Shibuda ni mpinzani?

Shibuda ni mpinzani?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,949
Reaction score
38,700
Inawezekana kweli ni mpinzani makini.

Nimeangalia mwenendo wake nimepata maswali mawili.

  1. Ni mpinzani dhidi ya mfumo mbovu wa CCM?
    Aliondoka kwa mbwembwe CCM hasa baada ya kutoshwa kugombea jimboni kwake kwa tiketi ya CCM, Ikumbukwe kwamba dhambi aliyoifanya ni kutangaza kutaka kupambana na JK kwenye mchakato wa uteuzi wa mgombea wa urais.
  2. Ni mpinzani wa upinzani?
    Kwa kauli na tambo zake amekuwa akibeza chama chake cha sasa na kuwakosoa kwa wazi viongozi wake na kuukosoa mfumo ama utaratibu wa chama hata kufikia kuchombeza kuwa CHADEMA kimejaa undugunaizesheni.
Tumweke fungu gani?
Ametuhumiwa kuihujumu CHADEMA kwa kuwaunga mkono Masalia na makundi ya wanachama wanaokivuruga, kwa nini hachukuliwi hatua? Ana turufu gani kwa chama? Au yanayosemwa dhidi yake ni propaganda za uchonganishi?
 
Shibuda ni game changer, ile dawa iliyotumika kumuondoa ras Chacha Wangwe haiwezi kufua dafu hapo.
 
Acheni ngano na magugu yakue pamoja kuongeza ukubwa wa luzuku, ila siku ya uchaguzi ngano itawekwa ikulu na magugu yatatupwa nje na kuchomwa moto!
 
Achana na Shibuda, kwani alikuja CDM kwa vile anaipenda si baada ya kutemwa CCM, mvutie pumzi afanye kosa la kikatiba CDM, then ataona moto wake, hivi atakwenda mahakamani na kushinda ambayo itakuwa aibu kubwa kwa CDM.
 
Shibuda ni game changer, ile dawa iliyotumika kumuondoa ras Chacha Wangwe haiwezi kufua dafu hapo.

Tumia uBongo (na sio sehemu nyingine ya mwili wako) kufikiri kuhusu unachopotaka kuposti...kabla hujafanya hivyo!
 
kwa hiyo mtu akiwa msema kweli anakuwa adui?
Ukweli upi anaousimamia Shibuda?

Je wakumbuka alichokisema kwenye mkutano mkuu wa CCM Dodoma? Pamoja na kumsifia JK kuwa ni kiongozi bora, alitamka kwamba atagombea urais na JK atakuwa kampeni meneja wake. Lakini yeye baadaye amewazodoa wanaotamka kugombea urais kupitia CHADEMA (akilenga uongozi wa juu) bila utaratibu.

Hebu nielimishe ni ukweli upi shibuda anausimamia?
 
hapa umenena mkuu......maneno ya hekima sana haya....

sidhani kama haxo maneno uliyomsifia nayo kama yana hekima kwa nchi kama Tz inayosifika kuwa na democrasia ya midomoni mwa watu pasipokua na vitendo vya democrasia
 
Achana na Shibuda, kwani alikuja CDM kwa vile anaipenda si baada ya kutemwa CCM, mvutie pumzi afanye kosa la kikatiba CDM, then ataona moto wake, hivi atakwenda mahakamani na kushinda ambayo itakuwa aibu kubwa kwa CDM.

sijakuelewa unachotaka kumaanisha
 
sijakuelewa unachotaka kumaanisha

Huyu sio CDM wa kweli, alikuja CDM kwa vile hakuwa na pa kwenda. Kumfukuza hiv hivi kwa matamshi ya reja reja anayoyatoa atakwenda mahakamani na atashinda. Wamvutie pumzi afanye kosa la kikatiba ya CDM, then atumuliwe. Namaanisha hivyo! au wasemaje
 
Back
Top Bottom