Shitambala ajibu agizo la Dr. Slaa

Viti maalum vya CHADEMA vinakwenda kwa watu maalum , Kanda maalum na familia maalum. Hivyo vilitengwa kwa watu wa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha tu, na kwa familia za Slaa, Mbowe na Ndesamburo

How ironic it is to look for seniorship member in JF by posting hearsayings and feelings. I thought here we talk/writting only when we have fact and data! I am getting tired now with this forum!
 
Shitambala usijivunjie heshima katika jamii. Madai yako ni ya msingi kabisa lakini namna unavyoyaleta katika jamii unazidi kutoa mianya ya utata juu ya shutuma za rushwa kwako. Nadhani kama uliweza kutuhumiwa kupokea fedha ili uuze Ubunge basi si ngumu kuhisi tena kuwa umepokea ili uisambaratishe chadema huko Mbeya. Katibu mkuu amekuandikia barua kuwa tuhuma hizo hazina msingi na si za kweli lakini wewe unasisitiza kuwa uchunguzi ahujaisha... ni uchunguzi gani huo na unaendeshwa na nani???? Sasa unakuja na dai jipya ... ngoja tusubiri uongozi wa juu utasema nini kuhusu hilo!

Nafikiri Mh. Shitambala unaweza kutenda vyema zaidi ya msimamo ulionao kwa manufaa ya chama na maisha ya baadae ya watanzania.
Kwenye bold hata mimi pananipa mashaka kama uongozi umeshasema tuhuma hazina msingi still mtuhumiwa anasisitiza uchunguzi haujaisha sijui anataka aambiwe tuhuma ni za kweli, kama hivyo basi yeye Shitambala atuambie kama tuhuma ni za kweli.
 
Viti maalum vya CHADEMA vinakwenda kwa watu maalum , Kanda maalum na familia maalum. Hivyo vilitengwa kwa watu wa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha tu, na kwa familia za Slaa, Mbowe na Ndesamburo

Uchuro wewe! Weka ushahidi usichonge utadhani umebanwa na mavi!
 
How ironic it is to look for seniorship member in JF by posting hearsayings and feelings. I thought here we talk/writting only when we have fact and data! I am getting tired now with this forum!

Don't run away form facts. Viti vimegawanywa kwa mtindo wa undugu undugu. Formula aliyotumia consultant iliwapa upendeleo relatives wa Ndesamburo, Mbowe na Slaa.
 
Viti maalum vya CHADEMA vinakwenda kwa watu maalum , Kanda maalum na familia maalum. Hivyo vilitengwa kwa watu wa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha tu, na kwa familia za Slaa, Mbowe na Ndesamburo
mbowe hajaweka ndugu yeye hupitisha mahawara
 
Source: Francis Godwin Blog.


JINAMIZI la uchaguzi limeendelea kukikumba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoa wa Mbeya baada ya viongozi wa wilaya na mkoa wa chama hicho kuibuka na kuwatupia lawama viongozi wa kitaifa wa Chadema kwamba hawajautendea haki mkoa wa Mbeya kutokana na kushindwa kutoa nafasi hata moja ya mbunge wa viti maalum toka mkoani hapa.


Wakizungumza na mtandao huu leo, viongozi wa Chadema mkoa na wilaya walisema viongozi wandamizi wa chama hicho hawajautendea haki mkoa wa Mbeya katika suala la ubunge wa viti maalum wakati mkoa huu ulikuwa wa pili baada ya Mwanza kwa kutoa kura nyingi kwa aliyekuwa mgombea urais kupitia Chadema,Dk.Willbroad Slaa.

Malalamiko hayo yamekuja siku mbili tu tangu Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Mbeya,Sambwee Shitambala kutangaza kujiuzuru uenyekiti kwa madai ya kupewa tuhuma zisizo za kweli kwama alipewa mlungula wa Sh.Milioni 600 na hivyo kuiachia CCM iibuke kidedea jimbo la Mbeya Vijijini.

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Kyela, Elick Sata Mwalyage, alisema hatua ya mkoa wa Mbeya kutopata viti maalum vya ubunge limewasikitisha sana viongozi wa mkoa,wilaya na wanachama ambao wamekuwa wakihoji ni kwanini mkoa umenyima nafasi hiyo.

