Shida ya maji Dodoma itaisha lini?

Shida ya maji Dodoma itaisha lini?

Nipo Hapa Kwenye Hili Jiji Linaloitwa Dodoma Mtaa Wa Kisasa (Nyumba 300), Kuna Shida Ya Maji Hadi Unajiuliza Kweli Hapa Ndio Makao Makuu Ya Nchi?

Wananchi Wa Hapa Hupata Maji Sometimes Mara Moja Kwa Wiki Ama Inaweza Ikatokea Yasitoke Kabisa Ndani Ya Wiki Nzima Mfano Kwa Muda Huu Ni Almost Wiki Mbili Maji Hayajatoka Na Ni Hapa Hapa Mjini.

Je Huko Kwingine Hali Ikoje, Wahusika Tunaomba Msaada Kwenye Hili Wawasaidie Wakazi Wa Dodoma Kwenye Suala La Maji.
Dom na maji inabidi wakae wamalize tofauti zao.
 
Huku Nkuhungu huwa yànatoka Mara mbili kwa wiki.... Hatujawahi kukosa maji inapofika siku yetu ya maji kutoka.....
Upo Nkuhungu sehemu gani!?!
Kuna kipindi mitaa ya Nkuhungu ilikuwa inakosa maji hata wiki.
 
To be specific kule nyumba 300 hata hayo masaa hawajui.. watu wamejaza madumu ndani kama wauza maji ikitokea yametoka tu ni wanasombelea ndani kama hayatatoka mwaka mzima imagine
Kwa kweli hali ni mbaya sana
 
Ukitaka maji yapatikane Dodoma 24/7 iondoe ccm madarakani kwa kuichagua chadema.
Mkiwa vijiweni mnamsifu anaupiga mwingi kumbe hata kuoga hamuogi.
 
Nipo Hapa Kwenye Hili Jiji Linaloitwa Dodoma Mtaa Wa Kisasa (Nyumba 300), Kuna Shida Ya Maji Hadi Unajiuliza Kweli Hapa Ndio Makao Makuu Ya Nchi?

Wananchi Wa Hapa Hupata Maji Sometimes Mara Moja Kwa Wiki Ama Inaweza Ikatokea Yasitoke Kabisa Ndani Ya Wiki Nzima Mfano Kwa Muda Huu Ni Almost Wiki Mbili Maji Hayajatoka Na Ni Hapa Hapa Mjini.

Je Huko Kwingine Hali Ikoje, Wahusika Tunaomba Msaada Kwenye Hili Wawasaidie Wakazi Wa Dodoma Kwenye Suala La Maji.
Rais anawapa watu wa ndondo mil.92 duu

View: https://www.instagram.com/p/CxJT8G2RJ5X/?igshid=MTc4MmM1YmI2Ng==
 
Huku Nkuhungu huwa yànatoka Mara mbili kwa wiki.... Hatujawahi kukosa maji inapofika siku yetu ya maji kutoka.....
Kumbe wewe ni jirani yangu

Mimi sijui shida ya maji , ninapoishi tuna karo la maji huwa tunategeshea mpira siku ya maji kutoka yaingia karoni, then tunabaki kutumia tu.
 
Hongereni sana, japo sisemei kwa miaka hii ya karibuni.
Unazungumzia miaka gani jombaa? Nipo hapa more than 7 years.... Ratiba ipo constant.... Hatujawahi kukosa maji siku ya ratiba ya maji kutakiwa kutoka.
 
Ndo tatizo la kukomaa kutekeleza matamko kama mazuzu, kisa ilitamkwa sijui mwaka 1963 huko kwamba Dodoma ndo pawe makao makuu ya nchi basi watu bila kutumia akili ni kujiendea tu ili mradi wafanye siasa za kishamba.......Dodoma ni sehemu ambayo ni jangwa, kwa nchi inayojikongoja yenye vipaumbele lukuki kukomaa kutumia matrilioni ya pesa kujenga upya makao makuu jangwani ni ufinyu wa kifikra.....​
 
Back
Top Bottom