Shibuda out

TAARIFA HII SIO YAKWELI, IPO KICHONGANISHI, haya mambo sio rasmi, tuweni makini. Jf itakuwa sasa kibanda cha kahawa!

Wewe ndiyo unasema siyo za kweli sisi tunakuambia ni za kweli sibiri muda utakuambia kama unatakuendelea kuufahamu ukweli mtafute mwanakamati kuu ya chama unayemfahamu then muulize, hata zitto mwenyewe waweza muuliza
 
Alitumia uhuru wa kutoa mawazo yake hivyo si vema kulaamu, mbona ya CCM huwa inaandikwa kwa utaratibu kama huu na kujadiliwa tena kwa kicheko.
Kikubwa ninahokiona ni kwamba ndani ya Chadema kuna watu wanajiona wao ndiyo wao na baadhi ya wengine kila wakisemaau kufanya kitu wanaonekana kama wasaliti / wamekosea kama ambavyo comrade Zitto anavyoandamwa na hasa kwa kuwa kwa kiasi fulani haelewani na Slaa na Mbowe kifikra, maana Zitto ana vision kubwa hivyo anaangalia na kuchambua mambo kwa mtazamo wa hali ya juu na kuona miaka kumi mpaka ishirini ijayo.

wacha habari zako ww,tangu lini zitto ukamfananisha na Dk Slaa??Dk Slaa is next level,ni sawa kifo na usingizi,vision ya Dk Slaa ni infinite. Nadhani U-premium member wako unaniti shaka na usikupe kibri cha Kuhadaa watu hapa jamvini,na ndio maana hujawahi kugongewa thanx hata moja hapa tangu ujiunge,sijui upo kwenye mlengo gani kifikra na kama unamuhusudu zitto hizo ni za kwako na si za jamvi...ebooo!!
 
Jamani nashindwa kuelewa,jamaa kama kasema ukweli ndio ulivyo,je, kwa nn unampangia maneno ya kuonge,eti asiongee ya ndani yaliyotokea.na mbona hilo la shibuda out umelipokea...je sio la ndani? halafu huyu dogo huyu Lema anamwambia zitto katumwa...hahaaa ni shida kweli kweli na huyu asipokaa sawa mwisho wa siasa zake za upepo uko karibu sana, au na yeye anatumwa na Mbowe? huu ni ulimbukeni tu unamsumbua lema .....na kama watu hawana nidhamu wataambiwa tu,kisa cha zito kumtetea shibda ni haki yake ya upenzi na uwezo wake wa kuona mbali,je mbowe anahofia shibudaa kumng'oa cheo na kukirudisha chama kanda ya ziwa?tusubiri tutaona mengi...mmejaribu kumchafua shibuda magazetini na jf lakini jueni shibua anaheshimika na kukubarika kuliko huyo slaa na mbowe..kwanza hawawezi kuwa marais wa nchi hii,mfanyabiashara na mwizi wa wake za watu....lema umechemka dogo...bado unasafari ndeeefu sanaaa.
 
wanaJF

kamati kuu ya chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) iliyokutana tarehe 30/4/2011 imeamua kumtoa shibuda kwenye nafasi ya kukaimu nafasi ya uenyekiti wa mkoa wa shinyanga, lakini kwnye kikao hicho nusura zichapwe kati ya lema na zitto baada ya lema, kumjia juu zitto ya kuwa mambo yote hayo ya shibuda kayasababisha yeye pale shinyanga kwa kuwaambia baraza la uongozi la mkoa kumteua shibuda kuwa kaimu mwenyekiti wakati katiba ya chama inasema kaimu mwenyekiti anapaswa kutokana na baraza la uongozi la mkoa,

huku shibuda akiwa si mjumbe wa baraza hilo, ndipo aliposimama zitto na kupinga kauli hizo ndipo wabunge na wajumbe wa kamati kuu walipo kuja juu na kumkumbusha zitto juu ya shibuda ya kuwa aliwatukana wabunge na akaambiwa aombe radhi akakataa na mpaka sasa hajaomba kwanini zitto unamtetea huyu jamaa, aliuza mjumbe huyo ambaye ni swahiba wa zitto bwana Msafiri mtemelwa




Wanataka kuleta GAMBA lao linoutukuza u kaskazini? Wanafikiria ni rahisi? tena wasipoangalia watakuja shy watatolewa nduki.Tena huyo mbunge aliyediriki kusema Shelembi ndo nani bora kaondoka maana alikuwa mzigo kwenye cc akae mkao wa kula.A taondoka ataicha CHADEMA SHY inanasonga mbele.
 
