Shibuda ashangiliwa na wabunge wa CCM

kweli kuna haja kwa viongozi wa chadema kumchukulia hatua za kinidhamu. hata hivyo haishangazi kwa mzee kama shibuda.huyu bado ni kada wa ccm. amekwenda chadema kutafuta ubunge,sitashangaa,baada ya miaka 5 atarejea nyumbani kwake ccm. chadema iwekeze kwa vijana. vijana ndio wameongoza mapinduzi tunisia na misri.
 
Mimi nafikiri CDM next time wawe makini na watu wanaotoka kwenye vyama vyao na kuingia CDM kwaajili ya kupata madaraka, mtu kama shibuda hakuingia CDM kwa kuwa anakipanda bali alifanya BANGUSILO (Tambara la kufutia miguu) ili kupata ubunge tu na maadamu aliupata basi kesha maliza.

Chakufanya CDM: kufanya utafiti je shibuda ameupata huo ubunge kwa kwasabu alijiunga CDM au Watu wa jimbo lake wananamkubali ?

Kumtayarisha kuanzia sasa mtu ambaye atakuwa mbadala wa shibuda.
 
Ukweli usiopingika ni kuwa Shibuda bado yuko CCM na anaweza kuwa msaliti mkubwa wa CHADEMA. Kwa wale wasiomjua vizuri hana sound background na amefika pale alipo kwa unafiki na kujipendekeza ndo maana mara nyingi hakomi kusema kuwa CCM imemlea. Hata Makamba alimstukia akaanza kumponda. Eti alitaka awe mgombea urais mwaka 2010! I think he is unfit for anything except sycomphancy.CHADEMA BEWARE!!!!
 
Nilifikiri ni mimi pekee yangu ambaye sikumuelewa huyu baba maana hakuna chochote alichangia kuhusu hotuba ya raisi.

Tuko wengi ndugu yangu tuliotoka Kapa katika mipasho ya huyo jamaa. Mimi nilishangaa sana kuona Bunge linageuka sehemu ya kuimbia taarabu au kughani mashairi. Kwa kweli Shibuda hajatutendea haki wapiga kura wake!!! Kama isingekuwa umaarufu wa CDM angekuwa hapo?
 
Hata leohapa JF kama unataka usifiwe wewe iponde CCM na JK unawezwa ukabebwa!!! sioni kwanini Shibuda mumshambulie mbona Mbowe mwenye kamwaga misifa mingi sana kwa Rais? Au kwakuwa Shibuda ni mtoto wa kambo? Nadhani aliyoyasema yote ni ya ukweli hasa ya Zanzibar mie binafsi nampongeza sana kwa ujasiri wake aendelee kuwa mwana demokrasia kwani yupo kwenye chama cha Demokrasia na Maendeleo aitumie vema Demokrasia yake.

YouTube - Mh. Freeman Mbowe ajadili hotuba ya Rais (Michuzi Blog)

Mh ulijitahidi sana kuja na lugha za ki neutral ili ufanane na great thinker sasa umeamua kuwa wazi kitu ambacho si kibaya ila kama great thinker declare interest hamna shida kwani hatuwezi kuwa wote hapa na mawazo sawa.suala siyo kuponda ni kukosoa,kushauri.na usichoke kuikosoa CDM ila usiiponde!
CHARACTER IS LIKE A PREGNANT YOU CANT HIDE IT.
tchao
 
Shibuda afukuzwe chamani haraka sana iwezekanavyo.Kwa jinsi alivyochangia bungeni nitashangaa kama ataendelea kuwepo.Bado ni mwana CCM hai ila alikuja CDM kuvuruga tu.Shibuda must Go,Aoneshwe mlango haraka sana,hatufai katika mapambano ya ukombozi wa nchi yetu
 
