Shida sio CCM shida ni Watanzania

Shida sio CCM shida ni Watanzania

Habari Wakuu.

Ukiwa makini utaelewa kwamba hapa Tanzania shida sio CCM shida ni Watanzania wenyewe (ambao wanaunda CCM).

Hivyo basi hata kama chama kingine kikiingia Madarakani shida na vilio vitakuwa ni vilevile tena inawezekana ikawa zaidi. WHY? kwasababu shida sio chama shida ni watanzania wenyewe.
Shida ni ccm yenyewe💯
 
Habari Wakuu.

Ukiwa makini utaelewa kwamba hapa Tanzania shida sio CCM shida ni Watanzania wenyewe (ambao wanaunda CCM).

Hivyo basi hata kama chama kingine kikiingia Madarakani shida na vilio vitakuwa ni vilevile tena inawezekana ikawa zaidi. WHY? kwasababu shida sio chama shida ni watanzania wenyewe.
Uwezi kusema tumekwama pakubwa kama taifa halafu uiondoe ccm kwenye lawama ni big no ccm ndio iliyo tufikisha hapa Kwa mazuri na mabaya yake.
 
Kama ndugu na ndugu tu kuna visa vya wifu kutoshikiriana na ujinga ujinga mwingi tu nan unategemea aje avunjwe makanyagio kisa kizazi kingine?
Mimi naona kama CCM hawatupi mateso ilitakiwa tupewe mateso makodi ya ajabu,hali iwe ngumu kweli kweli dadeki mpaka mtu akiwa njiani awe anaongea peke yake na kutoa ulimi nje kama Mbwa😁😁
 
Mimi nachojua watz wengi wanakipenda chama cha mapinduzi, hasa watu waishio mijini hii ni kwa utafiti niliofanya. Atakayejaribu kunipinga ahakikishe naye amefanya utafiti kwani tafiti hupingwa kwa tafiti.
Tafiti zako umefanya Kwa wazee bila shaka rudia kufanya Kwa vijana halafu jibu Kaa nalo ata usilete hapa ila kuwa makini kwenye tafiti Yako
 
Habari Wakuu.

Ukiwa makini utaelewa kwamba hapa Tanzania shida sio CCM shida ni Watanzania wenyewe (ambao wanaunda CCM).

Hivyo basi hata kama chama kingine kikiingia Madarakani shida na vilio vitakuwa ni vilevile tena inawezekana ikawa zaidi. WHY? kwasababu shida sio chama shida ni watanzania wenyewe.
Mkuu,

Miaka michache iliyopita, Tundu Lissu alifanya ziara Marekani. Akawa anatembelea jamii za Watanzania walioko Marekani. Akafanya mahojiano na rafiki yangu mmoja ana media company, online radio. Tundu Lissu haogopi challenge, akawa anachukua maswali ya watu, anayajibu.

Katika maswali yale, nilimuuliza swali. Nikamwambia kuwa nimemsoma muandishi nguli wa kutoka Peru anaitwa Mario Vargas Llosa, huyu alishinda nishani ya Nobel ya literature mwaka 2010. Mario Vargas Llosa (amefariki April 13 2025 akiwa na niaka 89) hakuwa muandishi tu. Alikuwa mtu maarufu sana Peru, akaingia mpaka kuwania urais wa Peru.

Sasa katika kitabu chake kinachoelezea maisha yake kinaitwa "A Fish Out of Water", Mario Vargas Llosa alielezea uzoefu wake katika siasa. Akasema siasa ukiiangalia kutoka nje, kuisoma, kuiandika, ni tofauti kabisa na siasa unayoifanya mwenyewe in realpolitik.

Siasa ya kusoma, kuchambua na kuandika imejaa ushairi mwingi wa manifesto za kuboresha maisha ya watu, kupandisha elimu, kuongeza viwango vya maisha bora, kuongeza huduma za afya na mambo ya kupandisha uchumi, mambo ya falsafa za kuweka watu pamoja, na mengine mengi kama hayo.

Mario Vargas Llosa alisema kuwa siasa ya ukweli ngunguru ngangara ile ya realpolitik wachezaji wenyewe uwanjani inajali mambo mawili tu.

Kupata power, na ukishapata power, kuendelea kuwa kwenye power. Hayo mengine yote ni usanii tu.

Nikamwambia Tundu Lissu, kwanza asante sana kwa kazi nzuri mnayoifanya. Tunahitaji a strong alternative party. Lakini, kwa maneno haya ya Mario Vargas Llosa, tutaamini vioi CHADEMA mkipata power hamtatugeuka na kufanya yaleyale ya CCM au vibaya zaidi?

