Shigongo: Hivi ndivyo nilivyomalizana na CCM

Shigongo: Hivi ndivyo nilivyomalizana na CCM

Jamaa kamalizwa and then anadai kamalizana? umemalizana kumalizwa!
Mnada wa Bank zinazokudai utasimamishwa kwa kauli za Kinana? kuwa utalipwa kidogo kidogo!
 
Ulikopa ili ufanye kazi ya CCM, umeshindwa kulipa deni lako kwa sababu CCM haijakulipa stahiki zako, wadeni wako wanataka kukufilisi kwa kushindwa kulipa deni...aliyesababisha yote hayo ni CCM hivyo "CCM inakufilisi E.Shigongo".
 
CCM ilisheni wanachama aisee...maana siamini kama watu wa aina hii wanajari wala kuipenda CCM.....Kazi ipo
 
Kwenye ukabila me simo...🙂
Usiyachukulie haya mambo siriazi. Ukiona ukabila unatajwa mara nyingi ni katika muktadha wa utani tu au matambiko kama alivyosema Nyerere kwa utani vile vile. By the way hata mimi ni Msukuma mkuu na tunataniwa sana kuwa tuko washamba. Hapa nilikuwa "namcheka" brother Shigongo kuwa kapigwa na chama changu cha kijani!
 
Kwisha habari yake Mashairi yote nilidhani karudi na check kumbe SOUND anajisifia kuwa Mwana Ccm kumbe haijui ..hiyo ccm yenyewe Tangu tupate Uhuru wanasema Nchi imeendelea lkn watoto wanakaa chini....sasa yeye asherehekea kupozwa kwa Maneno sijui Bank nao watatulizwa kwa Maneno ya Lumumba? Ukishauziwa Dhamana zako usije kujiliza tena humu!
Nilichogundua haka kajamaa ni kajanja kajanja na hapo kanajifanya kuisifia Ccm kakidhani ndiyo njia ya kusaidia kulipwa haraka..
Yaani wasukuma bwana..
 
Kichwa cha habari mi nilifikiri tayari keshalipwa.
Kijana pamoja na ngonjera zako hakuna hata single pen hutakayolipwa na hivi umeamua kumwaga mboga ndio kabisaaa.
Benki hazijui cha Lumumba wala msomali dhamana itabidi majembe azipige mnada,hukumbuki yaliyompata Capt J Komba we kalaga bao.
 
Ila Shigongo ungejua ulichokiandika? Dah! Kweli sijui tunaenda wapi.
Hebu we mwenyewe Shigongo fikiria na usomi wako wote unaingia mkataba ukiwa unajua unaweza lipwa au usilipwe halafu unatuambia eti ilikuwa ni risk kufanya hiyo kazi wakati hujui kama Chama kitashinda au la! Leo ndio umeweka wazi kile nilichoamini miaka yote kwamba CCM inatumia hela za serikali kujiendesha na sio hela za ruzuku na mapato yake. Ndio maana wakakimbilia kufuta sherehe za uhuru eti tunabana matumizi. Pumbavu sana.

Hvi Shigongo kumbe wanaposema wanaolalamika ni wapiga dili hawakosei kwa kiasi fulani? Wewe umepiga dili na sio haki mbele za Mungu unaejifanya unamwamini. Je? Ilitangazwa tenda na wewe ukashinda? Au mlipeana tu?

Shiigongo nilikuheshimu sana ila nimesoma hii makala mara mbili nashindwa kukushangaa! Unasema tupende kusema ukweli tusiogope wakati huo huo unatueleza ulivyokuwa unaogopa moyoni mwako hadi wafanyakazi wako waliliona hilo, na kwa nafasi yako ndani ya chama unaogopa kiasi hivyo vipi kuhusu mwananchi wa kawaida? Au wale wanamuziki waliokisaidia chama? Usiwadanganye wananchi ndugu yangu

Kuna bwana mmoja amekuuliza swali mbona wakati unafanya hilo dili hukusema? leo unadai unatangazia umma? Halafu unasema eti CCM sio kama watu tunavyokifikiria wakati huo huo Kinana anakuuliza mbona umeenda kusema hadharani wakati yeye alikuwa hayupo nchini? si ungemsubiri? then unaomba msamaha kua hukujua. CCM tunaijua haitaki tujue yanayofanyika ndani ya chama kwan mengi ni dili na wewe hilo unalijua usituchanganyie habari hapa

Ukweli utaendelea kubaki pale pale na unaujua usiwadanganye watu wakaingia matatizon bure. Na wakti mwingine fikiria kabla hujaandika humu JF habari kama hizi peleka kwenye magazeti yako
 
Kosa lako ni kufanya biashara na Chama tawala, huo uthubutu ndio uendelee nao hivyo hivyo hata wakati wa kudai malipo yako!! We ulisikiaga wapi chama tawala kinadaiwa tena na raia. Jamaa kakuuliza hiyo tenda ilitangazwa lini?
 
Ushapigwa mkwara unakuja kujishaua. Katika wanaCCM nisiowapenda (Mungu anisamehe) ni huyu bwana. Hata mwaka 2010 alipoangushwa kwenye kura za maoni kule Buchosa nilifurahi sana. Hakuna mwanaCCM mnafiki kumshinda huyu jamaa.
 
Hapo Shigongo tayari kamalizwa. Duh! Wazee wa chama sio kabisa.. wana mbinu. Wamemtuliza Erick kirahisi sana. Angeandika tayari kalipwa ingeeleweka. Ila hii ya ahadi za kisiasa tayari ndugu yetu kamalizwa.
 
wakina Lema na Lissu wakisema ukweli mnawaweka mahabusu.
 
Back
Top Bottom