Shigongo, kama biashara imekushinda, funga kampuni

Shigongo, kama biashara imekushinda, funga kampuni

chakii

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
21,564
Reaction score
28,453
Habari wanaJF

Kuna hii kampuni inaitwa Global Publishers ikiwa chini ya Bw. Erick Shingongo, kiukweli sidhani kama alisajili kampuni hii kwa ajili ya kuingilia faragha za watu lakini ndiyo kazi ambayo Global Publishers wanayoifanya kwa sasa.

Hapo awali Global Publishers walikuwa wakijikita zaidi katika uandishi wa majarida na vitabu lakini naona hiyo kazi wameona haiwalipi na hivi sasa wanazunguka kwenye nyumba za kulala wageni walipoweka kambi zao ili kudakua faragha za watu wanaofika katika nyumba hizo za kulala wageni wakiwa katika starehe zao.

Sitetei uzinifu lakini faragha ya mtu iheshimiwe, na siyo kazi ya Global Publishers kuwapiga chabo na kupiga picha bila idhini ya wahusika, huu ni udhalilishaji unaofanywa ma Global Publishers.

Wizara ya habari na utamaduni wakishirikiana na Brela waimulike tena hii kampuni huenda imesahau majukumu yake au imeshindwa kujiendesha kihalali.

Kuingiza hela kupitia udhalilishwaji wa watu fulani haikubaliki.
 
Kuna jamaa ana hasira nao sana na ameanza kuwafuatilia kama nao ni watakatifu kiasi hicho....wasishangae faragha zao nazo zikawa kwenye magazeti.....
 
sio vizuri kuingilia faragha za watu ila kwa namna flani inasaidia kupunguza faragha zisizo za halali... hawawezi kukufata na kukufotoa ukiwa na mkeo
 
nasikia shi(fimbo) siku hizi ana papazari wake wao kazi yake ni kuzunguka kwenye ma guest ya watu, kwenye parking za magari watu wanakupiga picha paparazi halafu wanakwambia eti utoe hela la sivyo kesho yake utajiona kwenye gazeti..
usipotoa pesa kesho yake utajikuta uko kwenye ukurasa wa mbele wa magazeti pendwa ya BUNDUKI, JUMAPILI, mbaya zaidi wanawafotoa wapenzi
 
GPL Kupitia OFM wanafanya kazi nzuri,Mtoa mada umeweka faragha tu lakini hawa Jamaa wapo kila sector kama unakumbuka walishaenda muhimbili na kujifanya madktari na kutibu wagonjwa,pia walishaenda kwenye ferry magogoni na kuingiza kitu mithili ya bomu bila kustukiwa,kwa kufanya hivyo wanawafumbua macho watu husika hivyo kuweka umakini na ndio maana katika hospital madaktari wengi feki wamekamatwa,ferry kwa sasa ukivuka kuna ukaguzi na pia JWTZ...Wezi wa Wake za watu nao wapo makini siku hizi.
 
Kumpiga mtu picha bila ruhusa sio jambo zur japo watu wanachukulia poa mfano upo kwenye harus watu wanakupiga picha halafu ukakosa hela ya kuzikomboa zile picha wanaondoka nazo na ww usijue wataenda kuzifanyia nn
 
Kuna jamaa ana hasira nao sana na ameanza kuwafuatilia kama nao ni watakatifu kiasi hicho....wasishangae faragha zao nazo zikawa kwenye magazeti.....

Mi namjua...ni yule padri aliyekuwa anabanjuka garini..
 
Hawa wawajibishwe wamevunja ndoa nyingi za watu.
 
Hawa GPL wanafanya makosa sana, nashangaa na serikali nayo iko kimya! Haki ya faragha inapotezwa kabisa!
Serikali ipi hiyo unayoizungumzia wewe ,Kama Tanzania hakuna serikali kuna uozo tu
 
  • Thanks
Reactions: ato
Huyo mwandishi arubaini yake haijamkuta.... ipo siku atakutana na wenye akili mbili...


nasikia shi(fimbo) siku hizi ana papazari wake wao kazi yake ni kuzunguka kwenye ma guest ya watu, kwenye parking za magari watu wanakupiga picha paparazi halafu wanakwambia eti utoe hela la sivyo kesho yake utajiona kwenye gazeti..
usipotoa pesa kesho yake utajikuta uko kwenye ukurasa wa mbele wa magazeti pendwa ya BUNDUKI, JUMAPILI, mbaya zaidi wanawafotoa wapenzi
 
nitashangaa sana kama askofu atamfukuza kazi yule padri.
ile ilikua ni faragha zao haikupaswa kuingiliwa
 
Mambo yako ukienda kufanyia kwenye sehemu za gharama kidogo haya mambo hayapo. Ila kama ukifanyia kwenye kichochoro lazima yakukute.
 
Nimecheka sana watu wanavyopigania uhuru wao wa faragha!..lol
 
Back
Top Bottom