Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,438
- 4,464
Hapo ni blaha blaha tupu! Kwa nini aambiwe yeye tu na sio wabunge wengine wa tanzania?
Mkitaka kuwajua wanyarwanda kwa kuplot vitu ingieni jukwaa la kimataifa.Kama waliweza kumwambia Kikwete mhutu watashindwa kumtengenezea huyo mama.Huyu mama anawasumbua sana bungeni mule.
sosoliso Shy- Rose Wangu amejibu
Bunge la Afrika mashariki ni sehemu nyingine ambayo ni kijiwe cha kupatia riziki,
Sio kweli! Jaribu kuwaza nje ya box!
Kuna mwendesha semina mmoja pale Mlimani City alikazana kuwaambia wanasemina wake "MNAPASWA KUWAZA NJE YA BOX".....Mmoja wa wanasemina alikerwa na kurudiwa rudiwa kwa kauli hiyo, akamuomba mseminishaji aeleze nini maana ya kuwa ndani ya box, nini maana ya kuwaza nje ya box na kwa namna gani mtu anawaza ndani au nje ya box...!! Bahati mbaya mseminishaji alishindwa kutoa ufafanuzi...kwa lugha nyepesi ailonekana kakariri msemo huo bila kuuelewa..macho_mdiliko ebu anzisha uzi mhususi utoe mhadhara juu usemi huo-KUWAZA NJE YA BOX
Huyu nae anataka kutumia turufu ya ''maslahi ya watanzania'' kuficha tabia yake mbovu iliyooza kama yai viza! Anajulikana na watu wa karibu yake kuwa ni mlevi na mgomvi na hali huwa mbaya sana anapolewa! Halafu anatumia ile ile mbinu mufilisi ya ma-ccm kusema ''lete ushahidi'' au ''wanataka kunichufua kwa sababu...''