fact only
JF-Expert Member
- Sep 9, 2024
- 975
- 1,356
- Thread starter
- #61
Mkuu shida ni Watanzania sio chama. Maelezo hayo tumeshajadiri Hapo juu. 👇👇CCM ndicho architect mkuu wa hali tunayoishuhudia leo, iwe ni watu kupigana vijembe, unafiki miongoni mwa viongozi, wasomi wazembe, au raia waliokosa uelewa wa kufuatilia mambo kwa kina. Hii ni kwa sababu chama hiki ndicho kilichoweka misingi ya mfumo wetu wa taifa tangu uhuru. Kama misingi hiyo ingekuwa imara na yenye maadili, leo tungekuwa tunavuna matunda ya maendeleo ya kweli. Huwezi kutenganisha msingi wa nyumba na uimara wa nyumba yenyewe. Vivyo hivyo, huwezi kutenganisha hali ya taifa hili na nafasi ya CCM. Hiki si chama tu kama vyama vingine, ni taasisi iliyoasisi mfumo mzima wa uongozi na maendeleo ya Tanzania. Hakujawahi kuwa na chama kingine kilichoshikilia hatamu kwa kipindi hicho chote, na kwa mantiki hiyo, hakuna namna ya kuitenganisha hali ya taifa letu na athari za CCM.
Lakini pia hatua moja ya kubadilisha jamii ni kujenga utamaduni wa kubadilisha chama tawala.
Kwa sasa hivi kuna watu wengi wameamini kwamba CCM ikitoka madarakani nchi itakuwa na machafuko. Kama wazee walivyoamini Nyerere akitoka madarakani nchi itakuwa na machafuko.
Hivyo sehemu ya kubadili mentality hii ya watu ni kubadili uongozi.
Tatizo watu wengi wanapenda majibu rahisi kwa maswali magumu.
Wanakuwa kama wale Wamarekani wanaotaka kuwe na kidonge cha kutibu matatizo yote. Kidonge au app ya simu.
Wakati kuna matatizo mengine ya jamii hayana shortcut. Hutakiwi kuchagua uongozi mzuri tu na kuuachia kila kitu. Uongozi unatakiwa kusimamiwa, ama sivyo utayumba.
Sasa kuusimamia uongozi maana yake ni kufanya kazi. Kusoma manifesto za vyama, kusoma bajeti, kuchambua ripoti, kufuatikia kazi za CAG, kudai habari, kudai haki, kulazimisha wabunge wabadili sheria, kufungua kesi mahakamani, kuandamana, kuhakikisha chaguzi zinakuwa za huru na haki, kulinda kura, kuelimisha wananchi.
Hii ni kazi kubwa, watu wengi wanapenda kulalamika lakini ukiwaambia fanyeni kazi hii na hii kupata mabadiliko mnayoyataka, wanakuwa wagumu. Sio tu wale ambao hawana elimu, ambao kwa kiasi fulani unaweza kuwa excuse kwamba mtu kama hana elimu unategemea vipi achambue mikataba na mambo ya uchumi kwa kina, bali pia hata hao wanaoitwa wasomi wengi wao ni wazembe.
Ndiyo maana utawasikia wengi hata upinzani wakiongea ni kupigana madongo personally, ad hominem attack, logical fallacies.
Ukimuuliza mtu naomba unielezee falsafa ya uchumi ya CHADEMA inasemaje, vipaumbele vya sera za CHADEMA kwenye uchumi ni vipi? Vinatofautianaje na vya CCM, watu wengi, hata hao wanaoitwa wasomi, hawawezi kukuelezea vizuri.
Kuna siku tulikuwa tumekaa tunaongea watu mbalimbali. Akaja jamaa mmoja kiongozi ongozi wa CHADEMA. Akawa anaongea sana. Sasa rafiki yetu mmoja akamuuliza swali. CHADEMA ina mrengo gani wa kisiasa? Inasimamia wapi? Right wing,? Far right? Center right, centrist, center left au far left?
Jamaa akawa anajiumauma hajui kaulizwa nini. Badala ya kutoa mrengo, akawa anatoa slogan za "Peoples Power".
Mpaka Godbless Lema akaingilia kumuokoa kujibu swali vizuri.
Watu wengi hawajali sera. Wanataka mtanange wa kuitoa CCM tu.
Hii inatengeneza uwezekano wa kuitoa CCM halafu watu wasijue cha kufanya baada ya kuiondoa CCM.
Kwa sababu focus yao yote ilikuwa kuiondoa CCM.