chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 21,564
- 28,453
Habari wanaJF
Kuna hii kampuni inaitwa Global Publishers ikiwa chini ya Bw. Erick Shingongo, kiukweli sidhani kama alisajili kampuni hii kwa ajili ya kuingilia faragha za watu lakini ndiyo kazi ambayo Global Publishers wanayoifanya kwa sasa.
Hapo awali Global Publishers walikuwa wakijikita zaidi katika uandishi wa majarida na vitabu lakini naona hiyo kazi wameona haiwalipi na hivi sasa wanazunguka kwenye nyumba za kulala wageni walipoweka kambi zao ili kudakua faragha za watu wanaofika katika nyumba hizo za kulala wageni wakiwa katika starehe zao.
Sitetei uzinifu lakini faragha ya mtu iheshimiwe, na siyo kazi ya Global Publishers kuwapiga chabo na kupiga picha bila idhini ya wahusika, huu ni udhalilishaji unaofanywa ma Global Publishers.
Wizara ya habari na utamaduni wakishirikiana na Brela waimulike tena hii kampuni huenda imesahau majukumu yake au imeshindwa kujiendesha kihalali.
Kuingiza hela kupitia udhalilishwaji wa watu fulani haikubaliki.
Kuna hii kampuni inaitwa Global Publishers ikiwa chini ya Bw. Erick Shingongo, kiukweli sidhani kama alisajili kampuni hii kwa ajili ya kuingilia faragha za watu lakini ndiyo kazi ambayo Global Publishers wanayoifanya kwa sasa.
Hapo awali Global Publishers walikuwa wakijikita zaidi katika uandishi wa majarida na vitabu lakini naona hiyo kazi wameona haiwalipi na hivi sasa wanazunguka kwenye nyumba za kulala wageni walipoweka kambi zao ili kudakua faragha za watu wanaofika katika nyumba hizo za kulala wageni wakiwa katika starehe zao.
Sitetei uzinifu lakini faragha ya mtu iheshimiwe, na siyo kazi ya Global Publishers kuwapiga chabo na kupiga picha bila idhini ya wahusika, huu ni udhalilishaji unaofanywa ma Global Publishers.
Wizara ya habari na utamaduni wakishirikiana na Brela waimulike tena hii kampuni huenda imesahau majukumu yake au imeshindwa kujiendesha kihalali.
Kuingiza hela kupitia udhalilishwaji wa watu fulani haikubaliki.