"Suala la kutopendekezwa wabunge wa viti maalum kutoka mkoa wa Mbeya limetusikitisha sana kama viongozi na wanachama wanahoji maana mkoa wetu kwanza umefanikiwa kupata wabunge wa wawili wa kuchaguliwa na pili ulishika nafasi ya pili kupata kura nyingi za urais ukilinganisha na mikoa mingine ambayo imepewa upendeleo huo,"alisema Mwalyage.

Mwalyage alisema hawaelewi kukosekana kwa mbunge hata mmoja wa viti maalum kutoka mkoa wa Mbeya ni tatizo ambalo limesababishwa na viongozi wa Chadema mkoa au taifa na kwamba wao kama viongozi wa Chadema wilaya wanaendelea kufanya utafiti kubaini kasoro zimetokana na nini.

Naye Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Chunya, George Mtasha,alisema viongozi wa makao makuu hawajautendea haki mkoa wa Mbeya kutotoa nafasi ya ubunge wa viti maalum na kwamba wanashangazwa idadi kubwa ya waliopendekezwa kuwa wabunge wa viti maalum wametokea mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

Mtasha alisema hakuna asiyefahamu kuwa viongozi wa wilaya zote za mkoa wa Mbeya walipigana kufa na kupona kuhakikisha Chadema inapata ushindi kwenye kata,majimbo na mgombea wa urais anapata kura nyingi lakini cha kushangaza umeishia kunyima nafasi ya viti maalum.

Mwenyekiti huo wa Chadema wilaya ya Rungwe, akizungumzia suala la kujiuzuru uongozi Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Mbeya, Shitambala, alisema amefanya demokrasia kwani kutokana na hali ilivyokuwa ikiendelea ndani ya chama walipanga baada ya uchaguzi mkuu kumalizike viongozi wa wilaya wangeshinikiza kufanyike mkutano mkuu wa chama kwa lengo la kumung'oa.

Kwaupande wake Katibu wa Chadema mkoa wa Mbeya,Eddo Makata alisema bado ana imani na viongozi wa makao makuu ya chama kwamba watautendea haki mkoa katika suala la viti maalum vya ubunge.

 
Jamani hapa lazima tuwekane sawa na tuwe wawazi ili kukinusuru chama vinginevyo chadema itatufia mikononi kama ccm inavyoelekea kufa mikononi mwa rais kikwete. Mimi lazima niseme ukweli kwa manufaa ya chama atakayecheka acheke, atakayenuna anune, atakayelia alie ilimradi ujumbe umefika. Tukubali tusikubali, tutake tusitake uteuzi wa viti maalum kwa chadema ulikubwa na mizengwe fulani ambayo kwa namna moja au nyingine isipodhibitiwa siku zijazo chadema KITAKUFA! Nasema hivi kwa sababu kuna harufu ya undugunaization ambao umesababisha baadhi ya maeneo ambako chadema kimepata viti viwili au zaidi vya majimbo lakin yamekosa walau kiti 1 maalum. Kwa mfano, kulikua na sababu gani kwa mkoa wa singida kupata viti 2 na kilimanjaro kupata viti 3 hadi 4 maalum halafu mkoa kama shinyanga ambako chadema wamezoa majimbo 4 na kuibiwa la shy mjini na mbeya ambako wamezoa majimbo mawili kukosa walau kiti kimoja maalumu!? Pia kuna sababu gani zanzibar kupewa viti maalum 3 wakati chadema wanajua no matter what they do out there, the island will remain CUF-CCM dominated! Nadhan zanzibar kiti kimoja au 2 vingetosha walau kimoja kikaenda shinyanga! Katika mazingira kama haya kwa nini mtu asihoji wakati anaona jina la christina lissu (sijui uhusiano wake na tundu lissu) na la binti ndesa to mention but a few, yakiwa kwenye orodha!!? Viongozi wa chadema lazima walione hili na walifanyie kazi mapema wasituletee tabia za kubebana kama za ccm. Chadema ndo kwanza kinakua na hakijawa na wawakilishi wengi sana kwa hiyo basi wapinzani wake wanaangalia kila pungufu linalotokea na wanapata cha kusema na kuandika. Naomba tusiwape nafasi wapinzani wetu wasije sababisha chama chetu kife na wao ccm wakaendelea kutamba wakati wananchi wamesha wachoka!! TAKE CARE., LONG-LIVE CHADEMA..