Kwa ufahamu wangu, kwenye chama kinachopenda kuwa wazi malumbano ni kawaida. Unajua Zitto pia ana mapungufu yake na Lema vile vile, ila kama alivyosema mmoja wa mchangiaji kwenye mada hii..kuna watu CDM wanajiona wao ndo wao mfano wazi ni Zitto. Kwa jinsi tunavyojua watu wa jimboni kwake, leo akitoka na kujiunga na CCM bado watampigia kura mtoto wao ila kwa kifupi ni unafiki. Lema yuko straight kama ilivyo watu wa Kaskazini, leo akisema anaingia CCM asitegemee atapata kijana yoyote anayemwunga mkono kwani tatizo si mtu bali ni CCM ya mafisadi...walete chama kingine au CUF yenye uongozi dhabiti na sera safi watapata kura siyo kwa Kigoma na Zitto wao. Hatutaki unafiki kwenye chama na kama akitaka aondoke hata leo CDM itabaki kuwa chadema na upinzani utabaki kuwa upinzani kwa kukemea maovu ya chama na kuelimisha wananchi.
 
Haya mambo yanayo ongelewa yawe ya ukweli au uongo ukweli utabaki palepale kwamba"ZITTO ANAIIMBA CHADEMA LAKINI MOYO WAKE UPO MBALI NA CHADEMA".nasema hivyo kwa sababu hakuna mgogoro wowote ninaoukumbuka ambao ulitokea cdm zitto asihusishwe.kila baya chadema zitto yupo.na hii hali itaendelea hivi hadi atakapojiengua mwenyewe CDM.zitto hana msaada wowote chadema zaidi ya kuleta migogoro.kadili siku zinavyoenda umaalufu wa cdm unapungua kigoma.je ni kwanini?
 
Conflicts kama hizi ni za msingi maana zinajenga! tatizo ni pale conflicts zinapotokana na ufisadi maana kuna waliofahidi ufisadi na wale wanaolia njaa! hapo huwa ni balaa!!. keep it up CDM! tofautieni kwa hoja za kujenga lakini mwisho muelewane na musiwe na vinyongo kama KIKWETE!
 
cdm tunataka msimamo na si undumilakuwili asieweza aachie ngazi,Lema naikubali kazi yako tahadhali! Usijerubuniwa ka Zitto,tunazidi muombea arudi kwenye mstari
 
Haya mambo yanayo ongelewa yawe ya ukweli au uongo ukweli utabaki palepale kwamba"ZITTO ANAIIMBA CHADEMA LAKINI MOYO WAKE UPO MBALI NA CHADEMA".nasema hivyo kwa sababu hakuna mgogoro wowote ninaoukumbuka ambao ulitokea cdm zitto asihusishwe.kila baya chadema zitto yupo.na hii hali itaendelea hivi hadi atakapojiengua mwenyewe CDM.zitto hana msaada wowote chadema zaidi ya kuleta migogoro.kadili siku zinavyoenda umaalufu wa cdm unapungua kigoma.je ni kwanini?

Nchi hii hakuna chama bali mikusanyiko ya wasaka tonge tu!! Haya jioneeni. CCM wanaparurana na kuvuana magamba huku CHADEMA wanataka kupigana. Mimi ni mshabiki wa LEMA kama LEMA ila si Chama lakini sasa naanza kujiuliza juu ya ukomavu wake kisiasa manane kauli zake zimekuwa za ngumi mbele!!
 