Tundu Lissu kwanza akayakubali kifalsafa maneno ya Mario Vargas Llosa, na akasema hiyo ndiyo sababu wananchi hawatakiwi kuwaachia viongozi tu waendeshe nchi. Wananchi wanatakiwa kuchujua ownership ya nchi yao na ku participate kuhakikisha wana uongozi wenye transparency na integrity. Institutionally.

Bila ya hivyo hata CHADEMA hawatafauku mitego ya uongozi.

Sasa nikajiuliza, kwa wananchi hawa hawa Watanzania na elimu hii hii au itabidi tukodishe wananchi kutoka nje?
 
Mkuu,

Miaka michache iliyopita, Tundu Lissu alifanya ziara Marekani. Akawa anatembelea jamii za Watanzania walioko Marekani. Akafanya mahojiano na rafiki yangu mmoja ana media company, online radio. Tundu Lissu haogopi challenge, akawa anachukua maswali ya watu, anayajibu.

Katika maswali yale, nilimuuliza swali. Nikamwambia kuwa nimemsoma muandishi nguli wa kutoka Peru anaitwa Mario Vargas Llosa, huyu alishinda nishani ya Nobel ya literature mwaka 2010. Mario Vargas Llosa (amefariki April 13 2025 akiwa na niaka 89) hakuwa muandishi tu. Alikuwa mtu maarufu sana Peru, akaingia mpaka kuwania urais wa Peru.

Sasa katika kitabu chake kinachoelezea maisha yake kinaitwa "A Fish Out of Water", Mario Vargas Llosa alielezea uzoefu wake katika siasa. Akasema siasa ukiiangalia kutika nje, kuisoma, kuiandika, ni tofauti kabisa na siasa unayoifanya mwenyewe in realpolitik.

Siasa ya kusoma, kuchambua na kuandika imejaa ushairi mwingi wa manifesto za kuboresha maisha ya watu, kupandisha elimu, kuongeza viwango vya maisha bora, kuongeza huduma za afya na mambo ya kupandisha uchuni, mambo ya falsafa za kuweka watu pamoja, na mengine mengi kama hayo.

Mario Vargas Llosa alisema kuwa siasa ya ukweli ngunguru ngangara ile ya realpolitik wachezaji wenyewe uwanjani inajali mambo mawili tu.

Kupata power, na ukishapata power, kuendelea kuwa kwenye power. Hayo mengine yote ni usanii tu.

Nikamwambia Tundu Lissu, kwanza asante sana kwa kazi nzuri mnayoifanya. Tunahitaji a strong alternative party. Lakini, kwa maneno haya ya Mario Vargas Llosa, tutaamini vioi CHADEMA mkipata power hamtatugeuka na kufanya yaleyale ya CCM au vibaya zaidi?

Tundu Lissu kwanza akayakubali kifalsafa maneno ya Mario Vargas Llosa, na akasema hiyo ndiyo sababu wananchi hawatakiwi kuwaachia viongozi tu waendeshe nchi. Wananchi wanatakiwa kuchujua ownership ya nchi yao na ku oarticipate kuhakikisha wana uongozi wenye transparency na integrity. Institutionally.

Bila ya hivyo hata CHADEMA hawatafauku mitego ya uongozi.

Sasa nikajiuliza, kwa wananchi hawa hawa Watanzania na elimu hii hii au itabidi tukodishe wananchi kutoka nje?
Inawezekana ndio Kwa wananchi awa kinachoitajika ni viongozi bora na wazalendo kabisa.
 
Inawezekana ndio Kwa wananchi awa kinachoitajika ni viongozi bora na wazalendo kabisa.
Viongozi wanatokana na wananchi. Yani uongozi unaanza kufundishwa tangu kwenye familia mtoto anavyokuzwa.

Sasa kama jamii imeharibika haifundishi watu uongozi tangu chini huku unategemeaje watajua uongozi bora wakiwa juu?

Yani mtoto unampiga makwenzi tu unam bully tangu mdogo, anajua ukiwa mkubwa ni haki yako kupiga wadogo zako, na yeye anasubiri awe mkubwa apige wadogo, siku huyu mtu akiwa rais unategemea atakuwa na heshima na uongozi wa kidemokrasia?

Si ndiyo ataona na yeye zamu yake ya kupiga watu imefika, kasubiri kwa utulivu sana sasa ana haki ya kupiga wenzake kama alivyopigwa yeye?
 