Samirnasir nafurahi sana kusoma hii post na pia naunga mkono kama CDM inahitaji kubadili mtindo wake wa viti maalum ili kupunguza malalamiko. Lakini pamoja na hayo yote pengine tusisahau mambo machache na hata tunapolaum tukumbuke hata hao walioshiriki kuandaa mchakato huu hawakuwa miungu wala watabiri kwa mfano
  1. Mchakato wa kutafuta viti maalum chadema ulivurugika mara ya kwanza wakati baraza la wananwake waliposhindwa kufikia mwafaka na hivyo mchakato tofauti ikabidi uangaliwe. Kwa hiyo tatizo kubwa lilianzia pale
  2. Ikumbukwe pia kwamba matangazo ya kupata wabunge kupitia viti maalum yalianza mapema sana kabla ya kuanza kwa kampeni na hivyo wakati huo vugu vugu la kampeni halikuwa kubwa kufanya watu wengi hasa walifikia vigezo kutuma maombi yao kwa CDM, najua wako wanachama wengi waliokuwa na vigezo lakini walizembea kutuma maombi kwa kujua kuwa viti vichache vitapatikana (siwezi kuthibitisha hili bali nafikiri lilikuwa hivyo) na kwa hiyo Wakati kitila amepewa kazi ya kuchagua hawa wawakilishi waliofikia vigezo pengine walikuwa wachache.
  3. Jambo jingine ambalo pengine ndilo lilikuwa gumu zaidi ni kutabiri kuwa CDM ingepata wabunge wawili mbeya na kukosa kabisa kagera, au wangepata viti vinne shinyanga na kukosa kabisa dodoma, kwa hiyo kusema kuwa shinyanga wamekosa kabisa mwakilishi wa viti maalu au mbeya wamekosa kabisa wakati wana wametoa wabunge zaidi ya wawili pengine lingekuwa gumu sana kulitabiri hasa tukikumbuka wakati kampeni zinaanza CDM haikuwa na nguvu sana mpaka kampeni zilivyoshika kasi. pia najua nafasi ya kubadili majina kwa kufuata priorities zikishapelekwa NEC ni ngumu hasa baada ya uchaguzi labda kama wangechelewesha kama walivyofanya CUF lakini pia kuna ambao wangelalamika kama hayo majina yangebadilishwa baada ya uchaguzi
  4. Kuhusu Zanzibar pamoja na kuwa najua walioteuliwa walifikia vigezo lakini ni muhimu pia kukumbuka kuwa CDM kuchukua japo wawakilishi watatu au wanne zanzibar inaleta sura ya muungano na pengine kuongeza washawishi huko ili siku zijazo kura ziongezeke hata huko
Najua na ninaamini CDM imejifunza kwa upande wake na hivyo watafanya utaratibu mzuri zaidi wakatoi huo huo wanannchi na hasa mama zetu na dada zetu tumejifunza pia kutake chances. Siamini kabisa kama kweli kitila ali[pokuwa anafanya mchakato kuu aliwaacha akina mama wa shinyanga na Mbeya wenye qualification zao kabisa kwa kufuata vigezo vilivyowekwa bila sababu
Naomba wanachadema wote badala ya sasa kuendelea kujadili yaliyopita basi tujifunza na ziwe lessons learbed in the future
 
Amejiuzulu kwa sababu ya tuhuma au viti maalumu? Kama ni la tuhuma wanaopaswa kumchunguza wamesema aendelee na kazi.yeye anasema anasubiri achunguzwe.hii ni danganya toto.tatizo ni viti maalumu,na nadhani chadema waliongelee kuondoa mashaka.ila ni shitambala mwenyewe anatuhumu na wala siyo watu.
 
nadhani viti maalum viendane na uwiano wa ushindi wa majimbo, mkoa ulioshinda majimbo mengi upewe viti vingi uliokosa usipewe

unaweza ukawa sawa,lakini je kama kuna mwingine ana uwezo zaidi lakini akawa mkoa ambao haukutoa mbunge itakuwaje?
Nadhani suluhisho ni kutafuta njia nzuri ya kuteua hao wateule.
Mfano kila mkoa uteue japo mtu mmoja kwa kuangalia sifa na jina likishaletwa toka mkoani haina haja kulijadilia zaidi ya kuhakiki vigezo vilivyo kubaliwa kuwa vitumike then wengine wapatikane kwa kuzingatiwa vigezo vya ushindani.
Lakini pia ni sijui kama ni tume ya uchaguzi au ni katiba inayotaka majina ya wabunge wa kuteuliwa yapelekwe mapema kabla ya uchaguzi mkuu, huu ni utaratibu mbovu unaonyima vyama uwezo wa kupeleka wateule kwa uwiano sawa.
 
