Jamani hapa lazima tuwekane sawa na tuwe wawazi ili kukinusuru chama vinginevyo chadema itatufia mikononi kama ccm inavyoelekea kufa mikononi mwa rais kikwete. Mimi lazima niseme ukweli kwa manufaa ya chama atakayecheka acheke, atakayenuna anune, atakayelia alie ilimradi ujumbe umefika. Tukubali tusikubali, tutake tusitake uteuzi wa viti maalum kwa chadema ulikubwa na mizengwe fulani ambayo kwa namna moja au nyingine isipodhibitiwa siku zijazo chadema KITAKUFA! Nasema hivi kwa sababu kuna harufu ya undugunaization ambao umesababisha baadhi ya maeneo ambako chadema kimepata viti viwili au zaidi vya majimbo lakin yamekosa walau kiti 1 maalum. Kwa mfano, kulikua na sababu gani kwa mkoa wa singida kupata viti 2 na kilimanjaro kupata viti 3 hadi 4 maalum halafu mkoa kama shinyanga ambako chadema wamezoa majimbo 4 na kuibiwa la shy mjini na mbeya ambako wamezoa majimbo mawili kukosa walau kiti kimoja maalumu!? Pia kuna sababu gani zanzibar kupewa viti maalum 3 wakati chadema wanajua no matter what they do out there, the island will remain CUF-CCM dominated! Nadhan zanzibar kiti kimoja au 2 vingetosha walau kimoja kikaenda shinyanga! Katika mazingira kama haya kwa nini mtu asihoji wakati anaona jina la christina lissu (sijui uhusiano wake na tundu lissu) na la binti ndesa to mention but a few, yakiwa kwenye orodha!!? Viongozi wa chadema lazima walione hili na walifanyie kazi mapema wasituletee tabia za kubebana kama za ccm. Chadema ndo kwanza kinakua na hakijawa na wawakilishi wengi sana kwa hiyo basi wapinzani wake wanaangalia kila pungufu linalotokea na wanapata cha kusema na kuandika. Naomba tusiwape nafasi wapinzani wetu wasije sababisha chama chetu kife na wao ccm wakaendelea kutamba wakati wananchi wamesha wachoka!! TAKE CARE., LONG-LIVE CHADEMA..