Shibuda ni mpinzani?

Shibuda ni mpinzani?

Hapo mkuu umenipa jibu kwamba Shibuda ana walio nyuma yake (ingawa ngumu kuthibitisha).

Kwa faida gani hasa?
Jambo usiloweza kulithibitisha ni majungu sasa je tuamini kuwa Msanii ni mtu wa siasa za majungu?
Chama
Gongo la mboto DSM


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hiyo ni thread mpya unayoweza kuianzisha.

Hapa namwongelea mwanasiasa Shibuda na mission yake CHADEMA.

Si umeshasema huwezi kuthibitisha sasa je majungu ndiyo yatakayoweza kuthibitisha?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Ngekewa kwa hivyo unatuaminisha kwamba wanasiasa ndivyo walivyo?
Je tunapaswa sasa kuwaamini?

Iweje tunafuata legacy zao huku tukitambua moyoni kwamba hawana uhalisia wa kiimani?

Shibuda yupo peke?
Wanasiasa hawaaminiki isipokuwa hatuna budi kuwatumia huku tukilipa gharama mkubwa kwa maslahi yao.

Tunawafuata kwa kuwa sisi wenyewe hatuwezi kukaa mbele aidha kwa kutoweza mikiki au kutopewa nafasi na hao waroho (wanasiasa) Baadhi yetu tunakubali kudanganywa kwa ahadi za uongo kwa kutishiwa kuwa hali iliopo kama amani itavurugika na kuondowa hata huo uhuru wa kukimbizana na riziki. Wengine kwa kuchoshwa kuona wachache ndio wananufaika na amani hiyo wanakubali kurubuniwa na wale waroho wengine ambao kama watapata madaraka basi nyimbo itakuwa ile ile ya kuwepo kwa amani , amani ambayo walishiriki kwa mikono yao kuiharibu ili wao wawe badala ya wale wa zamani.

Shibuda hayuko peke yake ingawa wengine huamuwa kufuja kule walikotoka na kusifu wanakokwenda na masilahi yao yasipotimia wanarudi na kuramba matapishi yao. Kwani kuna mpizani yoyote ambaye hapo awali hakuapa kukilinda CCM? Anachofanya Shibuda ni kujihakikishia kuwa ajira yake ataweza kuiomba kokote hali ikihitajika na wala hana haja ya kutukana.
 
MKUU Ngekewa,

Nadhani mwelekeo wako ni wa mtu aliyekata tamaa, watu waoga na wanaokata tamaa ni watu wasiofanikiwa maishani, japo nakuombea wewe ufanikiwe.

Naamini hakuna siasa za namna ya siasa za shibuda, ila kuna watu wa aina ya shibuda..anachokifanya yeye ni ubinafsi tu, yaani anatafuta namna ya siasa zinazoweza kumtambulisha yeye binafsi, ni selfcentred kind of person..siasa ni muunganiko wa watu wenye malengo fulani kwa kutumia serikali, lakini Shibuda ana aina yake na mfumo wake wa siasa..siasa za popo, si ndege wala si mnyama na kwa vyovyote aina ya siasa zake haitamvusha 2015! Ni vigumu kuaminika na hatoaminika tena kwa wapiga kura wake, awe amegombea cdm, ccm au binafsi..
Mark my word!

Wapo watu safi kwenye siasa, lakini siasa ni upinzani, kwa hiyo si wakati wote wanaonekana hivyo, ndo maana leo weka jina lolote la Mwanasiasa utapata wanaomsifu na watakaomponda lakini hiyo haiufanyi mchezo wote wa siasa uwe ni wa wezi watupu au wabinafsi watupu japo wezi wapo, hata kwenye dini wapo pia, hapa ni suala la mtu binafsi, lakini shibuda anataka asiwe na upande, anataka Ccm wampende na Chadema wasimchukie, huu ni unafiki, hakuna kitu kama hicho na hasa siasa zetu, atapotea kabisa maana kote hatoaminika!..ndo anakoelekea, kushindwa vibaya sana na kupotea
 
Last edited by a moderator:
Je wananchi wapenda amani! nipo nani ta kuwepo , Naanza na kusema kwamba eti Shibuda nae anajiita mpambanaji?

nasema hapana Shibuda kapoteza mwonekano wa kuitwa MBUNGE, Kwani amekuwa na sura mbili tofauti, Lakini Kwa walopitia falsa wanajua mahala popte kuna wafuta upepo kama Shibuda.

Shibuda nilishawahi kuongea nae kwa Takribani dakika 15 unaweza kuzani ni Mkombozi kumbe ni galasa kama aina ya akina Nchemba, Wasira na Mbatia.

Jamani akina MREMA Wapo wengi nao ni akina Shibuda Tahazali yangu kwa Shibuda 2015 hataingia mjengoni Kwanza Mwaka juzijuzi aliponea kwa KASULUMBAYI ndo alimpigia debe na kushinda UBUNGE.

Shibuda kapoteza Umaarufu kabaki DEBE TUPU!!!!!!!!
 