Katika hili la viti maalum, CDM MUST be more cautious, or else prejudges are getting too close to reality
 
Tabia hii ya upendeleo katika kuteua wabunge wa viti maalum(Wanawake) ilianza tangu mwaka 2005. Marehemu chacha wangwe alilipigia kelele lakini hakusikilizwa kwa sababu wachaga wameshika nafasi nyingi za uongozi wa kitaifa wa chama. Hata huyo Dr. Kitila alikuja na hiyo formula yake ili apendelee mkoa wake wa Singida(Kitila ni mzaliwa wa Singida). Tabia hii isipokomeshwa hakika CHADEMA itakosa uaminifu mbele ya umma wa watanzania.

Upendeleo unaofanywa katika CHADEMA si katika uteuzi wa viti vya wanawake tu, bali hata katika kugawa rasilimali za chama kwa maendeleo ya chama. Wagombea katika baadhi ya makoa husaidiwa fedha kwa ajili ya kampeni; wagombea katika mikoa mingine huachwa bila msaada wowote. CHADEMA ITABADILISHWA NA WANACHAMA NA SI VIONGOZI. WAJUMBE WA KAMATI KUU, BARAZA KUU NA MKUTANO MKUU WASIKUBALI UPUUZI HUU. Si makosa ya kibinadamu yaliyotokea katika uteuzi wa wabunge wanawake bali ni makusudi mazima kwa ajili ya familia, ndugu na marafiki za viongozi wa juu.

WANACHAMA WA CHADEMA KAMWE MSIKUBALI CHAMA KIFE. CHUKUENI HATUA MADHUBUTI KUREKEBISHA MAMBO; WANACHAMA NDIO WENYE UAMUZI WA MWISHO KWA MUSTAKABALI WA CHAMA NA SIYO VIONGOZI. Shitambala na wenzako wa Mbeya unganeni na wanavchama wengine kurekebisha mambo ndani ya chama; Kamwe usikubali kutoka ndani ya chama, CDM ni mali yenu
 
Tabia hii ya upendeleo katika kuteua wabunge wa viti maalum(Wanawake) ilianza tangu mwaka 2005. Marehemu chacha wangwe alilipigia kelele lakini hakusikilizwa kwa sababu wachaga wameshika nafasi nyingi za uongozi wa kitaifa wa chama. Hata huyo Dr. Kitila alikuja na hiyo formula yake ili apendelee mkoa wake wa Singida(Kitila ni mzaliwa wa Singida). Tabia hii isipokomeshwa hakika CHADEMA itakosa uaminifu mbele ya umma wa watanzania.

Upendeleo unaofanywa katika CHADEMA si katika uteuzi wa viti vya wanawake tu, bali hata katika kugawa rasilimali za chama kwa maendeleo ya chama. Wagombea katika baadhi ya makoa husaidiwa fedha kwa ajili ya kampeni; wagombea katika mikoa mingine huachwa bila msaada wowote. CHADEMA ITABADILISHWA NA WANACHAMA NA SI VIONGOZI. WAJUMBE WA KAMATI KUU, BARAZA KUU NA MKUTANO MKUU WASIKUBALI UPUUZI HUU. Si makosa ya kibinadamu yaliyotokea katika uteuzi wa wabunge wanawake bali ni makusudi mazima kwa ajili ya familia, ndugu na marafiki za viongozi wa juu.

WANACHAMA WA CHADEMA KAMWE MSIKUBALI CHAMA KIFE. CHUKUENI HATUA MADHUBUTI KUREKEBISHA MAMBO; WANACHAMA NDIO WENYE UAMUZI WA MWISHO KWA MUSTAKABALI WA CHAMA NA SIYO VIONGOZI. Shitambala na wenzako wa Mbeya unganeni na wanavchama wengine kurekebisha mambo ndani ya chama; Kamwe usikubali kutoka ndani ya chama, CDM ni mali yenu
 
Pia kuna malalamiko ya mikoa kukosa fedha za uendeshaji, mathalani katika miaka 5 iliyopita, Chadema mkoani Mbeya haijawahi kupata senti yoyote kutoka sehemu ya ruzuku ya Chama kwa uendeshaji wake mkoani hapa, hili pia lifanyiwe kazi katika kipindi hiki.
 
