Sheria inaruhusu mwalimu kujitoa CWT na kujiunga na chama anachokipenda?

pambe samanini

JF-Expert Member
Oct 27, 2015
368
169
Kwa miaka kadha sasa walimu wamekuwa wakilalamika kuhusiana na chama Chao cha cwt kuwa hakiwatendei haki hasa za kuwatetea kupata stahiki zao kwa mwajli ikiwa pamoja na kupanda daraja, mazingira bora ya kufanyia kazi nk.

Hata hivyo makato yasiyo wanufaisha wanachama wao wakati na baada ya kustaafu kazi yao, pia utumiaji mbovu wa mali za chama bila kushirikishwa wanachama na pia chama kinanuka rushwa, ufisadi nk

Hata hivyo siku hizi pamekuwepo na vyama vingine vya kutetea haki zao km CHAKAMWATA, CHAWAKAMA nk ambavyo vimeleta ushawishi mkubwa wa walimu kujiunga navyo ili waweze kuondoka CWT.

Hata hivyo CWT wanasema hata kama walimu hao watajiondoa CWT bado wataendelea kukatwa ada ya uwakala na CWT kwa sababu wao ndiyo wenye mkataba kisheria na siyo vyama vingine vya walimu suala ambalo litapelekea walimu hao watakaojiondoa cwt kukatwa jumla ya 3% ikiwa CWT ada ya uwakala 2% na 1% ya vyama vingine.

Pamoja na migongano hiyo ya kimaslahi baina ya vyama hivi kuonaonekana ni suala la kisheria ambalo linahitaji marekebisho ya sheria ndo walimu hawa waweze kujitoa kwenye CWT na kujiunga na vyama vingine.

Je kwa sheria za sasa walimu hawa hawawezi kujitoa kabisa CWT na kujiunga na vyama wanavyovipenda?

Au serikali ina ubia gani wa kisheria na CWT kuwafanya wao ndo mawakala wa makato hayo yanayodaiwa na walimu kuwa haramu?

Pia, je mwajiri anaweza kumkatalia mtumishi wake mwalimu kujiunga na chama kingine kwa kuwataka CWT kuwacha wanachama hao bila ya kuwakata ada ya uwakala 2% nk

Kwa maswali haya naomba msaada huo
 
Walimu siwatishi ila muwe macho na huu uanzishwaji holela wa hivi vyama vipya vinavyodai vinapigania maslahi ya walimu. Kwanza formation yake kwa maana ya jina lenyewe inatia Shaka mf:"CHAKAMWATA", CHAWAKAMA" na vyote vimeibuka ghafla tu kama uyoga. Kwakuwa % kubwa ya walimu sio wadadisi wa mambo wataingia kichwakichwa kwenye mkumbo wa kukiacha chama chao cha walimu na kukimbilia kwenye hivyo vipya ambavyo havijajipambanua malengo yake hasa ya kuanziashwa kwake.rai yangu, walimu muwe macho hasa kipindi hiki kwani vitakuja kila aina ya majina ya vyama vikijinasibu kupigania masilahi yenu, kwakuwa wengi wenu mpo desperate mtasumbuliwa sn, kama mna kumbukumbu nzuri, hata kipindi kile cha luddism & chartism wkt imepamba moto, ili kudhoofisha muungano ule vilianzishwa vyama uchwara vyenye malengo kama ya hivyo vya awali na mwishowe harakati zile zilizimwa. So kuweni makini na hilo. Walimu. Mungu ibariki Tanzania na Walimu wake pia.
 
Kuna siku kwa mfano CWTZx kitaitisha mgomo wa walimao nchi nzima halafu kitaibuka CHAMAWTAKULAWAPI kitaibuka kwenye vyombo vyote vya habari na kupewa nafasi kubwa kwenye kile chombo kikuu cha umma na kukanusha vikali luhusu mgomo huo huku wakisema hawaitambui na hawakishirikishwa na wananchi waipuuze.
Matokeo yake ni divide and rule itakua imeshinda.
 
Back
Top Bottom