Huwa nawasoma humu jamvini viongozi makini wa chadema mara mojamoja.Dr Slaa,Mnyika,Zitto na wabunge wengine wa chadema akina Regia.Nawauliza swali naomba anyone of you can respond.Najua cdm kama chama kina utaratibu na kanuni zake.Mbunge wa cdm lazima awe mwanachama wa cdm.Kwa kuwa Shibuda amejidhihirisha wazi kuwa sio mwanachama wa chadema kwa kutokubaliana na falsafa ya nguvu ya uma na kuonyesha wazi kuwa ana chuki na mwenyekiti Mbowe.Anasema yeye ni m2 huria hawezi kubinafsishwa na wa2 wachache wenye fikra za ubinafsi.Hapa anaendeleza propaganda zilezile ambazo ccm wamekuwa wakitumia kuiangusha cdm na hasa viongozi wake.Sasa iweje tena na Mbunge ambaye najua lazima atakuwa amesaini kutii na kuheshimu uongozi wa chama chake.Kuna vikao vya chama huko ndo mahali sahihi shutuma kama hizi kuziweka hadharani sio bungeni wala kwenye vyombo vya habari!Kwa nini Shibuda asichukuliwe hatua?Naomba nieleweshwe jamani.Kama tuna hofu ya kupoteza jimbo hilo mi sioni tatizo kuliko kuwa na mashushushu wa ccm ndani ya chama chetu.
 
Jana nilivunjika sana moyo. Heri utukanwe na mtoto wa jirani, kuliko wako wa kumzaa. Inauma sana na ndio maana CCM walishangilia sana! Zilikuwa ni dakika kumi za mashambulizi kwa wanaCHADEMA na uongozi mzima! Nadhani hii inahusiana na bifu na Wenje,maana naona chama kilimpuuza na malalamiko yake ya kijinga.

Chadema kimeshakuwa chama kikubwa sasa, inabidi wawe na uwezo wa kuthubutu kuwachukulia hatua wanaovunja sheria na taratibu za Chama. Ilibidi waanze na Zitto! Hofu yangu ni kwamba itajengeka hisia kwa wanachama kwamba ukiwa mkubwa kwenye chama, hata ukikosea hakuna atakayekuchukulia hatua. Hii impunity ndio inayoiua CCM!

Shibuda anatufundisha umuhimu wa kuwa na katiba mpya yenye tume huru ya uchaguzi! Shibuda anajipendekeza kwa rais na CCM kwakuwa anajua watamlinda wakati wa uchaguzi! Watu kama wakina Cheyo na Mrema wasingekuwa ndumilakuwili kama tungekuwa na tume huru ya uchaguzi! CCM wanapenda kuwa na proxyies upinzani kwakuwa wanajua kuwa upinzani wanaweza kuuana wenyewe kisiasa kwa urahisi sana. It worked with NCCR, why not try it now?

Chadema wachukue hatua,shibuda hastahili kuwa na kadi ya chadema. Ameongea mengi hadharani, sirini anaongea mangapi? Chadema inawezaje kumshirikisha shibuda ktk mikakati yao ya maendeleo ya chama?Chadema ina sapoti kubwa sana ya vjana, hyo ndio hazina yao! Sio wazee kama shibuda ambao wanahesabu siku zao kisiasa. Bank on the youths!

WANGEANZA na wanafunzi wa kidato cha kwanza mwk 2010 ambao wan miaka 13.... hawa ndo wapiga kura wa keli 2015 MBOWE chukua kadi acha kuanagalia ukubwa wa ruzuku kwani tumetoka wapi??? 11to 48!!!!!!!!!!!!! aaaagggggghhhhhhhhhh
 
mohamedi vua shati lako la CUF angalia shibuda kaongea nn usitete ujinga wapombavu wakubwa nyinyi
ujingaujinga tu mtu mzima anajikomba nn kumbuka alichinywa mtu bariadi au nayo ni mipango
 
