SAKO LA NYANI
New Member
- May 17, 2013
- 3
- 1
Naomba kuleta mada hii ubaoni wadu japo tupate kujadili kwa mapana.
Nakumbuka kipindi nasoma sekondari miaka ya 90's ,mnapofika darasa la saba karibu na kumaliza kunafomu tulikuwa tunazijaza kama sikosei zilikuwa zinaitwa TSM9. Pale tulikuwa tunajaza shule ambazo mtu ungependa uchaguliwe kwenda kuendelea na masomo ya sekondari.
Nakumbuka tulikuwa tunachagua shule za sekondari mbili naya ufundi moja, nahata matokeo yalikuwa yakitoka unakuta kuna waliochaguliwa kwenda sekondari za kawaida na wale wanaokwenda shule za ufundi kama Mtwara Tech, Moshi Tech, Ifund Tech, Tanga Tech nk.
Na wanafunzi waliokuwa wakitoka kwenye hizi shule baada ya kumaliza form four walikuwa ni mafundi wazuri tu na hata wengine waliobahatika kwenda kusomea ualimu ndio walikuwa walimu wazuri sana wa masomo ya sayansi katika shule zetu za sekondari wakati ule kama Azania, Ilboru, Kibaha nk, lakini leo hii hizi shule hata hazipo tena kwenye nyuso za wanataaluma.
Swali langu kwa serikali ni je imeshindwa kuziendeleza hizi shule za ufundi? Na pia kwa maanguko haya ya matokeo ya kidato cha nne kwa miaka ya karibu hasa katika masomo ya sayansi serikali inajifunza nini kapo.
Pia shule hizi zilikuwa zinawafanya vijana wengi wanaotoka kwenye hizi shule waweze kujiajiri wenyewe hata kama hawakufanikiwa kuendelea na masomo ya juu zaidi.
Inaniuma sana kuendelea kuandika kwani hizi shule zilikuwa zina tija kubwa sana kwa taifa letu la Tanzania.
Nakumbuka kipindi nasoma sekondari miaka ya 90's ,mnapofika darasa la saba karibu na kumaliza kunafomu tulikuwa tunazijaza kama sikosei zilikuwa zinaitwa TSM9. Pale tulikuwa tunajaza shule ambazo mtu ungependa uchaguliwe kwenda kuendelea na masomo ya sekondari.
Nakumbuka tulikuwa tunachagua shule za sekondari mbili naya ufundi moja, nahata matokeo yalikuwa yakitoka unakuta kuna waliochaguliwa kwenda sekondari za kawaida na wale wanaokwenda shule za ufundi kama Mtwara Tech, Moshi Tech, Ifund Tech, Tanga Tech nk.
Na wanafunzi waliokuwa wakitoka kwenye hizi shule baada ya kumaliza form four walikuwa ni mafundi wazuri tu na hata wengine waliobahatika kwenda kusomea ualimu ndio walikuwa walimu wazuri sana wa masomo ya sayansi katika shule zetu za sekondari wakati ule kama Azania, Ilboru, Kibaha nk, lakini leo hii hizi shule hata hazipo tena kwenye nyuso za wanataaluma.
Swali langu kwa serikali ni je imeshindwa kuziendeleza hizi shule za ufundi? Na pia kwa maanguko haya ya matokeo ya kidato cha nne kwa miaka ya karibu hasa katika masomo ya sayansi serikali inajifunza nini kapo.
Pia shule hizi zilikuwa zinawafanya vijana wengi wanaotoka kwenye hizi shule waweze kujiajiri wenyewe hata kama hawakufanikiwa kuendelea na masomo ya juu zaidi.
Inaniuma sana kuendelea kuandika kwani hizi shule zilikuwa zina tija kubwa sana kwa taifa letu la Tanzania.