

Sasa swali la kujiuliza why mkurugenzi akuwapa before wakati wanakwenda kwenye office yake kwa utulivu na amani?
 
Uchanzo cha chadema ni wapi?! Kwa mfano maandamano ya kinondoni, chadema wangefanya Je?! Mpaka siku ya mwisho jioni saa 12, bado Mkurugenzi amewanyima viapo vyao vya kuwatambulisha vituoni na kesho yake saa 12 kura zinapigwa, wamefanya Je?!! Wakati huo wenzao wana viapo zaidi ya wiki!!! Kwa nini usione tatizo lilipo?! .

Tundu Lissu alisababishaje kumiminiwa risasi kama chatu?! Na Je Mawazo alifanya nini mpaka acharangwe mashoka, kama nyama buchani?! Hebu eleza chanzo chao cha matatizo

Kuhusu ndege kukamatawa huko Canada Je kosa la CDM ni lipi?! Kwamba wewe hujui alieleteleza hilo deni?! Jibu maswali yangu



Baada ya kulazimisha nakuandamana ili kuchukua hizo form wamepata faida gani? Kwanini wasingetumia Busara ya kawaida tu.
 
Na si unaona walipata baada ya kuandamana that's means labda wasingeandamana wasingepata kabisa

Sasa swali la kujiuliza why mkurugenzi akuwapa before wakati wanakwenda kwenye office yake kwa utulivu na amani?
Ilo anaweza kujibu mkurugenzi tu cz ye ndio anajua kwa nn alichelewesha...hoja yangu mawazo mbadala yasikilizwe
 
Na si unaona walipata baada ya kuandamana that's means labda wasingeandamana wasingepata kabisa




Sasa swali la kujiuliza why mkurugenzi akuwapa before wakati wanakwenda kwenye office yake kwa utulivu na amani?


Baada ya kuzipata zimewasaidia nini?
 
Back
Top Bottom