Mkuu,

Miaka michache iliyopita, Tundu Lissu alifanya ziara Marekani. Akawa anatembelea jamii za Watanzania walioko Marekani. Akafanya mahojiano na rafiki yangu mmoja ana media company, online radio. Tundu Lissu haogopi challenge, akawa anachukua maswali ya watu, anayajibu.

Katika maswali yale, nilimuuliza swali. Nikamwambia kuwa nimemsoma muandishi nguli wa kutoka Peru anaitwa Mario Vargas Llosa, huyu alishinda nishani ya Nobel ya literature mwaka 2010. Mario Vargas Llosa (amefariki April 13 2025 akiwa na niaka 89) hakuwa muandishi tu. Alikuwa mtu maarufu sana Peru, akaingia mpaka kuwania urais wa Peru.

Sasa katika kitabu chake kinachoelezea maisha yake kinaitwa "A Fish Out of Water", Mario Vargas Llosa alielezea uzoefu wake katika siasa. Akasema siasa ukiiangalia kutika nje, kuisoma, kuiandika, ni tofauti kabisa na siasa unayoifanya mwenyewe in realpolitik.

Siasa ya kusoma, kuchambua na kuandika imejaa ushairi mwingi wa manifesto za kuboresha maisha ya watu, kupandisha elimu, kuongeza viwango vya maisha bora, kuongeza huduma za afya na mambo ya kupandisha uchuni, mambo ya falsafa za kuweka watu pamoja, na mengine mengi kama hayo.

Mario Vargas Llosa alisema kuwa siasa ya ukweli ngunguru ngangara ile ya realpolitik wachezaji wenyewe uwanjani inajali mambo mawili tu.

Kupata power, na ukishapata power, kuendelea kuwa kwenye power. Hayo mengine yote ni usanii tu.

Nikamwambia Tundu Lissu, kwanza asante sana kwa kazi nzuri mnayoifanya. Tunahitaji a strong alternative party. Lakini, kwa maneno haya ya Mario Vargas Llosa, tutaamini vioi CHADEMA mkipata power hamtatugeuka na kufanya yaleyale ya CCM au vibaya zaidi?

Tundu Lissu kwanza akayakubali kifalsafa maneno ya Mario Vargas Llosa, na akasema hiyo ndiyo sababu wananchi hawatakiwi kuwaachia viongozi tu waendeshe nchi. Wananchi wanatakiwa kuchujua ownership ya nchi yao na ku oarticipate kuhakikisha wana uongozi wenye transparency na integrity. Institutionally.

Bila ya hivyo hata CHADEMA hawatafauku mitego ya uongozi.

Sasa nikajiuliza, kwa wananchi hawa hawa Watanzania na elimu hii hii au itabidi tukodishe wananchi kutoka nje?
Hongera Sana Mkuu pia nimefurahi Sana kuona wewe ni miongoni mwa-watu walio nielewa hoja yangu pamoja sana Mkuu. Ujue Watu wanalalamika tu kuhusu chama lakini shida sio chama shida ni jamii(Watanzania )hata kama chama kikibadirishwa.
 
Habari Wakuu.

Ukiwa makini utaelewa kwamba hapa Tanzania shida sio CCM shida ni Watanzania wenyewe (ambao wanaunda CCM).

Hivyo basi hata kama chama kingine kikiingia Madarakani shida na vilio vitakuwa ni vilevile tena inawezekana ikawa zaidi. WHY? kwasababu shida sio chama shida ni watanzania wenyewe.
Shida siyo watanzania shida ni Msoga
 
Viongozi wanatokana na wananchi. Yani uongozi unaanza kufundishwa tangu kwenye familia mtoto anavyokuzwa.

Sasa kama jamii imeharibika haifundishi watu uongozi tangu chini huku unategemeaje watajua uongozi bora wakiwa juu?

Yani mtoto unampiga makwenzi tu unam bully tangu mdogo, anajua ukiwa mkubwa ni haki yako kupiga wadogo zako, na yeye anasubiri awe mkubwa apige wadogo, siku huyu mtu akiwa rais unategemea atakuwa na heshima na uongozi wa kidemokrasia?

Si ndiyo ataona na yeye zamu yake ya kupiga watu imefika, kasubiri kwa utulivu sana sasa ana haki ya kupiga wenzake kama alivyopigwa yeye?
Pia Kwa kuongezea Mkuu wananchi ambao tunawategemea kuwa viongozi sio wawajibikaji imeanzia kwenye ngazi za familia na kuendelea mpaka kwenye elimu za ngazi za juu.

