SHINYANGA: DC aendesha oparesheni ya usafi na kuwakamata Wananchi ambao miti iliyopandwa mbele ya nyumba zao imekufa

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro ameendesha oparesheni ya usafi na Mazingira kukagua usafi na miti.

Kupitia oparesheni hiyo amewawajibisha Wananchi ambao miti yao imekufa kwa kuwalipisha faini ya Shilingi 50,000 kwa mti na kuwataka wapande mingine.

IMG-20180226-WA0051.jpg

Pichani ni; Wananchi ambao miti iliyopandwa mbele ya makazi au biashara zao imekufa wakipanda kwenye gari la Jeshi la Polisi
=====


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameendesha oparesheni ya usafi na Mazingira kukagua usafi na miti iliyotelekezwa na kuwawajibisha wananchi ambao miti yao imekufa kwa kulipa faini ya shilingi 50,000/= kwa kila mti na kuwataka wapande miti mingine.

Mkuu huyo wa wilaya amefanya oparesheni hiyo Februari 24,2018 katika mitaa mbalimbali mjini Shinyanga ambapo kila mwananchi ambaye miti iliyopandwa kwenye eneo lake imekufa aliwajibishwa kwa kufanya uzembe na kusababisha miti ife.

Katika opareshini hiyo kila mwananchi aliyepigwa faini alikuwa anapatiwa risiti ya malipo na aliyeshindwa kulipa alikuwa anapandishwa kwenye gari la polisi kwa hatua zaidi za kisheria. Akizungumza wakati wa oparesheni hiyo Matiro ambaye alikuwa ameambatana na maafisa mbalimbali na askari polisi alisema hataki kuona miti iliyopandwa kupitia kampeni ya upandaji miti iliyozinduliwa Septemba 23,2017 yenye kauli mbiu ya ‘Shinyanga Mpya,Mti Kwanza’ inakufa kwa uzembe kwani walikubaliana kila mwananchi atunze miti hiyo.

“Miezi mitano iliyopita tulianzisha kampeni ya upandaji miti wilayani hapa ili kuboresha mazingira na kupambana na mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha jangwa,tukapanda miti na kumtaka kila mwananchi atunze iliyopo kwenye eneo lake”,alieleza Matiro. “Nimeanza kukagua miti hii ili nione imefikia hatua gani,kama mti uliopo kwenye eneo lako lazima tukuwajibishe,wote tuliokuta miti imekauka tumewapiga faini ya shilingi 50,000/=”,aliongeza.

Matiro alisema wilaya hiyo imepiga marufuku kwa mifugo kuzurura mitaani,ikikamatwa kwa kila mfugo faini ni kati ya shilingi 50,000/= na 100,000/=,iwe ng’ombe,mbuzi,kondoo au punda, tukikuta mti umekauka faini ni shilingi 50,000/=. Afisa Misitu wa Manispaa ya Shinyanga,Emmanuel Nyamwihura alisema wanatoza faini hizo kwa mujibu wa sheria ya Usafi na Mazingira ya Mwaka 2014.
 
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro ameendesha oparesheni ya usafi na Mazingira kukagua usafi na miti.

Kupitia oparesheni hiyo amewawajibisha Wananchi ambao miti yao imekufa kwa kuwalipisha faini ya Shilingi 50,000 kwa mti na kuwataka wapande mingine.

View attachment 701866
Pichani ni; Wananchi ambao miti iliyopandwa mbele ya makazi au biashara zao imekufa wakipanda kwenye gari la Jeshi la Polisi
Maisha haya unamlipisha mtu fine isiyo na maelezo tena ya elfu 50!!? Kwa mti uliokufa wenyewe!? Tumelaaniwa
 
Mtu wa kwanza kutafuta kivuli cha mti ni wewe. Lakini kwa ujinga hujui nani alipanda huo mti. Tumelaaniwa kwa kutopanda miti .hatafu wakamatwe wote wasiopanda na kutunza miti wakati waitegemea
Maisha haya unamlipisha mtu fine isiyo na maelezo tena ya elfu 50!!? Kwa mti uliokufa wenyewe!? Tumelaaniwa
 
Mtu wa kwanza kutafuta kivuli cha mti ni wewe. Lakini kwa ujinga hujui nani alipanda huo mti. Tumelaaniwa kwa kutopanda miti .hatafu wakamatwe wote wasiopanda na kutunza miti wakati waitegemea
Ww umepanda mingapi
 
Mm namuunga mkoni dada mange tukaandamane tu tupate katiba mpya hakuna namna sasa

Juzi kaja "mtawala" sio kiongozi mtaani kwangu kaja kuulizia (ada???) ya kubeba taka. Anataka 5k, nikamwambia sio tatizo, ila sikuwa najua kumbe hata wanabeba taka(yaani hata kuwaeleza wananchi wake kuwa kuna huo utaratibu hawezi siju amepewaje hilo jukumu). "Anyway" nikamwambia njoo baadae kwa sasa nina kazi zangu(hapa home nina ka ofisi ka nyumbani).

Kaja leo nikamwuliza (hapa nimepanga kuna nyumba tatu) wale wengine wanalipa shs ngapi(kaya jirani zangu zina wapangaji kuanzia wanne)? Akaanza kumung'unya maneno. Nikambandika lingine, hivi mimi(naishi peke yangu) mmoja nalipa sawa na familia yenye watu 8? Kimya. Nikawa nawaza eti naye huyu katumwa na watu tunawaita viongozi(ki ukweli ni watawala tu kama baba yao) wameshindwa kuweka utaratibu mzuri ili vitu kama hivi kuwe na "rationale" sahihi ya kulipia hiyo huduma??? (by the way si tunalipa kodi na baba amesema anakusanaya sana sasa wezi kawamaliza???)

Anyhow nimetoa tu mfano wa jinsi ambavyo utawala huu umeshindwa kabisa(na hii ni kwa ngazi zote, huu ni mfano mdogo tu) kutengeneza watu wenye ubunifu, wamebaki kutenda kumfurahisha BABA MTUKUFU ambaye kawazidi hata wale mitume tunaowaamini(kwa wanaoamini).

MUNGU WABARIKI WATANZANIA(MAANA TANZANIA? ILISHABARIKIWA TAYARI).

muchetz.
 
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro ameendesha oparesheni ya usafi na Mazingira kukagua usafi na miti.

Kupitia oparesheni hiyo amewawajibisha Wananchi ambao miti yao imekufa kwa kuwalipisha faini ya Shilingi 50,000 kwa mti na kuwataka wapande mingine.

View attachment 701866
Pichani ni; Wananchi ambao miti iliyopandwa mbele ya makazi au biashara zao imekufa wakipanda kwenye gari la Jeshi la Polisi
Ukiwa ccm. Unakuwa na akili za kushikiwa. Kwa kawaida watu wanapanda miti kipind cha masika, sasa na kiangazi chote hiki tena shinyanga ilivyo Kane...hawa viongozi wanatumia madaraka vibaya, mafuta ya gari kuwakamata wanachi kwa ujinga wao.
Tanzania ya vi-wender
 
Siwapendi Ma-DC ila kama wataamua kusimamia mambo ya msingi kama upandaji wa miti nitawaunga mkono
 
Back
Top Bottom