Philip unamkuza bila sababu kwa nini umeanzisha thread kwa ajili ya mtu mchovu kama huyo uliandika kwenye thread nyingine kwamba unajiandaa kwenda kupambana naye nenda mapema kutengeneza mfumo wa mawasiliano kule usimuachie
 
jamani shibuda ni ccm na ni mzigo kama alivyokuwa ccm,hapo CDM kaenda kuvuruga akimaliza anarudi ccm kama alivyofanya Mrema alipoingia NCCR-Mageuzi akavuruga,akaenda TLP nako amevuruga.

Uliona wapi mwenyekiti wa chama au bodi ambaye kazi yake ni kuendesha vikao na mikutano anakuwa yeye ndo mhasibu,mtunza fedha mlipaji,mchukua ruzuku na kila anakohamia anakuwa mwenyekiti taifa,hakuna wenye uwezo?

hao ndo tunawaita viongozi wa vyama vya upinzani,wanongoza upinzani au wanavuruga upinzani kukwamisha harakati za ukombozi?,shibuda anakitu gani,anamvuto gani ndani ya CDM zaidi ya kuwavuruga makamanda wapambanaji.

tusipoteze muda kujadili kina hamnazo kama kina shibuda
 
MKUU Ngekewa,

Nadhani mwelekeo wako ni wa mtu aliyekata tamaa, watu waoga na wanaokata tamaa ni watu wasiofanikiwa maishani, japo nakuombea wewe ufanikiwe.

Naamini hakuna siasa za namna ya siasa za shibuda, ila kuna watu wa aina ya shibuda..anachokifanya yeye ni ubinafsi tu, yaani anatafuta namna ya siasa zinazoweza kumtambulisha yeye binafsi, ni selfcentred kind of person..siasa ni muunganiko wa watu wenye malengo fulani kwa kutumia serikali, lakini Shibuda ana aina yake na mfumo wake wa siasa..siasa za popo, si ndege wala si mnyama na kwa vyovyote aina ya siasa zake haitamvusha 2015! Ni vigumu kuaminika na hatoaminika tena kwa wapiga kura wake, awe amegombea cdm, ccm au binafsi..
Mark my word!

Wapo watu safi kwenye siasa, lakini siasa ni upinzani, kwa hiyo si wakati wote wanaonekana hivyo, ndo maana leo weka jina lolote la Mwanasiasa utapata wanaomsifu na watakaomponda lakini hiyo haiufanyi mchezo wote wa siasa uwe ni wa wezi watupu au wabinafsi watupu japo wezi wapo, hata kwenye dini wapo pia, hapa ni suala la mtu binafsi, lakini shibuda anataka asiwe na upande, anataka Ccm wampende na Chadema wasimchukie, huu ni unafiki, hakuna kitu kama hicho na hasa siasa zetu, atapotea kabisa maana kote hatoaminika!..ndo anakoelekea, kushindwa vibaya sana na kupotea

Mkuu nakuaminia lakini kwa kweli mimimsio muoga bali imetokea kuwa nina tabia ya kuangalia ukweli na kuueleza kama ulivyo! Nikianzia na suala la wanasiasa ni kuwa wao ni binaadamu kama sisi na tabia yetu binaadamu ni kupenda kuwa mbele mbele ya wenzetu. Tunajitahidi kusoma , kufanya kazi za kuzalisha mali, biashara nk. vyote hivi tukiwa na lengo la kuona kuwa tunapata maisha bora kwetu na walio karibu yetu. Sasa mchukulie yule anaejitahidi kufikia malego haya kwa kuwa mbele katika kuwaongoza watu. Haijawahi kutokea kiongozi akajikosesha priviledges hata siku moja. Wamekuwa wakijifikira wao na kila mmoja utasikia ana lawama katika matumizi. Wala hakuna anaetowa chake kwa ajili ya Chama. Kulikuwa na mwaka hapa kiongozi fulani aliakidai chama chake kwa pesa za kampeni. Sijui Mkuu labda unao mfano wa kiongozi aliejitolea nafsi yake hasa zaidi ya maneno?
Unamshangaa Shibuda na kumuona mtu pekee kwa wanasiasa, kwani kafanya nini kikubwa zaidi ya ile tabia yetu ya kuangalia njia gani ya kufikia mradi wetu? Mbona kuna Viongozi wanaotowa maneno ya uchochezi wa dhahiri na tunawabeba juu? Huyu si Shibuda aliepokewa kwa shangwe alipotumia ujanja wa kutoka sehemu moja kwenda nyengine?
Shibuda si mjinga kama unavyofikiria wewe na hilo la kufikiri kuwa akitoka alipo atakosa ajira ya kisiasa. Kumbuka Shibuda hakuwa mtu anaejulikana kabla ya kutengeneza mazingira ya kuonekana kuwa anaonewa na CCM na ukweli wenyewe ni kuwa Shibuda si mmoja katika kundi la kutafuta umaarufu kwa njia za CHADEMA na ndio maana sasa anaonekana kuwa hafai kuwa katika kundi. Na kwa kutambua hilo ndio anajienguwa huku akiamini kuwa uchaguzi ujao utakuwa na mgombea binafsi na huko ndio atatupa karata yake.
 
duh!kazi kweli kweli!ukweli mzee,its like a sword!badala ya kujibu hoja mnatoa kashifa or mara makapi or mara masalia!u wont get far brother with the vision of ur part!badilisheni mbinu mkubwa!
 
Back
Top Bottom