Shetani hakumdanganya Eva/Hawa

Shetani hakumdanganya Eva/Hawa

THE LINE

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2023
Posts
206
Reaction score
311
Shetani hakumdanganya Hawa na Adam kama baadhi ya viongozi wa dini na baadhi ya wapendwa katika dini wanavyosema na kumlaumu katika ibada zao isipokuwa shetani alimwambia Hawa ukweli.

Shetani alimwambia Hawa ukweli ambao Mungu hakutaka Adam na Hawa waujue. Katika bustani ya Eden Shetani/Ibilisi(nyoka) alimwambia Hawa mambo makuu mawili;

1. Wakila matunda waliyokatazwa watakuwa kama Mungu.

2. Wakila matunda waliyokatazwa hawatakufa.

Nikianza na jambo la kwanza, Shetani alimwambia Hawa kuwa wakila matunda ya mti waliokatazwa basi watakuwa kama Mungu kwa kujua mema na mabaya.

Kweli baada ya Adam na Hawa kula matunda waliyokatazwa walipata maarifa ya kutambua mema na mabaya na kufikia hatua ya kujitambua kuwa wako uchi na kuanza kujifichaficha. Mpaka hapa hakuna uongo uliosemwa na shetani. Rejea (mwa 3:1-12).

Katika jambo la pili, Mungu baada ya kugundua Adam na Hawa wamekula matunda aliyowazuia, wamepata maarifa na wamekuwa kama yeye kwa kujua mema na mabaya aliamua kuwafukuza kutoka katika bustani ya Eden ili wasije kujiongeza tena wakatwaa matunda ya mti wa uzima wakala wakaishi milele. Hii ina maana Shetani hakudanganya kwa maana Adam na Hawa wangefanikiwa kula tunda la mti wa uzima wasingekufa na wangeishi milele na hii inaonyesha shetani hakuwa muongo. Mungu mwenyewe anathibitisha hili jambo katika (mwa 3: 22-24)

Kwa kuzingatia hayo mambo wawili inaonyesha si kila kitokacho kwa shetani ni uongo au ni jambo baya kwa binadamu mana bila nyoka kutimba bustanini huenda binadamu bado angekuwa zezeta asiye na maarifa yoyote lakini pia bila Mungu kuingilia kati huenda binadamu tusingekuwa tunawaza kuhusu kifo na kupata majonzi ya kufiwa na wapendwa wetu mana tungeishi milele. Tafakari
 
... jambo moja ( kwa hayo maandiko) tuna hakika nalo; walikula lile tunda walilokatazwa. Swali, mbona hawakuwa kama Mungu? Mbona walikufa?

Huoni kwamba Shetani aliwaingiza chaka? Logic rahisi hivi nayo ni ngumu kueleweka? Makubwa utaelewa kweli?
 
... jambo moja ( kwa hayo maandiko) tuna hakika nalo; walikula lile tunda walilokatazwa. Swali, mbona hawakuwa kama Mungu? Mbona hawakufa?
Akikuelewa na aikane nafsi yake. Hiyo ni mumo kwa pale!😂😂😂
 
... jambo moja ( kwa hayo maandiko) tuna hakika nalo; walikula lile tunda walilokatazwa. Swali, mbona hawakuwa kama Mungu? Mbona walikufa?

Huoni kwamba Shetani aliwaingiza chaka? Logic rahisi hivi nayo ni ngumu kueleweka? Makubwa utaelewa kweli?
Jamaa someni kwa kuelewa na si kufuata nadharia za watu wengine.

Katika mwanzo 3:22-24 Mungu mwenyewe anathibitisha we ni nani mpaka upinge? Kuhusu kuwa kama Mungu, Mungu alisema mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu(Mungu na wenzake) na kuhusu kufa, Mungu ndiye aliyeingilia kati kabla ya kitendo cha kula tunda la mti wa uzima hakijafanyika, kwa maana wangekula wasingekufa.

Ila tunda la mti wa ujuzi walikula ndo maana wakajua mema na mabaya, Mungu akachukia akawahi wasile tunda la mti wa uzima wakaishi milele.

