rweyy
JF-Expert Member
- Aug 5, 2011
- 229
- 146
habari wana jf kuna kesi imelwetwa hapa kwangu niweze kutoa ushauli ila kabla ya sijatoa ushauri nimeona nipokee ushauri kutoka kwenu wana jf kuna kaka mmoja ni jilani yetu ameoa na ana mtoto mmoja kuna mdogo wake wa kike katoka kijijini kaja kwake ili amtafutie shule asomee huku mjini kamaliza kidato cha nne ila hapa nyumbani kuna kaka yake na mkewe huwa anakuja siku za weekend huyo shemejie yuko chuo ila kila weekend lazima aje pale nyumbani sasa huyu kaka alipigiwa simu na mdogo wao wa mwisho aliyeko kijijini kuwa huyu dada anaeishi nae hapo kwake ana uhusiano wa mapenzi na shemejie baada ya uchungunzi wa huakika kakuta ni kweli na baada ya kumuuliza dada kakubali ni kweli sasa afanyeje? mkewe akiulizwa wafanyeje ni kulia tu kwamba kaka kaniabisha. kumuzuia shemeji asije pale anashindwa maana shemeji na mkewe kwa sasa hawana wazazi.huyo shemeji anamuona dada yake kama baba na mama kumurudisha dada kijijini hatakwoswa elimu. akiendelea kukaa hapa uhusiano utaendelea .ninaomba ushauri kipi kifanyike