Tabia hii ya upendeleo katika kuteua wabunge wa viti maalum(Wanawake) ilianza tangu mwaka 2005. Marehemu chacha wangwe alilipigia kelele lakini hakusikilizwa kwa sababu wachaga wameshika nafasi nyingi za uongozi wa kitaifa wa chama. Hata huyo Dr. Kitila alikuja na hiyo formula yake ili apendelee mkoa wake wa Singida(Kitila ni mzaliwa wa Singida). Tabia hii isipokomeshwa hakika CHADEMA itakosa uaminifu mbele ya umma wa watanzania.

Upendeleo unaofanywa katika CHADEMA si katika uteuzi wa viti vya wanawake tu, bali hata katika kugawa rasilimali za chama kwa maendeleo ya chama. Wagombea katika baadhi ya makoa husaidiwa fedha kwa ajili ya kampeni; wagombea katika mikoa mingine huachwa bila msaada wowote. CHADEMA ITABADILISHWA NA WANACHAMA NA SI VIONGOZI. WAJUMBE WA KAMATI KUU, BARAZA KUU NA MKUTANO MKUU WASIKUBALI UPUUZI HUU. Si makosa ya kibinadamu yaliyotokea katika uteuzi wa wabunge wanawake bali ni makusudi mazima kwa ajili ya familia, ndugu na marafiki za viongozi wa juu.

WANACHAMA WA CHADEMA KAMWE MSIKUBALI CHAMA KIFE. CHUKUENI HATUA MADHUBUTI KUREKEBISHA MAMBO; WANACHAMA NDIO WENYE UAMUZI WA MWISHO KWA MUSTAKABALI WA CHAMA NA SIYO VIONGOZI. Shitambala na wenzako wa Mbeya unganeni na wanavchama wengine kurekebisha mambo ndani ya chama; Kamwe usikubali kutoka ndani ya chama, CDM ni mali yenu
Siku hizi kila mtu anaijua sana CDM na utaratibu wao duu
 
Ni mwanamama gani wa mbeya aliyekuwa anafaa tujaribu kumuweka kwenye criteria zilizobainishwa tuone anapata score kiasi gani.?

Unajua ni challenge kumrizisha kila mtu. Ukisema Upendeleo uwe kwa kigezo mikoa mbayao chadema ilipata kura au wabunge wengi jibu linatukuwa lile lile Arusa, Kilimanjaro itakuja kidedea.

Arusha , Mbeya kilimanjaro kupata wabunge zaid ina maana Zenj tanga Mtwara wasipate.
 
tatizo la viti maalum ni la kimuundo zaidi kwani majina yalipelekwa kabla ya uchaguzi mkuu bila kujua matokeo ya tarehe 31/october yatakuwa je.......watu walipohamasika baada ya kampeni kuanza tayari majina yalishapewa maksi na kupangwa bila kujali anatoka wapi, tatizo watu hatutaki kujionyesha tunaunga vyama mbadala hasa wakina dada zetu ....madha yake ni kukosa viti maalum kwa mikoa mingine.....ila na wale walio pitia viti maalum kwa muda mrefu nao waachie ngazi wengine ili kuimarisha vyama
 
ANGALIZO:ifike mahali wanachama wa cdm wawe matured,kama m2 anaona haridhiki na jambo ndani ya chama kuna vikao,km m2 hawezi ku2mia vikao aondoke,utaratibu wa viti mahalumu hauwezi kuwa gumzo wakati kila mt2 anajua kilichotokea,mbona hamjadiri vya ccm mchakato uliojaa rushwa na kasoro nyingi?ACHA KUJADIRI YALIYOPITA JENGENI CHAMA KWA mustakabali endelevu
 
Ndivyo chama kinavyojengwa hivyo. Rumi haikujengwa kwa siku moja, lazima CDM ikubali kuwa kuna kupanda na kushuka. Shitambala asiweke masharti mengi sana, na mimi sikuona haja ya yeye kujiuzulu kwa sababu ya maneno ya mitaani. Kama ingekuwa maneno tu yanamfanya mtu ajiuzulu basi pasingekuwa na viongozi. Unapojiuzulu ni pale unapoona kwa dhamiri yako kabisa kuwa una hatia katika tuhuma hizo, lakini kama ni maneno tu ya mitaani, no Mr Shitambal alitakiwa kupuuza kwa manufaa ya chama. Mwana mapinduzi huwa hakati tamaa mapema kiasi hicho.

Long live CHADEMA
 
Back
Top Bottom