Tuwaandae mabinti zetu kujenga familia na sio kuwa omba-omba

Tuwaandae mabinti zetu kujenga familia na sio kuwa omba-omba

Shytown

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2025
Posts
736
Reaction score
1,311
Ile dhana iliyojengeka ya kuwa andaa watoto wa kike kuwa omba omba imetuharibia kabisa kizazi cha sasa na kuongoza idadi ya singo mother na kupelekea kuwa na kizazi kisicho jua umuhimu wa baba;

1. Tunalea watoto wa kike tukiwaaminisha kuwa baba ndiye anatakiwa aendeshe familia kwa kila kitu
2. Tuna lea watoto wa kike tukiwaaminisha kila kitu kizuri anatakiwa aombe/anunuliwe na mwanamme
3. Tunawalea watoto wa kike tukiwaamini Ada za watoto, kujenga nk ni kazi ya mwanaume
4. Tunawalea watoto wa kike tukiwaaminisha kuwa Kipato chao ni chao pengine na familia zao (waliko toka)
5. Tunawalea watoto wa kike wakiamini akishakuwa na kipato kizuri sasa ni wakati wa kuishi kwa uhuru/kuwa singo kwa kutokubali tena maelekezo yoyote ya mumewe (kudai usawa bila kujali majukumu ya kawaida ya mama)
6. Tunawalea watoto wa kike huku wakiamini hata akifeli shuleni sio tatizo kwani ataolewa
7. Wanawake wakishakuwa na kipato wanaona kulea mtoto/watoto peke yao (singo mother) sio tatizo na hivyo ndoa nyingi za wanawake wenye kipato kuvunjika na hii imepekea kuwa na kizazi cha watoto wasiojua umuhimu wa baba ambapo ni hatari sana kwa siku zijazo.
8. Tunawalea watoto wa kike wakifikiri kile wanaochona kwenye tamthilia zawazungu ndiyo maisha BILA kujua wale ni waigizaji wapo kazini (zingatia neno WAIGIZAJI)


Hiyo mentality inatakiwa ibadilike kabisa kwa wazazi na kwa watoto wa kike kwani haya malezi/mafundisho yametuharibia kabisa watoto wa kike na hata wale walisoma na kuwa na kazi nzuri....
Najua wanawake hutumia maandiko kuhalalisha wao kuomba wanaume ILA Biblia ilichomaanisha ni tofauti...
1. Wanawake walio andikwa kwenye Biblia ambapo watatunzwa na kupewa kila kitu na wanaume ni wale ambao Mumewe anauwezo na wao wanakaa nyumbani, kuzaa na kulea familia
2. ILA Wanawake wanaotoka kwenda kwenye Biashara au makazini na kuacha watoto wanalelewa na house girl hao wanatakiwa kushiriki katika maendeleo ya familia iwemo kujenga nk kwa asilimia 100%

Hii tabia ya wanawake kuwa omba omba imepelekea mabiti wetu wengi, kuangukia wanaume ambao sio ndoto zao kwani wamekuwa wakifikiri yule mwanamme anaye ombwa na kutoa ndiye mzuri kumbe wanaume wa namna hiyo baadhi hutumia huo mtego...wameshajua udhaifu wa ombaomba ni kumpatia anachotaka kwa wakati huo...

TUBADILIKE NA KUWA ANDAA WASICHANA KUSOMA, KUFANYA KAZI MBALI MBALI NA KUSHIRIKI MOJA KWA MOJA KWENYE MAENDELEO YA FAMILIA ZAO.....
 
Ile dhana iliyojengeka ya kuwa andaa watoto wa kike kuwa omba omba imetuharibia kabisa kizazi cha sasa na kuongoze idadi ya singo mother na kupelekea kubwa na kizazi kisicho jua umuhimu wa baba;
Mtoa mada naomba huo mfano wa kuandaa watoto wa kike kuwa maomba omba sijaelewa kabisa ni mzazi anakaa na mwanae kumwambia mama kuanzia sasa wewe ni ombaomba au inakaaje hii..
 
Tia helaaaa
Tia helaaaa
Tia helaaaa
Tia helaaaa

Ni kweli hao mabinti mnawalea vibaya, lakini nilichokuja kugundua hao mabinti wakifikia umri wa miaka 30+ wanaanza kuwa na sifa za kuwa mashangazi.

Hapo tena hatokua akiomba pesa au sijui ulimaanisha kuomba nini.
Ila kama ni pesa hatoomba tena badala yake anakua anamba 🔥 🔥
Na kama akakutana na kijana ambaye yeye ana degree ya mikunjo basi yupo radhi yeye ndo atoe pesa kabisa ili apate mikunjo, misuguano au mikazo..

Kwahiyo naweza conclude kwa kusema hizo tabia sio za kudumu hivo tusiogope sana
 
Nafikiri kinachohitajika ni kujenga mtazamo kwamba wanawake na wanategemeana na si kuzidiana. Kila mmoja anamhitaji mwenzake.

Itabidi tumenye maganda yote ya tamaduni za kizamani. Mfano bibilia na quran zimepitwa sana na wakati vinataka mwanaume apendelewe kwa kila kitu.

Sasa tunaachaje hizi tamaduni? Ni ngumu sana. Kuna mkanganyiko mkubwa hapa.
 
Back
Top Bottom