Mwanzo 22-24 inasema hivi; nanukuu

"22 Bwana Mungu akasema, Basi huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu,kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima,akala akaishi milele; ²³ kwa hiyo Bwana Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa: ²⁴ Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka makerubi upande wa mashariki mwa bustani ya Edeni na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima."

Kama na hapa usipoelewa basi samahani.
 
Shetani hakumdanganya Hawa na Adam kama baadhi ya viongozi wa dini na baadhi ya wapendwa katika dini wanavyosema na kumlaumu katika ibada zao isipokuwa shetani alimwambia Hawa ukweli.

Shetani alimwambia Hawa ukweli ambao Mungu hakutaka Adam na Hawa waujue. Katika bustani ya Eden Shetani/Ibilisi(nyoka) alimwambia Hawa mambo makuu mawili;

1. Wakila matunda waliyokatazwa watakuwa kama Mungu.

2. Wakila matunda waliyokatazwa hawatakufa.

Nikianza na jambo la kwanza, Shetani alimwambia Hawa kuwa wakila matunda ya mti waliokatazwa basi watakuwa kama Mungu kwa kujua mema na mabaya.

Kweli baada ya Adam na Hawa kula matunda waliyokatazwa walipata maarifa ya kutambua mema na mabaya na kufikia hatua ya kujitambua kuwa wako uchi na kuanza kujifichaficha. Mpaka hapa hakuna uongo uliosemwa na shetani. Rejea (mwa 3:1-12).

Katika jambo la pili, Mungu baada ya kugundua Adam na Hawa wamekula matunda aliyowazuia, wamepata maarifa na wamekuwa kama yeye kwa kujua mema na mabaya aliamua kuwafukuza kutoka katika bustani ya Eden ili wasije kujiongeza tena wakatwaa matunda ya mti wa uzima wakala wakaishi milele. Hii ina maana Shetani hakudanganya kwa maana Adam na Hawa wangefanikiwa kula tunda la mti wa uzima wasingekufa na wangeishi milele na hii inaonyesha shetani hakuwa muongo. Mungu mwenyewe anathibitisha hili jambo katika (mwa 3: 22-24)

Kwa kuzingatia hayo mambo wawili inaonyesha si kila kitokacho kwa shetani ni uongo au ni jambo baya kwa binadamu mana bila nyoka kutimba bustanini huenda binadamu bado angekuwa zezeta asiye na maarifa yoyote lakini pia bila Mungu kuingilia kati huenda binadamu tusingekuwa tunawaza kuhusu kifo na kupata majonzi ya kufiwa na wapendwa wetu mana tungeishi milele. Tafakari
Mkuu sasa kwani kabla ya kula haya Matunda walikuwa wanakufa?Kwani kabla ya kula hayo matunda walikuwa hawajui mema na mabaya?Kwani shetani yeye aliwahi kula hayo matunda?Unaposoma maandiko yoyote kabla ya kuhitimisha jiulize Maswali.

Issue kubwa kwenye simulizi hii ni utii.Ni kukosa imani kwamba Mungu aliyetuumba au aliyewaumba Adamu na Eva na Nia njema na ni Mwema.Ni kuamini kwamba Mungu alikuwa na Sinister Agenda dhidi ya Binadamu aliyomuumba.Ni mbegu ya Shaka,wasiwasi ambayo shetani aliipanda.

Aliipanda kwanza kurudia Maelekezo ambayo Mungu Aliwapa Adam na Eva na kumuaminisha Eva naye Eva kumuaminisha Adam kwamba Huyu Mungu sio mwema kama ambavyo anatuaminisha.Kosa lile ambalo lilimuangusha Ibilisi ndilo ambalo lilimuangusha Adamu.

So Always Shetani anachokwamba ni Muongo na ni Baba wa Uongo.Shetani kamwe hasemi ukweli wowote ULE
 
Mkuu sasa kwani kabla ya kula haya Matunda walikuwa wanakufa?Kwani kabla ya kula hayo matunda walikuwa hawajui mema na mabaya?Kwani shetani yeye aliwahi kula hayo matunda?Unaposoma maandiko yoyote kabla ya kuhitimisha jiulize Maswali.

