Sheria inasemaje kuhusu Wabunge walioaga Dunia?

Sheria inasemaje kuhusu Wabunge walioaga Dunia?

Kuntakint

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
1,767
Reaction score
1,526
Zimepita siku karibu mwezi sijamsikia spika wa bunge letu kusema lolote kuhusu nafasi za wabunge wetu waliyochukuliwa kwa mapenzi ya mungu. Na sijasikia hata sisi wananchi ambao tunalipa kodi na kuwalipa wabunge kusikia chochote kuzungumzia kuhusu nafasi zilizo wazi kwa waliochukuliwa na muumba.

Kwani sheria inasemaje kuhusu mbunge anapofariki mbona hakujaitishwa uchaguzi wa kujaza nafasi zao??. Halafu inakuwaje mbunge ambaye ameingia bungeni kwa tiketi ya chama kuendelea kuwa bungeni??wakati chama kilichomteua imemfuta uanachanma wake?

Inamaana kwasasa kuwa mbunge wa Tanzania spika ndie anayesema kuwa wewe ndiye mbunge, bila kuwa na chama cha siasa?.

Watanzania wenzangu ebu tuamke tuache kufuatilia umbeya na ushabiki usiyofaa huku pesa zetu zikiliwa na baadhi ya watu. Tunatakiwa kusimama imara na kujua pesa zetu zinatumikaje.

Usilalamike kuwa sukari inapanda wakati pesa ambayo ingepunguza bei ya sukari unaichia analipwa mbunge, ambaye hakustahili kuwa bungeni. WATANZANIA AMKENI NA KUJUA HAKI ZETU.

Spika wa bunge anaendesha bunge vibaya inabidi tumwondoe kwasababu tunaoumia ni sisi wananchi. Tunadharau vitu bila kufuatilia lkn ndiyo vitu zinazosababisha maisha yetu kuwa magumu.

Inakuwaje spika ambaye tumemchagua kuwa mbunge na kuchaguliwa na wabunge wenzake ambao ndio wawakilishi wetu awe na POWER kuliko sisi tuliowachagua na kumweka madarakani.

Watanzania bila kuwa pmj na kushirikiana kuwaondoa hawa viongozi walafi, tutateseka sana. Watu wanauwawa/ wanatekwa na tunawajua watekaji na wauaji tumebaki kusema tumwachie mungu. MUNGU ATAKUSAIDIAJE PASIPO WEWE KUJISAIDIA?.

Tukatae uonezi bila kujali dini, kabila wala rangi. Leo tunalaani mauaji ya Floyd aliyeuwawa huko marekani wakati hapa kwetu ndio vinara wa mauaji, kuna mauaji mabaya hapa kwetu kuliko hata ya Floyd.

Sisi watanzania tunamchinja mtanzania mwenzetu bila kujali utu wake kwasababu ya itikadi ya vyama kweli???. Unamkata mapanga mtanzania mwenzako kwa tamaa ya madaraka ambayo utayaacha hapa hapa duniani. Jiulize je hii ni akili. Wewe polisi unampiga Mtaanzania mwenzako mpaka unamuua bila sababu hivi unategemea kupokelewa huko mbinguni?.

WATANZANIA WENZANGU TUNATAKIWA TUBADILIKE KWA KUJIFUNZA KWA HAYA YANAYOENDELEA MAREKANI.

Sisi ni ndugu tusivurugwe na hawa wachache wenye tamaa ya mali.
 
Kamanda umeshaelezwa bunge la zt halihojiwi popote na maamuzi yake ni sahihi
 
Ndugu kwanza nashindwa nianzie wapi ila fanya haya yatakusaidia humu jamvini!

_ Weka uzi wako kwa aya/paragraphs, itafanya ulichoandika kivutie na pia kueleweka mapema.

_Jiepushe na utumiaji wa wingi katika nyuzi za namna hii,mfano umetumia sana wingi "tumemchagua Mbunge" hapa mbunge hachaguliwi na wote,avoid generalization , mfano nikuulize swali WEWE ULIMPIGIA KURA MB NDUGAI? KAMA NDIO JE UNADHANI WOTE ULIOSEMA TULIMPIGIA KURA WOTE NI WA JIMBO LA KWA NDUGAI?

_epuka kuleta mijadala isiyo na ushahidi, sheria zipo na ignorance of law haikulindi chochote, avoid such fallacious statement, umesema WATANZANIA "tunauana kisa madaraka" Wewe umeshaua wangapi mkuu?

_Jikite kwenye hoja moja, be specific,mfano hoja yako mwanzoni unahoji na unataka kujua sheria zinasemaje pale mbunge anapofariki, mara kati kati tena unaleta habari mara sijui za mbunge kuwa mbunge alihali ashafukuzwa uanachama ,,humo humo tena umelalamika kuhusu speaker NDUGAI yaani hueleweki


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye wabunge waliofariki, Katiba ipo wazi kuwa kuna kipindi kiti kikiwa wazi muda fulani kabla ya Bunge kuvunjwa kunakuwa hakuna uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi.
 
Unachanganya changanya tu vitu! Uandishi wako hauna paragraph hivyo unachosha kusoma. Kuhusu Wabunge waliofariki au hata kuhama vyama, kuna muda wake!

Kwa sasa hata kama Wabunge wote watakufa kwa Corona, hautaitishwa uchaguzi mwingine maana muda wa kufanya hivyo umeahapita. Na usisahau mwezi huu wa Juni Rais atalivunja hilo Bunge kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2020.

Na hayo ya Wabunge kurudishwa Bungeni kwa mgongo wa Spika ni ya kisheria hivyo yasikuumize kichwa. Kama unaona kuna mapungufu kwenye hizo sheria za nchi, wewe kama Mtanzania mwenye uchungu na nchi yako, angalia njia sahihi za kuchukua ili kukomesha madhaifu hayo kutojirudia tena siku za usoni. Tutakuunga mkono!

Umeona lakini wenzako tunavyo andika? Na wewe ubadilike sasa. Paragraph ni muhimu sana.
 
Back
Top Bottom