Shitambala ajibu agizo la Dr. Slaa


Kweli kabisa hatukimbii matatizo bali tunayakabili mpaka tupate suluhu
 
mi naona ni vema wakamwacha bwana shitambala akajiuzuru kwani akiendelea kukalia kiti chake wakati uchunguzi unaendelea hakutakuwa na haki yoyote itakayotendeka. CDM siyo shitambala pekee. Apishe wengine washike usukani nauhakika tutafika. Pia ni vema wale wote wanaodhaniwa hawafai kuwepo kwenye chama watoke mapema ili nguvu ya kukijenga chama ianze mapema..:A S-alert1:
 
Sidhani shitambala Katuhumiwa na chama kula mlungula bila shakaka atakuwa amejistukia......
 
Du! Shitambala hivi kweli umekuwa mwenyekiti wa CDM mkoa halafu hujui mchakato wa kuwa pata wa bunge viti maalumu? amakweli ahere umejihuzuru....... hunamtazamo mzuri wa kiuongozi in other language you are incapable leader
 

Ukichunguza sana toka mwanzo katika maelezo yake anayo maamuzi tayari juu ya hatma yake. Wayafanyie kazi madai yake, lakinii ikishindikana na kuendelea kumbembeleza ni wastage of time. Wamuachie aende
 

Nilikuwa mmoja wa wagombea viti maalum toka mkoa wa Iringa, nimetoa mchango mkubwa kwa wagombea wote wa mkoa wa iringa na nje ya Iringa kama Ubungo, Segerea yalipo makazi yangu na Kilombero kwa dada Regia

Nilizunguka karibu kata zote za Isimani licha ya kutokuwepo mgombea ubunge ili kuhakikisha angalau tunapata kura wakati wa kampeni. niliomba likizo kazini na baadaye kuacha kazi ili nikafanye kampeni mkoani Iringa, Nina Digrii ya uchumi pia tukisema digrii ni vigezo. Bahati mbaya sikubahatika kuwa mmoja wa wateule, lakini mchango wangu nilikuwa nautoa kwa Chama, sikuwa nautoa ili nipate ubunge wa viti maalum, nimefurahi kwa walioteuliwa, nampongeza dada Yangu Chiku Abwao kwa kuteuliwa kuwa Mbunge viti maalum na kazi yangu ni kumsaidia, kushirikiana naye na kuchota uzoefu na uwezo toka kwake na siyo kupiga majungu.

Bahati nzuri mimi ni Muislamu na wakati wote siamini kama Kitila alitumia kigezo cha dini yangu kuniacha nje kwa sababu hata Chiku Abwao ni muislamu kwa hiyo wenye hoja kama hizo za udini ni wanasiasa waliofilisika kimawazo.

Sitaki kuzungumzia hoja ya kwa nini mbeya wamekosa mbunge wa viti maalum lakini napingana na wanaoendekeza majungu na kujaribu kujenga Taswira kwamba walitakiwa wawe wabunge wa Viti Maalum no Matter What????

Kazi ya kulikomboa taifa hili haiwezi kuletwa na wanasiasa ambao akili yao ni kuwa wabunge au wateule. Mtazamo wangu mara zote umekuwa mmoja. Tuungane pamoja , Tushirikiane na waliopata nafasi, lakini waliopata nafasi wafanye kazi kwa bidii ili tulio nje tusipate nafasi ya kusema "Hata mimi ningefaa kuliko yule" hizi hoja za kwa nini Christine Lisu kateuliwa au Kwa nini Lucy Owenya ni upuuzi. Tusubiri performance yao ndipo tuwaseme. Naamini Dr Kitila Mkumbo ni Mtu makini na alifanya kazi yake kwa vigezo. Namjua kitila kwa kuwa ni kiongozi wangu lakini yeye hanijui na sihitaji wala sikuhitaji kujipenyeza nijulikane kwani naamini wanaofanya kufanya hivyo ni wale wasiojua kuwa Siasa is a process, you need to start somewhere, you need to learn from others etc, siyo kulazimisha kupata nafasi za kuongoza.

Kama mtu ana vigezo hatuwezi kumkataa eti kwa kuwa anaitwa Kabwe au Mbowe au Slaa eti kuogopa undugunization

Undugunization ni kuteua watu wasio na vigezo kwa kuangalia majina, Naamini akila Owenya na Lissu wana vigezo na watatuwakilisha vema.

