Sheria ya mita 200 inatekelezeka kweli?

Sheria ya mita 200 inatekelezeka kweli?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,153
Reaction score
162,568
Hivi kiuhalisia sheria hii inatekelezeka?

Ni kituo gani cha kura kiko isolated kiasi hicho?

Kwa mazingira ya nchi yetu na jinsi vituo vingi vya kura vilivyokaa,utamshawishi vipi Jaji(kumbuka kesi teyari iko mahakani) akuelewe unapotaka kusimamia utekelezaji wa sheria hii?

Hapa Usa-River mkoani Arusha kwa mfano,kuna kituo kiko jirani na soko na cha zaidi ni kuwa,hiyo siku ya kupiga kura ambayo ni Jumapili,siku hiyo ni siku ya soko kwa soko la hapa Usa-River.Sasa katika mazingira haya,sheria hii utaitekelezaje?

Kwa mtazamo wangu,hii sheria is a dead letter by itself and will always be so.
 
Mkikaa mita 200 na CCM nao watakaa mita 800 ili kuwe na security zone kati kati ya mita 600?

Ndugu zangu mna watoto wadogo na wake wabichi, na wazee wanaowategemea. Fikiri kabla ya kuamua, piga kura yako rudi home uwatendee haki watoto wako na jamii yako wakuite baba anayewatimizia majukumu kwa mjibu.
 
Hao ni vibaka tu acha wajifanye ngangali wapigwe risasi . hawana family na maisha yamewapiga kwahiyo wanatafuta jinsi ya kufa
 
Hao ni vibaka tu acha wajifanye ngangali wapigwe risasi . hawana family na maisha yamewapiga kwahiyo wanatafuta jinsi ya kufa

maisha yamewapiga kwa sababu ya sera mbovu za CCM.

Secondary miaka 6
Diploma miaka 2
degree miaka 3
masters miaka 3
PhD miaka 9 Jumla miaka 23,mtu kasoma kwa miaka 23 kwa kiingereza ila kiingereza chake akikuazimisha hauchomoki kwenye interview zinazojielewa. Utasema hicho chama kina sera nzuri za kukuza elimu?
 
Ukitazama hili jambo kwa makini utaona kwamba limekaa kisiasa zaidi, huu ni ubishani wa kivyama na sio serikali! Kama kuna mtu kalitamka hili kama serikali sio sahihi! Huyu katoa kauli ya Chama chake, Serikali lazima iheshimu sheria za nchi.

Kukaa mitaa 200 kutoka kituo cha kupigia kura ni suala la kisheria,na ni sahihi kufanya hivyo! Mtu kwenda nyumbani ni hiari yake ila sheria haimzuii kukaka mita 200. Atakayemfuata au kumfukuza aliyekaa mitaa 200 kutoka kituoni anataka kuchafua amani ya nchi.


Mbona CCM wanataka kulazimisha watu waende kukaa majumbani wanataka nini? Mbona ni wao tu? Kura zao za maoni waliibiana sana kura na wengine walikamatwa na kura(Gaudensia Kabaka ni shahidi), wengine waliyakataa matokeo ya kura za maoni wakilalamika sana! Leo iwe CCM na upinzani? Tuacheni utani! Tuipende amani,tuipende nchi yetu!
 
Hao wanaotaka kulinda kura wamejiandaa kitumia silaha gani kwa kazi hiyo?
Je, wakihisi jambo fulani haliko sawa watachukua hatua gani?
Nani atawaongoza katika hatua wanayochukua?
 
Hairuhusiwi mikusanyiko au ishara yoyote ya Kisiasa we leta Ubishi likikukuta ni wewe na Familia yako sio Vyama, yule dogo wa ishu ya Mwamunyange anaepanda na kushuka hivi sasa ni bi Mkubwa wake akina Malya wamejidai eti wakiisimamia ile kesi itachukuliwa kisiasa. Vijana muwe tayRi kwa hilo
 
Hao wanaotaka kulinda kura wamejiandaa kitumia silaha gani kwa kazi hiyo?
Je, wakihisi jambo fulani haliko sawa watachukua hatua gani?
Nani atawaongoza katika hatua wanayochukua?

silaha yetu ni macho na mdomo, na kama mambo ya wizi tumeyaona, ndo watakapojua kwamba ccm hatuitaki
 
Salary Slip,

..kwa hiyo kisheria ukawa wako sahihi.

..tatizo liko kwenye utekelezaji ambapo vituo viko maeneo ambayo yana msongamano.

..kama ni hivyo basi suala hilo inabidi lipelekwe kwenye chombo cha kutunga sheria ambacho ni BUNGE.

..BUNGE ndilo lenye mamlaka ya kubadili sheria hiyo.

..kwa upande mwingine nadhani BUSARA ingetumika kushughulikia suala hili, badala ya kutoa VITISHO.

NB.

..kwa mtizamo wangu ukawa wamekosea kupeleka suala hili mahakamani. ccm wako desperate sasa hivi na usijeshangaa akapatikana jaji kada wa ccm akaamua shauri hili ndivyo-sivyo.
 
Kwann ccm tu wakatae na co wengn watu tuna ushahid wa mabox yalioingzwa arumeru kpnd Joshua anagombea lazm tulnd kura na lazma tushnde
 
Mnahamasishana ujinga. Mimi najua Edo alisema sisi tupige kura turudi nyumbani, ulinzi ni juu yake.
 
Hao wanaotaka kulinda kura wamejiandaa kitumia silaha gani kwa kazi hiyo?
Je, wakihisi jambo fulani haliko sawa watachukua hatua gani?
Nani atawaongoza katika hatua wanayochukua?
Maswali yako ni ya msingi sana. Yanahitaji majibu makini kupata picha kamili.
 
Mi nashauri mahakama ingetoa tafsiri juu ya hi sheria ili kuondoa mkanganyiko baina ya wapga kura,pia nashangaa xana kuona ccm wamekazana xana kukataza watu wasisimame umbari wa mita 200
 
Hairuhusiwi mikusanyiko au ishara yoyote ya Kisiasa we leta Ubishi likikukuta ni wewe na Familia yako sio Vyama, yule dogo wa ishu ya Mwamunyange anaepanda na kushuka hivi sasa ni bi Mkubwa wake akina Malya wamejidai eti wakiisimamia ile kesi itachukuliwa kisiasa. Vijana muwe tayRi kwa hilo
sawa tuko tayari.tutasubiri matokeo tukiwa mita 200 kwa mujibu wa sheria na kama ilivyokua katika chaguzi zilizopita.swala la eti piga kura alafu kalale sijaona logic yake bado.
 
Ni suala la busara tu litumike. Nafikiria vijana waliopiga viloba wakkakizunguka kituo cha kupigia kura na matokeo yakatangazwa mgombea wao akashindwa sijui nini kitaendelea katika kituo kile. Pia watu wanaweza kwenda kufanya Fujo makusudi pale watakapoona mgombea wao ameshindwa uchaguzi ilimradi tu kutibua. Kwa nn tusiwaamini mawakala wetu tuliowapa dhamana ya kuangalia kura zetu.
 
Back
Top Bottom