Jamani kama ni kweli watu tunao waamin kama viongoz wetu kwenye mapambano dhid ya wakoloni weusi waeshimiwa zitto na lema mnatuvunja moyo kaeni chin kubalianeni tafadhali tunawapenda tunawategemea msituangushe wana cdm. Shibuda usituaribie chama tafadhari ukiendelea tutaomba mkutano wa kitaifa kupiga kura ya kutokuwa na iman na wewe umetoka ccm umekuja cdm ni chama makin kwa watu makin chini ya uongozi makini unaoongozwa na katiba ya chama makin na si ujanja hivyo badilika, kama hayo yametokea wewe ndo sababu ukiona watu zaid ya watatu wanakukosoa kitu kimoja ujue kuwa udhaifu huo unao ivyo badilika
 
HEKO WAHESHIMIWA ZITTO NA LEMA KWA UKOMAVU WENU KIDEMOKRASIA:
HATA SIKU MOJA WALA MSIOGOPE KUKUBALIANA KUTOKUKUBALIANA KATIKA HOJA BILA CHUKI WALA MIZENGWE


Waheshimiwa Zitto, Lema na kamati kuu zima, napenda niwapongeze tena saaana kwa jinsi mnavyohakikisha kwamba NEMBO YETU YA 'DEMOKRASIA' kweli inafanya kazi kiukweli ndani ya chama katika vyombo vyetu vyote vya maamuzi.

Huo ndio ukomavu wa kidemokrasia, uwazi wa kuendesha mambo kuonyesha utayari wa CDM kuongoza taifa bila kwepo TABAKA LA WATEULE ndani ya chama ambao kauli zao hazipingwi. Nawapongeza pia kukataa kubariki maamuzi ya barabarani katika kuteuana ukaimu mwenyekiti huko Shinyanga. Mhe Shibuda sasa ajindae tu kuingia kwenye kinyang'anyiro katika kukijenga chama huku kwa ushirikiano zaidi.

Ndio demokrasia ndani ya vyama inapokomaa na baada ya hapo wote wawili kuendelea kusalimiana na kuendeleza harakati za kufanya kazi kwa pamoja zaidi kutetea maslahi ya umma wa Tanzania.

Nasema ni ndani ya CHADEMA tu ndimo kulimo kiwango hicho cha juu cha demokrasia na misingi ya maadili ya vipi kushika uongozi KWA KUZINGATIA ITIKADI YETU YA 'NGUVU NA MAMLAKA YA UMMA' katika kila tulitendalo na maamuzi tunayoingia.

Mwisho, chama bila mikiki mikiki ya ndani lakini kwa misingi ya disciplined democratic space exercising tayari ni marehemu mtarajiwa kama kilivyo CCM ambako tofauti tu ya maoni kesho yake mtu anakolimbwa kwa kile anachokiamini.

Well said bro
 
Conflicts kama hizi ni za msingi maana zinajenga! tatizo ni pale conflicts zinapotokana na ufisadi maana kuna waliofahidi ufisadi na wale wanaolia njaa! hapo huwa ni balaa!!. keep it up CDM! tofautieni kwa hoja za kujenga lakini mwisho muelewane na musiwe na vinyongo kama KIKWETE!

Pointi
 
Jamani nashindwa kuelewa,jamaa kama kasema ukweli ndio ulivyo,je, kwa nn unampangia maneno ya kuonge,eti asiongee ya ndani yaliyotokea.na mbona hilo la shibuda out umelipokea...je sio la ndani? halafu huyu dogo huyu Lema anamwambia zitto katumwa...hahaaa ni shida kweli kweli na huyu asipokaa sawa mwisho wa siasa zake za upepo uko karibu sana, au na yeye anatumwa na Mbowe? huu ni ulimbukeni tu unamsumbua lema .....na kama watu hawana nidhamu wataambiwa tu,kisa cha zito kumtetea shibda ni haki yake ya upenzi na uwezo wake wa kuona mbali,je mbowe anahofia shibudaa kumng'oa cheo na kukirudisha chama kanda ya ziwa?tusubiri tutaona mengi...mmejaribu kumchafua shibuda magazetini na jf lakini jueni shibua anaheshimika na kukubarika kuliko huyo slaa na mbowe..kwanza hawawezi kuwa marais wa nchi hii,mfanyabiashara na mwizi wa wake za watu....lema umechemka dogo...bado unasafari ndeeefu sanaaa.
<br />
<br />