Narudia, sijibu hoja ya Shitambala lakini napingana na walalamikaji wenzangu kwani mimi pia nilikuwa mgombea na nimetoswa na nina furaha, amani na hapa nilipo napanga mikakati ya kuchangia chama ili 2015 tufanye vizuri zaidi

Nawasilisha
 
REYES......wanasiasa wana midomo mitamu hali mikononi mwao wamebeba mikuki iliyochongoka....... ndimi zao zadondosha asali wakati mioyo yao imejaa sumu tene ya mamba.....! nawapenda wanasiasa wa ukweli...ambao nakiari bado ni wachache..ila wabwabwajao wapo wengi...! MANENO YA WANASIASA YASIWE KIPIMO...KIPIMO KIWE MATENDO.....sio ZITTO/MBOWE/SLAA/SHIBUDA/MREMA/LIPUMBA/CHEYO/MAKAMBA/MAGUFULI KASEMA HIVI NA HIVI KWA MASLAHI YA TAIFA(si ya chama) bali BALIZITTO/MBOWE/SLAA/SHIBUDA/MREMA/LIPUMBA/CHEYO/MAKAMBA/MAGUFULI KAFANYA HIVI NA HIVI KWA MASLAHI YA TAIFA
 
Kila ambapo binadamu yupo, hapakosekani madhaifu pia.
dawa ni kutafuta ufumbuzi kwa faida ya wengi

Shitambala kawa muwazi (transparent) ni vizuri kwa uongozi wa CDM nao ukawa wazi ktk hili.
 
Kila ambapo binadamu yupo, hapakosekani madhaifu pia.
dawa ni kutafuta ufumbuzi kwa faida ya wengi

Hoja nzito inapounganishwa na hoja nyepesi!
Je, Shitambara angeweza kujiuzuri kwa Mkoa wa Mbeya kutokupata viti Maalum? Hapana, hii ni hoja nyepesi na yeye kama M/Kiti alipaswa kutatua tatizo na kufuatilia kujua mgawanyo utakavyokuwa maana orodha na utaratibu uliwekwa bayana na kwa kiongozi kama yeye alipaswa kupigania na kujua nafasi ya mkoa wake. Katika hatua hii lazima tutambue kuwa CHADEMA ilikuwepo tangu vyama vingi vilipoanza wakati huo wewe na mimi hatukuwa wapenzi wala wanachama ni hao wakina Mbowe, Slaa na Ndesapesa ndo walikuwepo. Sasa kila kitu kinachanzo na kumbuka ni 2005 ndo chadema wameanza kusimamisha mgombea Urais vilivyoleta viti maalum kwa namna hiyo tutegemee maboresho makubwa zaidi ktk mambo mengi. Natambua hata Shitambara mwenyewe atagundua hiyo nafasi ya M/mkoa aliipata kiulaini laini ni sawa leo hii nataka kuwa M/kiti wa TLP/UDP/APPT Maendeleo huko Lindi nawini kilaini. Kama aliingia CHADEMA kwa dhamira safi lazima akipiganie chama na kuleta mabadiliko.
Swala la Rushwa, hii ndiyo hoja ya kumfanya mtu akae pembeni lakini lazima uwepo uchunguzi ili kukusafisha au kukuweka kwenye hatia vinginevyo hakuna maana na itakuwa ni kero ndani ya chama. Kwa hiyo nikupongeze kwa kujihuzuru kwako sasa ni juu ya chama kufanya uchunguzi wake. Ndugu zangu kwa sasa tutakuwa na Miungu watu sana wanaojisadikisha kuwa bila wao hakuna CHADEMA. CHADEMA SASA NI TAASISI NA SI KIKUNDI TU CHA WATU. TUTAISIMAMIA NA HAITA KUFA. MBOWE, SLAA, NDESA WATAPITA LAKINI CHADEMA ITABAKI.
 
Hoja za Shitambala bado sizielewi sana. Hoja zake ni kama zinafanana na za marehemu Chacha Wangwe.
1. Je Hoja za Shitambala ni shutuma anazopewa au ni viti maalum? Mimi ninaona ni kama hoja ya shutuma ya rushwa kwa sababu anahusisha na suala la kupisha uchunguzi.
2. Kama hoja ni kuhusu tuhuma, ni nani anayemtuhumu kuwa kapokea rushwa? ni uongozi wa juu wa Chadema au viongozi wenzake kutoka wilaya za Mbeya?kama siyo viongozi wa juu wa Chadema kwanini anakataa kumtii Katibu Mkuu?

Ki ukweli hizo tuhuma inaonekana kuwa yeye mwenyewe ndiye anayezizungumzia zaidi kuliko hata wanachama wengine na ni yeye anayetaka kutoa nafasi ili uchunguzi ufanyike. kama waliomtuhumu ni viongozi wa ngazi za wilaya halafu ikagundulika kuwa hakupokea rushwa atamlaumu nani na nini hatima ya Shitambala? Ni sura gani ya uongozi anayoionyesha kujifanya mwajibikaji eti anapisha uchunguzi ufanyike wakati viongozi wa juu wa Chama wanamwambia asijiuzulu?

Halafu watu wasisahau kuwa CCM haijaacha kuchochea vurugu katika vyama vya upinzani, wala si kweli waliopo katika vyama vya upinzani ni wapinzani. Kitu kikubwa ni kuwa vyama havina uwezo wa kuwatambua na kuwakataa watu hao wanaojiunga kwa malengo yao kwa sababu chama hakina uwezo huo na lazima kifuate utaratibu uliowekwa. Hivyo hayo yanayotokea yanaweza yakawa ndiyo matokeo ya kazi ya waliotumwa kukiua Chadema.
 
Political leaders normally do Mistakes.
Analytical leadres normally do blunders plus bloodshed.

msimamo wangu unaeleweka!!!
 
Hayo ndiyo maneno
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…