Issue kubwa kwenye simulizi hii ni utii.Ni kukosa imani kwamba Mungu aliyetuumba au aliyewaumba Adamu na Eva na Nia njema na ni Mwema.Ni kuamini kwamba Mungu alikuwa na Sinister Agenda dhidi ya Binadamu aliyomuumba.Ni mbegu ya Shaka,wasiwasi ambayo shetani aliipanda.

Aliipanda kwanza kurudia Maelekezo ambayo Mungu Aliwapa Adam na Eva na kumuaminisha Eva naye Eva kumuaminisha Adam kwamba Huyu Mungu sio mwema kama ambavyo anatuaminisha.Kosa lile ambalo lilimuangusha Ibilisi ndilo ambalo lilimuangusha Adamu.

So Always Shetani anachokwamba ni Muongo na ni Baba wa Uongo.Shetani kamwe hasemi ukweli wowote ULE
Msingi wa hoja zetu ujikite katika mada kuu kwa kuzingatia vifungu vya biblia nilivyo nukuu na si kuleta hoja za jumla. Ukitumia hoja za jumla huwezi pata maana halisi ya nukuu hizo.

Note:
Huu uzi ukitumia common sense huwezi elewa, ila ukitumia critical sense kuusoma mbona utakubaliana na mimi.
 
Uongo +ukweli = Uongo
Ukweli + Uongo = Uongo
Ukweli + Ukweli = Ukweli
Uongo +Uongo = Uongo

Shetani aliongea Uongo Kwa sababu hakusema kweli yote.
Kama shetani alisema ukweli kama usemavyo, tuambie aadamu na Hawa wapo nyumbani kwako tuje kuwaona?
Au Babu yako mzaa Babu yupo?
 
Wazungu wasinge tutawala nafikiri hata sisi tungeweka hadithi zetu kwenywe kitabu kimoja, sadiki na chitemo , Juma na uledi , mutegeki na nyembo, akili na adili, chilunda apambana na chui , Lindu ampiga kampilima, chunguza na maua , asiye sikia la mkuu, androko na simba , fuata nyuki ule asali , na nk.
 
Uongo +ukweli = Uongo
Ukweli + Uongo = Uongo
Ukweli + Ukweli = Ukweli
Uongo +Uongo = Uongo

Shetani aliongea Uongo Kwa sababu hakusema kweli yote.
Kama shetani alisema ukweli kama usemavyo, tuambie aadamu na Hawa wapo nyumbani kwako tuje kuwaona?
Au Babu yako mzaa Babu yupo?
Soma uzi kwa umakini na vifungu nilivyonukuu utaona moja ya miongoni ya miti ya matunda waliokatazwa ni mti wa ujuzi wa mema na mabaya pamoja na mti wa uzima.

Adam na Hawa walifanikiwa kula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya wakapata maarifa ya kujua mema na mabaya, hata Mungu mwenyewe anakubali. Mwanzo 3:22-24

Adam na Hawa hawakufanikiwa kula tunda la mti wa uzima mana Mungu aliwahi kuwafukuza kabla hawajala. Endapo wangekula maneno ya nyoka yangetimia. Mungu mwenyewe anathibitisha hapohapo mwanzo 3:22-24.
Onyesha uongo wa shetani kwa kujikita katika mada.
 
Wazungu wasinge tutawala nafikiri hata sisi tungeweka hadithi zetu kwenywe kitabu kimoja, sadiki na chitemo , Juma na uledi , mutegeki na nyembo, akili na adili, chilunda apambana na chui , Lindu ampiga kampilima, chunguza na maua , asiye sikia la mkuu, androko na simba , fuata nyuki ule asali , na nk.
Ni kweli mana kabla ya ukoloni haya mambo hayakuwepo mababu zetu walikuwa na taratibu zao huko nyuma.
Ila kwa kuwa tulikubali kupokea tamaduni zao angalau basi tuzisome kwa kuelewa.
 
Back
Top Bottom