Mnabuduhe
JF-Expert Member
- May 8, 2015
- 352
- 590
Naomba nitangaze maslahi binafsi kwanza! Mimi ni Mzaliwa wa Shinyanga,Wilaya ya Kishapu.
Hivyo ninaumizwa sana na uwakilishi hafifu toka mfumo wa vyama vingi ulipoanza hapa Tanzania mwaka 1992.
Mkoa wangu huu pendwa wa WASUKUMA wazee wa Nduhu Tabu hata kama anapingu mkononi!!!!! Tubadilike aisee.
Tumekuwa na tabia ya kupeleka Uwakilishi hafifu sana Bungeni,Tunapeleka watu ambao hawawezi kutetea rasilimali zetu na haki za watu wa Shinyanga hasa juu ya Ardhi,Madini,Pamba na Elimu duni.
Hii nadhani inachochewa kwa kuchagua watu wasio na uchungu na Ustawi wa Watu wa Mkoa wa Shinyanga.
Mosi,Watu wa Shinyanga wamekuwa wakichagua Raia wenzao wenye asili ya Mashariki ya Kati wakidhani wanachagua WAZUNGU!
Kumbe Jamaa ni Watu wanao tafuta kukuza Mitaji yao na kufanya mazingira ya Biashara zao kuwa Rafiki.
Hili la kuchagua watu wenye asili ya Mtume wa Mwenyezi Mungu ni tatizo la Tanzania nzima kwa kweli! na unapotaka Kulizungumza unaitwa Mkabila na Mbaguzi mkubwa! lakini Ukweli unabaki kuwa Ukweli tu! Hao Jamaa hawanaga shobo na matatizo ya watu wenye Asili ya Tanganyika Halisi.
Pili,Nenda Kilimanjaro nenda Manyara Nenda Ruvuma nenda Mwakaleli nenda Tanga hata kama Ulizaliwa huko na Maisha yote Umeishi nao ila tu Wakishajua we ni Mtafutaji mpiganaji Muongoza njia hawawezi kukuamini Uwawikilishe asilani.
Mwenye Ushahidi toka mfumo wa Vyama Vingi Uanze anitajie yeyote aliyewahi kuwa Mbunge toka Mkoa wa Kilimanjaro mwenye Asili ya Shinyanga.
Anitajie yeyote mwenye asili ya Kagera aliyewahi kuwa Mbunge kutokea Mkoa wa Mara.Nitafuta mara moja Uzushi huu.
Tuchague watu watakao kuwa radhi kuwapatia Watu wa Kwao Uwakilishi wa Kweli bila Mashaka! tukiendekeza makapile na madoti na masoda tutaendelea kuwa Kichwa cha Mwenda Wazimu.
Sijataja jila la mtu anayegombea,sijaweka picha ya mtu anayewania! nimeheshimu Demokrasia.
Salamu hizi pia ziwafikie Wanyamwezi - Tabora, Wasingida,Katavi na jirani yake,Walugulu watani zangu,na Kamwene.
Tubadilike Wasukuma wenzangu!
Asalam Aleikum.