Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,116
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekemea vikali vitendo vinavyoendelea vya baadhi ya Mashabiki kupiga Mashabiki na Viongozi wa Timu pinzani na kusema imeanza kukusanya ushahidi wa matukio yote ya aina hiyo kupitia CCTV camera zilizoko uwanjani.
"Watu wote wanaohusika na vurugu kwenye mpira wa miguu (Mashabiki na Viongozi) watachukuliwa hatua kali za kinidhamu pia wote wanaotoa shutuma kwa Viongozi na maneno ya kuhamasisha vurugu katika mpira wa miguu nao watachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni zilizopo".