Shughuli za Bunge la Afrika Mashariki, zasimama kwa muda usiojulikana

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
buu.jpg

Shughuli za Bunge la nne la Jumuiya ya Afrika Mashariki zimesimama kwa muda usiojulikana kutokana na nchi mbili za Kenya na Sudani Kusini kushindwa kukamilisha mchakato wa kuwachagua wabunge watakaoziwakilisha kwenye bunge hilo.

Afisa Habari wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Bw Bobi Odiko amesema wakati kenya ikiwa bado inakabiliwa na changamoto za kuwapata wabunge wawakilishi wao kutoka kwenye vyama vya siasa,baadhi ya wananchi wa Sudani Kusini wamewasilishan rasmi pingamizi la kusimamisha kuapishwa kwa wabunge wa bunge hilo kwa madai kuwa wabunge waliochaguliwa kutoka nchi hiyo hawakupatikana kihalali.

Bw Odiko amesema hatua hiyo itaathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za bunge hilo la nne ambapo kwa mujibu wa sheria na taratibu kwa sasa shughuli zote zitalazimika kusimama ikiwemo ya kuwapisha wabunge wapya,kuchagua spika na kuunda kamati haziwezi kufanyika hadi mchakato wa kuwapata wabunge kutoka nchi zote wanachama utakapokamilika.

Alipolipokuwa anafunga Bunge la tatu la Jumuiya hiyo Spika wa Bunge hilo anayemaliza muda wake Mh Daniel Kidega alisema kuwa walishatoa taarifa ya kuitaka nchi ya Kenya kukamilisha haraka mchakato wa kuwapata wabunge wao ili kuepuka kukwamisha utendaji kazi wa bunge hilo.

Hadi sasa nchi tano wanachama ikiwemo Tanzania,Uganda,Rwanda,Burundi na Sudani Kusini zimeshawasilisha majina ya wabunge wanaoziwakilisha japo majina ya wabunge wa nchi ya Sudani Kusini wamewekewa pingamizi.

Chanzo: ITV
 
HUU MUUNGANO UMEKAA KINAFIKI SANA,KUVIZIANA KWINGI MTU AKOSEE KIDOGO MWINGINE ASEPE NA ASSETS
 
Utaratibu wa kuchagua wajumbe ungekuwa unafanyika na wawakilishi wabobevu wa siasa, sheria na uchumi kutoka nchi zinazo unda muungano huu, hii ya kuchagua kila nchi wawakilishi wake ni upuuzi maana fitna, majungu, kibri, kujiona ndio vinafanya mchakato wa kuchagua wawakilishi mwisho wanaenda wasio na sifa kwa kuwa tu chama kimewapenda, wengine wanaenda ili kumkomoa fulani akose, mchakato ni wa hovyo hovyo tu.
 
buu.jpg

Shughuli za Bunge la nne la Jumuiya ya Afrika Mashariki zimesimama kwa muda usiojulikana kutokana na nchi mbili za Kenya na Sudani Kusini kushindwa kukamilisha mchakato wa kuwachagua wabunge watakaoziwakilisha kwenye bunge hilo.

Afisa Habari wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Bw Bobi Odiko amesema wakati kenya ikiwa bado inakabiliwa na changamoto za kuwapata wabunge wawakilishi wao kutoka kwenye vyama vya siasa,baadhi ya wananchi wa Sudani Kusini wamewasilishan rasmi pingamizi la kusimamisha kuapishwa kwa wabunge wa bunge hilo kwa madai kuwa wabunge waliochaguliwa kutoka nchi hiyo hawakupatikana kihalali.

Bw Odiko amesema hatua hiyo itaathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za bunge hilo la nne ambapo kwa mujibu wa sheria na taratibu kwa sasa shughuli zote zitalazimika kusimama ikiwemo ya kuwapisha wabunge wapya,kuchagua spika na kuunda kamati haziwezi kufanyika hadi mchakato wa kuwapata wabunge kutoka nchi zote wanachama utakapokamilika.

Alipolipokuwa anafunga Bunge la tatu la Jumuiya hiyo Spika wa Bunge hilo anayemaliza muda wake Mh Daniel Kidega alisema kuwa walishatoa taarifa ya kuitaka nchi ya Kenya kukamilisha haraka mchakato wa kuwapata wabunge wao ili kuepuka kukwamisha utendaji kazi wa bunge hilo.

Hadi sasa nchi tano wanachama ikiwemo Tanzania,Uganda,Rwanda,Burundi na Sudani Kusini zimeshawasilisha majina ya wabunge wanaoziwakilisha japo majina ya wabunge wa nchi ya Sudani Kusini wamewekewa pingamizi.

Chanzo: ITV
Kama Tanzania ilichelewesha wabunge sembuse nchi changa Sudan Kusini .hilo bunge lisubiri tuu .kwanza linapunguziwa matumizi .ngoja na Somalia wajiunge waje na wawakilishi Wa Al shabaab
 
Back
Top Bottom