JAMANI NI VYEMA TUKAELEWA KUWA CHADEMA SASA NI CHAMA KIKUBWA, SI SAWA NA TLP, NRD, UDP, JAHAZI ASILI, NLD nk. Mnapokuwa ktk chama kikubwa ni lazima mtofautiane ktk mambo mengi mengine ni madogomadogo na mengine ni ya msingi. Mfano CCM ni chama kikubwa na sasa wanatofautiana sana ktk njia ya kutumia kuwashughulikia MAFISADI maana ktk watoa maamuzi MAFISADI pia wamo. Si vyema kusema SHIBUDA Afukuzwe, apewe ONYO au ATENGWE na CHAMA. CDM watakuwa hawajengi bali wanabomoa maana haitapata kutokea DUNIANI wote tukaamini na kuongea lugha moja ktk HOJA itakayokuwa mbele yetu. Hivyo kuvumiliana na kuchukuliana ni jambo la msingi ktk kujenga CHAMA CHA KIDEMOKRASIA kama ilivyo CDM.

Tukumbuke kosa lilishafanywa na VIONGOZI wa CDM kwa kuwapokea wakina PROF. KAHIGI, SHIBUDA, WENJE, NYIMBO na wengine wengi Bila kuwafanyia VETTING kama kweli hawa watu wanaamini ktk Demokrasia na Ideology za CDM au wanajiunga ili wapate nafasi ya Kugombea UBUNGE, najua muda ulikuwa hautoshi kwa VETTING kufanyika hivyo viongozi walikuwa na uamuzi wa aina tatu, moja wawapokee na kuwapitisha kugombea au wawapokee na wasiwapitishe kugombea ubunge au wasiwapokee kabisa. SASA viongozi wa CDM waliona ni BUSARA kuwapokea na kuwapitisha kugombea UBUNGE wapo walioshinda ndio hao wakina KAHIGI,WENJE na SHIBUDA na wapo walioshindwa kama mzee NYIMBO. SASA si sahihi kutumia hasira ktk kushughulikia matatizo yanayosababushwa na wageni hawa ndani ya CDM. Maana Viongozi wa CDM wakati wanafanya uamuzi wa kuwapokea na kuwapitisha wawe wagombea ubunge kupitia CDM iliwapasa watambue kuwa mbeleni kuna matatizo kama haya yanaweza kujitokeza, sasa yamejitokeza dawa si kutimuana dawa ni kuyakabili na kuyatatua kwa busara na mbinu za kisasa za usuluhishi wa mogogoro.

Tukumbuke SHIBUDA na wenzake walisha zoea ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI WA CCM, na siku zote walisha zoea kuwaogopa na kuwatii viongozi wenye nguvu ya kiserikali(dola) na kichama. Viongozi wa CDM hawana nguvu za DOLA hivyo kwa SHIBUDA kuwahofia ni ngimu. Pia tukumbuke SHIBUDA anaungomvi na Mbunge mwenzie wa CDM mh. WENJE na aliwapelekea viongozi wa CDM mgogoro huo wautatue lakini wameupotezea sasa SHIBUDA anaamini yeye anachukuliwa kama mtoto wa kambo CDM. Hivyo kauli nyingine zinatokana na Hasira alizonazo.

PIA wana CDM kumbukeni kauli za SITTA na MWAKYEMBE pia zinawaudhi viongozi wa CCM lakini wanazipotezea na kuandaa mkakati wa kichama kuwashughulikia, (naomba nieleweke sio kwamba nawaunga mkono, bali muelewe kwa wana siasa MASLAHI ( wachumia tumbo) kwao chama kwanza nchi na wananchi baadae) sasa CDM isiingie ktk mtego huo ktk kushughulikia suala la SHIBUDA ni lazima MASLAHI ya TAIFA yawekwe mbele na ya CHAMA yafuate baadae.

Kumbukeni SHIBUDA kwa zaidi ya miaka 40 yeye anaimba wimbo wa CCM hivyo inawezekana hajajijua kuwa sasa yupo CDM na wimbo wa CDM ni peoples power bila kujali nguvu za DOLA za kiongozi. AMINI nawaambia SHIBUDA itafika mahala atabaini CCM si nyumbani tena hivyo hatokuwa na jinsi bali kutii uongozi na chama cha CDM
 
jana hata mm nlumia sn na taarab alyo2imbia hyu mzee acye na hta chembe ya busara. Yan ckmwelewa mwnzo mwsho. Cdm vjana 2ko nyma yenu. Msvunjwe moyo na mpuuz km shibuda. Hana jipya keshazoea majungu. Kama vp fukuywha mbali.



