Sheria ya ndoa inahitaji maboresho

Sheria ya ndoa inahitaji maboresho

Shytown

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2025
Posts
468
Reaction score
791
Nilisikia kwenye Chombo cha Habari kuwa; Kwa sheria ya ndoa ya Tanzania, baba ndio anatoa hela za kila kitu kwenye Familia na hela ya Mke haihusu familia......

1. Baba ana wajibu wa kulea na kutunza familia ikiwemo kujenga nyumba, kulipa ada na kila kitu cha familia yake. Nikaona hii ni ile Sheria iliyopo kwenye Biblia ikieelekeza kuwa, kazi ya mama (mke) itakuwa ni kuzaa na kulea familia ikiwemo kuangalia maadili mema ya Watoto

Kimsingi hii sheria ilikuwa inafaa miaka ya 70 ambapo wanawake walikuwa wanakaa nyumbani kazi yao ni kuzaa na kuangalia familia LAKINI maisha yamebadilika kiasi kwamba wamama wanatoka Kwenda kufanya kazi na jukumu la msingi la mama ambalo ni kulea watoto anafanya dada wa kazi (house girl)

Sasa kama mama anatoka Kwenda kufanya kazi na kuacha jukumu lake la msingi kabisa la kulea Watoto afanye House girl; kwa nini sheria isitamke kuwa; kwa wale wanawake wenye kipato (waajiriwa/wafanyabiashara); kipato chao atashirikiana na baba kuendesha familia? Dunia imebadilika sana; wapo wanawake wengi tu wenye vipato vikubwa kuliko wanaume zao....iweje sheria yetu iwatenge kuchangia maendeleo ya familia?
HUO USAWA (50/50) WANAO DAI KILA SIKU, KWANINI HAUHUSISHI KUSHIRIKIANA MAJUKUMU KWA USAWA??

2. Kiwanja cha nyumba cha Baba/Mama
Kuna watu wana oana mmoja wao akiwa na kiwanja
Kulingana na mabadiliko ya Dunia, nafikiri ipo haja ya kuweka sheria vizuri kuwa; kama watu wataoana (ndoa) na kuridhiana kwa pamoja kujenga kwenye kiwanja cha mmojawapo; basi kile kiwanja walicho amua kujenga sio cha mmoja wao tena, bali ni sehemu ya nyumba (familia). Ina maana, huko baadae ikitokea kuna haja ya kugawana; Nyumba itahesabiwa ni Pamoja na kiwanja chake na hakuta kuwa na mmoja wao kudai kuwa alikuwa na kiwanja kabla ya kuoana....

Nasema hivyo kwani mambo yamebadilika; kuna mamluki wanaweza kutumia hiyo gape ya Sheria yetu kulazimisha wajenge kwenye kiwanja chake akijua huko mbeleni atadai chukua nyumba uniachie kiwanja changu, huku akilindwa na sheria....

Nawasilisha...
 
Hata hiyo biblia inawataka wanawake watoke wafanye kazi..... Mke mwema nani aweza kumuona? huamka alfajiri kufanya kazi na kuwapatia watu wa nyumbani mwake chakula.... and blaa blaa blaaa
Cha msingi hapa ni kuwa mtu ataambatana na mumewe na watakuwa kitu kimoja. Watachuma pamoja na kufanya kwa kushirikiana. Tatizo linakuja kwa vidume na vijike wanaotaka mtelezo, wanaowaza mwenzie afwe yeye arithi... 😀 😀 😀 😀 wanaowaza mwenzie ajenge yeye akae bureeeee
 
Nilisikia kwenye Chombo cha Habari kuwa; Kwa sheria ya ndoa ya Tanzania, baba ndio anatoa hela za kila kitu kwenye Familia na hela ya Mke haihusu familia......