Mfano nitakupa kwa wanafunzi wa Vyuo vikuu "Lecture anaweza toa kazi Leo J"nne akasema nahitaji hii kazi J"nne ijayo asilimia 95% ya wanafunzi wataifanya siku ya kukusanya yani asubuhi ya j"nne na wengine watakusanya hawaja maliza ikiwa walipewa wiki nzima. Sasa hiyo ndiyo jamii tuliyo nayo Tanzania.
 
Hongera Sana Mkuu pia nimefurahi Sana kuona wewe ni miongoni mwa-watu walio nielewa hoja yangu pamoja sana Mkuu. Ujue Watu wanalalamika tu kuhusu chama lakini shida sio chama shida ni jamii(Watanzania )hata kama chama kikibadirishwa.
Naam,

Lakini pia hatua moja ya kubadilisha jamii ni kujenga utamaduni wa kubadilisha chama tawala.

Kwa sasa hivi kuna watu wengi wameamini kwamba CCM ikitoka madarakani nchi itakuwa na machafuko. Kama wazee walivyoamini Nyerere akitoka madarakani nchi itakuwa na machafuko.

Hivyo sehemu ya kubadili mentality hii ya watu ni kubadili uongozi.

Tatizo watu wengi wanapenda majibu rahisi kwa maswali magumu.

Wanakuwa kama wale Wamarekani wanaotaka kuwe na kidonge cha kutibu matatizo yote. Kidonge au app ya simu.

Wakati kuna matatizo mengine ya jamii hayana shortcut. Hutakiwi kuchagua uongozi mzuri tu na kuuachia kila kitu. Uongozi unatakiwa kusimamiwa, ama sivyo utayumba.

Sasa kuusimamia uongozi maana yake ni kufanya kazi. Kusoma manifesto za vyama, kusoma bajeti, kuchambua ripoti, kufuatilia kazi za CAG, kudai habari, kudai haki, kulazimisha wabunge wabadili sheria, kufungua kesi mahakamani, kuandamana, kuhakikisha chaguzi zinakuwa za huru na haki, kulinda kura, kuelimisha wananchi.

Hii ni kazi kubwa, watu wengi wanapenda kulalamika lakini ukiwaambia fanyeni kazi hii na hii kupata mabadiliko mnayoyataka, wanakuwa wagumu. Sio tu wale ambao hawana elimu, ambao kwa kiasi fulani unaweza kuwa excuse kwamba mtu kama hana elimu unategemea vipi achambue mikataba na mambo ya uchumi kwa kina, bali pia hata hao wanaoitwa wasomi wengi wao ni wazembe.

Ndiyo maana utawasikia wengi hata upinzani wakiongea ni kupigana madongo personally, ad hominem attack, logical fallacies.

Ukimuuliza mtu naomba unielezee falsafa ya uchumi ya CHADEMA inasemaje, vipaumbele vya sera za CHADEMA kwenye uchumi ni vipi? Vinatofautianaje na vya CCM, watu wengi, hata hao wanaoitwa wasomi, hawawezi kukuelezea vizuri.

Kuna siku tulikuwa tumekaa tunaongea watu mbalimbali. Akaja jamaa mmoja kiongozi ongozi wa CHADEMA. Akawa anaongea sana. Sasa rafiki yetu mmoja akamuuliza swali. CHADEMA ina mrengo gani wa kisiasa? Inasimamia wapi? Right wing,? Far right? Center right, centrist, center left au far left?

Jamaa akawa anajiumauma hajui kaulizwa nini. Badala ya kutoa mrengo, akawa anatoa slogan za "Peoples Power".

Mpaka Godbless Lema akaingilia kumuokoa kujibu swali vizuri.

Watu wengi hawajali sera. Wanataka mtanange wa kuitoa CCM tu.

Hii inatengeneza uwezekano wa kuitoa CCM halafu watu wasijue cha kufanya baada ya kuiondoa CCM.

Kwa sababu focus yao yote ilikuwa kuiondoa CCM.
 
Kweli
Pia Kwa kuongezea Mkuu wananchi ambao tunawategemea kuwa viongozi sio wawajibikaji imeanzia kwenye ngazi za familia na kuendelea mpaka kwenye elimu za ngazi za juu.

Mfano nitakupa kwa wanafunzi wa Vyuo vikuu "Lecture anaweza toa kazi Leo J"nne akasema nahitaji hii kazi J"nne ijayo asilimia 95% ya wanafunzi wataifanya siku ya kukusanya yani asubuhi ya j"nne na wengine watakusanya hawaja maliza ikiwa walipewa wiki nzima. Sasa hiyo ndiyo jamii tuliyo nayo Tanzania.
 
Back
Top Bottom