Shida ni Pikipiki au Udereva?

Shida ni Pikipiki au Udereva?

Wasalaam.Pikipiki ni usafiri wa haraka na pia imetoa ajira kwa vijana na faida kibao. Haipiti mwezi bila kusikia kifo kilichosababishwa na piki piki.Shida ni nini?je ni asili ya piki piki au udereva au miundombinu?
Shida ni udereva...
Kwa nchi ya magharibi ya mbali ni rahisi kupata leseni ya kuendesha gari lakini ni vigumu sana kupata leseni ya pikipiki.
 
Udereva: motorist wengi wanaendesha kihuni kwa kutozingatia alama yoyote ya barabarani. Pia wanafanya wana haraka kuliko watumiaji wengine wote wa barabara na wanataka wawe wa kwanza kana kwamba kuna mashindano.

Dharau kati ya motorist na drivers: wenye magari wanawaona motorists kama adui na kutojali uwepo wao barabarani.

Miundo mbinu: Barabara zetu nyingi ni nyembamba sana na hazina sehemu ya waendesha pikipiki na waenda kwa miguu, kama zipo basi zimejaa mashimo na ni nyembamba sana.

Madereva wengi wanajifunza udereva wa kuwasha, ingiza gia na kutembea bila kusoma alama za barabarani na tahadhari zingine muhimu.

Pombe na bangi pia vina mchango mkubwa katika ajali hizi.
 
Chanzo kikubwa cha ajali za byke ni uzembe wa madereva unaosababishwa na matumizi ya MIHADARATI na pombe kali,

unakuta dereva ana overtake main rod kizembe anajaa kwenye semi,
Kungekua na barabarani special kwa watu wa pikipiki, magari na waenda kwa miguu , ingepunguza , ndio manaa nikasema uendeshaji mbovu na miundo mbinu duni
 
Udereva: motorist wengi wanaendesha kihuni kwa kutozingatia alama yoyote ya barabarani. Pia wanafanya wana haraka kuliko watumiaji wengine wote wa barabara na wanataka wawe wa kwanza kana kwamba kuna mashindano.

Dharau kati ya motorist na drivers: wenye magari wanawaona motorists kama adui na kutojali uwepo wao barabarani.

Miundo mbinu: Barabara zetu nyingi ni nyembamba sana na hazina sehemu ya waendesha pikipiki na waenda kwa miguu, kama zipo basi zimejaa mashimo na ni nyembamba sana.
Samahani.Hivi, tofauti ya 1-motorists,2-drivers na 3-riders na 4--bikers ni ipi?
 
Kungekua na barabarani special kwa watu wa pikipiki, magari na waenda kwa miguu , ingepunguza , ndio manaa nikasema uendeshaji mbovu na miundo mbinu duni
mi naona waache uzembe na matumizi ya MIHADARATI na ulevi halafu wafate sheria za barabarani.

Apo vipi
 
Back
Top Bottom