Wewe ni Mkuki Moyoni au Mkuki Makalioni kwa hiyo unakusumbua unashindwa kukaa chini na kufikiri!!
Unawezaje kumfananisha Shibuda na Mbowe,on what grounds? Na kuhusu Slaa,huyo mwanamke aliyemchukua Slaa ni wa kwako? Au mkuki umepita kwenye hako kashimo katikati ya makalio yako kwa hiyo unakutekenya?
Kama mwanamke anakutambua wewe ni Mume wake kwa nn aende kwa mwanaume mwingine? Stop writing bulshit!! Just for ur information,Dr.Slaa is expecting a baby from Josephine in the next couple of dayz!!
Na wewe ukikaa legelege watu si tu watakuchukulia mkeo bali watakuja hata kulala naye kwenye hikohiko kitanda chako!
It is ur duty to protect ur wife,Kwanza mwanaume lijali hawezi kulalamika hadharani akichukuliwa Mke,ni Aibu na Matusi!!
Dr.Slaa is a great man and an African Legend!!
 
Conflicts kama hizi ni za msingi maana zinajenga! tatizo ni pale conflicts zinapotokana na ufisadi maana kuna waliofahidi ufisadi na wale wanaolia njaa! hapo huwa ni balaa!!. keep it up CDM! tofautieni kwa hoja za kujenga lakini mwisho muelewane na musiwe na vinyongo kama KIKWETE!

Hakika kama wangekuwa wanapinga kwa hoja ni vema na haki ila kwa kutaka kupigana!! Mimi binafsi naogopa naona kuna bundi ameeingila CHADEMA na mwisho wake yasije yakawa yale ya NCCR-Mageuzi kule Tanga ambapo watu walitokea madirishani na wengine kujichimbia chini ya meza. CHADEMA kuweni makini msije mkawa historia. Hizo chokochoko si dalili njema hata kidogo
 
ama kweli ww ni tumaini jipya la ukimwi(haemorhegic virus)yaani na wewe unadhani utaweza kusimama mbele ya umma na kutoa hotuba wakakuelewa?......yaani kwa taarifa yako wewe endelea kubeba mikoba ya wakubwa tu na kutumika kufanya umbeya humu, pia pole kwa ufupi wa uono wako huo.....sina maneno yanyofanana na wewe.................nikiamua kuongea kama ww utakimbia humu.
 
TAARIFA HII SIO YAKWELI, IPO KICHONGANISHI, haya mambo sio rasmi, tuweni makini. Jf itakuwa sasa kibanda cha kahawa!

Sasa wewe kipimo cha kujua kuwa huu ni ukweli au ni uongo ni upi? Si unaelezwa kinachoendelea? We brain yako ikoje. Aliyekuwa ndani ya kamati kaeleza kilichotokea we unasema sio kweli. Aya tuambie wewe ukweli ni upi?
 
<br />
<br />


Wewe ni Mkuki Moyoni au Mkuki Makalioni kwa hiyo unakusumbua unashindwa kukaa chini na kufikiri!!
Unawezaje kumfananisha Shibuda na Mbowe,on what grounds? Na kuhusu Slaa,huyo mwanamke aliyemchukua Slaa ni wa kwako? Au mkuki umepita kwenye hako kashimo katikati ya makalio yako kwa hiyo unakutekenya?
Kama mwanamke anakutambua wewe ni Mume wake kwa nn aende kwa mwanaume mwingine? Stop writing bulshit!! Just for ur information,Dr.Slaa is expecting a baby from Josephine in the next couple of dayz!!
Na wewe ukikaa legelege watu si tu watakuchukulia mkeo bali watakuja hata kulala naye kwenye hikohiko kitanda chako!
It is ur duty to protect ur wife,Kwanza mwanaume lijali hawezi kulalamika hadharani akichukuliwa Mke,ni Aibu na Matusi!!
Dr.Slaa is a great man and an African Legend!!

Mkuu ungetoa hoja na si kumtukana mwenzio Mkuki Moyoni!! Hujaonyesha ukomavu wa kupingana kwa hoja. Tukiendelea hivi kuna siku tutataka milango ifungwe ili tupigane humu ndani ya jamvi!!
 
Back
Top Bottom