Ok "Life is Short" labda nijielimishe kupitia kwako! Nipe faida hai, tangible, zinazoonekana, za ukweli na zinazofanana na hizo ambazo kwazo sisi tutanufaika kuliko wao watakavyotufaidi! Kumbuka kwa Watanzania wa sasa na Tanzania yetu lazima tuishi sio kusaidia wenzetu tena kama enzi zile tulipojitolea kwa hali na mali zetu, Ni wakati sasa na labda hii itatuamsha kwamba tufunge mikanda na hii BIG RESULTS NOW isiwe tena ni kama misemo ya mipasho!
Tungekuwa kama wenzetu Kenya na Wakenya basi "labda" kungekuwa na kila nia na haja ya kulipigania shirikisho lakini kwa sasa nasema BADO! Tujiinue kwanza humu ndani; kielimu, kitekinolojia, kiuchumi..viwanda, miundombinu ya usafirishaji, uzalishaji mali, chakula etc etc( mf. tunaingiza mchele, mahindi toka nje...kweli hii ni sahihi??) jazia na mengine unayoyajua halafu hebu tuandikie hapa hapa JF kwamba kwa nini mimi SIONI, ZANZIBAR-NYAMWEZI, Na wengine tusitake kuachana na huu up..uzi wa EAC?
Tupeleke hata hizi efforts zetu kufufua viwanda vyote vilivyokufa nchini..na kumbuka viwanda hivi ambavyo vilitoa ajira kwetu vilitaifishwa kiujanja ujanja na mikataba mibovu na hawa hawa makupe kwa nia ya kutugeuza sisi SOKO la kuuzia bidhaa zao. Nimewahi kumshuhudia waziri mmoja wa viwanda akisema "...hatuwezi kutaifisha kile kiwanda kwa sababu mkataba ulioingiwa unamkinga....kiwanda kimefungwa muhusika kahamisha machines na kila kitu kapeleka Kenya, huku ninyi mumekaa mwatoa mimacho tu....)
Na sasa hivi kwa elimu yetu ilivyoduni vijana wetu wengi hawawezi kushindanishwa na baadhi ya wenzetu wanaokuja humu nchini, ukisema tuingie tu then tutajirekebisha mbele kwa mbele au eti watatufanya na sisi tuamke nakataa...tunawaona walivyo huko kwao tunaweza kujifunza toka kwao wakiwa hukohuko! na sisi hapa tukiwasugua vizuri waliopewa dhamana hizi au kujenga uzalendo kwenye utendaji wetu nasi tutafikia.
Tuachane na kudanganywa danganywa huku kusiko na tija, tunataka kuzidi kujiangamiza tu! Vizazi vijavyo watakuwa makoloni ya hawa watu. Tazama tu hazina ya elimu wanayopatiwa vijana wetu, uliona matokea ya mitihani mbalimbali ilivyotoa taswira ya tunakoelekea. Jee tusipoamka sasa na kuhakikisha vijana hawa wanapatiwa hasa elimu inayotoa ushindani wa sasa na wa wakati ujao je watakuja kuwa wapi kama si vibaraka wa hawa watu? Na sizungumzii tu hata kwa hii EAC, hata nchi nyingine..wakija hapa na kuomba kazi hasa kwa mashirika makubwa makubwa wabongo wenzetu wamekuwa hawazipati hizi kazi japo zinafanyikia kwao. Nenda Nigeria halafu tafuta ni idadi gani ya wabongo wanaofanya kazi kule kwenye mashirika haya makubwa....
Tubadilike sasa na si kusubiri au kujitumbukiza zaidi kwenye shimo tutaloshindwa kutoka! Humu ndani tumalizane kwanza kabla ya kwenda huko nje.