Huyu mzee ni mpumbavu kabisa kwani anafikiri kuwa yeye ndiye aliyeisaiia chadema na kuwa hata akisimama kwa chama chochote anaweza kuibuka na ushindi kitu ambacho si kweli watu hawakuchagua shibuda, bali walichagua dr slaa na chadema hivyo wakaona wasipoteze kura zao kwa ccm kwanza pamoja na ushindi ni ushindi lakini si wakujivunia sana ukilinganisha na kina mr. II hivyo basi ajue kabisa hata ktk huo ubunge aliponea hupuchupu. kama alikuwa anajiona anakubalika na wananchi angebaki ccm. Amejaa tamaa na urafi wa madaraka m-bw-a yule.
 
Shibuda amepoteza sifa ya kuwa mpiganaji coz alibainisha wazi kuwa ni swahiba wa FISADI namba 1 (JMK). So sioni haja ya kuendelea kumuacha kwenye chama. Achinjiwe baharini kama CCM inavyowafanya wanachama wake wanaopinga ufisadi na uchafu mwingine wa CCM.
 
ni vema chadema wajue kuwa shibuda ni nyoka ndani ya chama, yule ni kada wa ccm ndani ya chadema CCM imeweka makada 2 miongoni mwao mmoja ni shibuda:embarrassed:
 
Huwa nawasoma humu jamvini viongozi makini wa chadema mara mojamoja.Dr Slaa,Mnyika,Zitto na wabunge wengine wa chadema akina Regia.Nawauliza swali naomba anyone of you can respond.Najua cdm kama chama kina utaratibu na kanuni zake.Mbunge wa cdm lazima awe mwanachama wa cdm.Kwa kuwa Shibuda amejidhihirisha wazi kuwa sio mwanachama wa chadema kwa kutokubaliana na falsafa ya nguvu ya uma na kuonyesha wazi kuwa ana chuki na mwenyekiti Mbowe.Anasema yeye ni m2 huria hawezi kubinafsishwa na wa2 wachache wenye fikra za ubinafsi.Hapa anaendeleza propaganda zilezile ambazo ccm wamekuwa wakitumia kuiangusha cdm na hasa viongozi wake.Sasa iweje tena na Mbunge ambaye najua lazima atakuwa amesaini kutii na kuheshimu uongozi wa chama chake.Kuna vikao vya chama huko ndo mahali sahihi shutuma kama hizi kuziweka hadharani sio bungeni wala kwenye vyombo vya habari!Kwa nini Shibuda asichukuliwe hatua?Naomba nieleweshwe jamani.Kama tuna hofu ya kupoteza jimbo hilo mi sioni tatizo kuliko kuwa na mashushushu wa ccm ndani ya chama chetu.

Bwana mchangiaji hebu jaribu kujiuliza utawafukuza wangapi? kuna yule anaitwa 30 kucaingia kwake hakuna tofauti na shibuda. Muhimu ni kuwa wamejulikana nia yao ni kuivuruga cdm. Pia wametoa fursa ya kitu cha kuweka kwenye katiba kuwa watu hawa wanaofifisha matumaini ya binadamu wadogo wadogo kwa kutumikia viongozi wa mafisadi wawecontrolled. cdm wanatakiwa wawe waangalifu na kuwa dharau. Chibuda mpaka sasa amewafaidisha cdm kuliko hasara anayotaka kuwapa. Hata hawa wanaopanga mikakati ya kina shibuda sina hakika kama wanauwezo wa kutathimini mambo (they are doing more of damage kwa ccm and the goverment than kuzisaidia hiyo nayo ni advantage nyingine). cdm wamejua ndani yao mna mamluki wakilitumia hili vizuri lina faida kwao, wakiamua kushindwa kua makini watasambaratika, choice is there for the to choose.
 
Back
Top Bottom