1. Baba ana wajibu wa kulea na kutunza familia ikiwemo kujenga nyumba, kulipa ada na kila kitu cha familia yake. Nikaona hii ni ile Sheria iliyopo kwenye Biblia ikieelekeza kuwa, kazi ya mama (mke) itakuwa ni kuzaa na kulea familia ikiwemo kuangalia maadili mema ya Watoto

Kimsingi hii sheria ilikuwa inafaa miaka ya 70 ambapo wanawake walikuwa wanakaa nyumbani kazi yao ni kuzaa na kuangalia familia LAKINI maisha yamebadilika kiasi kwamba wamama wanatoka Kwenda kufanya kazi na jukumu la msingi la mama ambalo ni kulea watoto anafanya dada wa kazi (house girl)
Sasa kama mama anatoka Kwenda kufanya kazi na kuacha jukumu lake la msingi kabisa la kulea Watoto afanye House girl; kwa nini sheria isitamke; kuwa kwa wale wanawake wenye kipato (waajiriwa/wafanyabiashara); kipato chao atashirikiana na baba kuendesha familia? Dunia imebadilika sana; wapo wanawake wengi tu wenye vipato vikubwa kuliko wanaume zao....iweje sheria yetu iwatenge kuchangia maendeleo ya familia?

2. Kiwanja cha nyumba cha Baba/Mama
Kuna watu wana oana mmoja wao akiwa na kiwanja
Kulingana na mabadiliko ya Dunia, nafikiri ipo haja ya kuweka sheria vizuri kuwa; kama watu wataoana (ndoa) na kuridhiana kwa pamoja kujenga kwenye kiwanja cha mmojawapo; basi kile kiwanja walicho amua kujenga sio cha mmoja wao tena, bali ni sehemu ya nyumba (familia). Ina maana, huko baadae ikitokea kuna haja ya kugawana; Nyumba itahesabiwa ni Pamoja na kiwanja chake na hakuta kuwa na mmoja wao kudai kuwa alikuwa na kiwanja kabla ya kuoana....

Nasema hivyo kwani mambo yamedadilika; kuna mamluki wanaweza kutumia hiyo gape ya Sheria yetu kulazimisha wajenge kwenye kiwanja chake akijua huko mbeleni atadai chukua nyumba uniachie kiwanja changu, huku akilindwa na sheria.

Nawasilisha...

unahoja
usikilizwe!
 
Kukisha kuwa na upendo wa kweli hizo sheria hazina nafasi , tatizo lipo kwenye mahusiano ya ujambazi na kitapeli
Upendo wa kweli hauwezi ku last long kwa sababu mwanamke ni kiumbe emotional (muda wowote anaweza kubadilisha hisia zake dhidi yako)
 
Suala la usawa wa jinsia taratibu linaanza kuleta mzozo kwenye jamii yetu. Kuanzia mwanzo tunaanza kueneza hii sera kuna kitu cha muhimu kilisahaulika, ambacho ni "haki sawa inaenda sambamba na wajibu sawa".

Wanawake kwa miongozo kadhaa walipendezwa na kufurahia faida za haki sawa pamoja na wao kupewa kipaumbele chini ya kampeni za "mwanamke akiwezeshwa anaweza" bila kujumuishwa kwenye majukumu.

Sasa tupo kwenye mkwamo, kila siku linaibuka kundi kubwa la wanaume ambao wanashindwa kubeba hayo majukumu kwa sababu advantage ya kupewa nafasi nyingi waliyokua nayo kipindi cha patriarchy imeondolewa.

Upande wa mwanamke nae pamoja na kupewa fursa sawa na mwanaume bado anataka aendelee kupata ile privilege ya provision kutoka kwa huyo huyo mwanaume kama ilivyokuaga nyakati za patriarch.

Usawa wa kijinsia sio kitu kibaya lakini lazima tukubaliane suala moja. Kama tumeamua kuweka usawa basi na wajibu uwe sawa ikiwemo kufumua hiyo sheria ya ndoa, na kama tukiamua kuipa jinsia moja kipaumbele basi na ibebeshwe wajibu mkubwa zaidi. Wanawake watakubaliana na hilo? Sina uhakika.
 
Back
Top Bottom