Shemeji anataka nimkopeshe

Shemeji anataka nimkopeshe

pilau

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
1,595
Reaction score
450
Jamani hii ni nini? Mke wa jamaa mmoja ambaye sina ukaribu naye na wala sio jirani yangu kivileeee....lakini namfahamu mumewe ambaye anauwezo wa kimaisha .... gari mbili za kutembele ajira serikalini.. mkewe amemfungulia mradi wa kuku wa nyama na mayai..kifupi hela ya kubalilisha mboga haipigi chenga... lakini ananiambia shemeji nikopeshe 100,000/= lakini chonde chonde....mume wangu asijue.. iwe siri yetu... jamani ushauri...
 
Mkopeshe!tena usifikiri mambo mengine! Cha muhimu ukaribu naye ndo hautakiwi! Kwani kukulipa inaweza kuwa inshu!
 
kwa nini anakuita shemeji na sio kaka? kumbuka umesema hamko karibu na mme wake kivile!!!1
 
Jamani hii ni nini? Mke wa jamaa mmoja ambaye sina ukaribu naye na wala sio jirani yangu kivileeee....lakini namfahamu mumewe ambaye anauwezo wa kimaisha .... gari mbili za kutembele ajira serikalini.. mkewe amemfungulia mradi wa kuku wa nyama na mayai..kifupi hela ya kubalilisha mboga haipigi chenga... lakini ananiambia shemeji nikopeshe 100,000/= lakini chonde chonde....mume wangu asijue.. iwe siri yetu... jamani ushauri...

Mwambie amkope mke wako(kama una mke), halafu wewe unampa huyo mkeo hela kwa ujanja wa kama za ziada vile kumbe kuna mpango unatengeneza, yaani usimwambie mkeo

Ama, kama huna mke
Mwambie ukweli unavyojisikia kuhusu kumkopesha, bila shaka itakuwa ni kwa manufaa ya ndoa yake
(lend what you can afford to loose usije baade kuleta tena kilio)

NB;
life is not so rigid that way, tusaidiane tu kwa nia njema ya kukabiliana na changamoto za maisha, nothing else!!
Ahsante!!
 
Hela inaenda hiyo shemeji....
kwanini hataki mme ajue???
 
Anaanza huyo na ukimuachia akuzowee basi..amkope mumewe na hayo mambo yakuambiana usimwambie mume wake ndio mbaya.........
 
ha ha ha imekula kwako na siku ukimdai akikukana na ukizingatia mmewe halijui patakua hapatoshi hapo
 
Jamani hii ni nini? Mke wa jamaa mmoja ambaye sina ukaribu naye na wala sio jirani yangu kivileeee....lakini namfahamu mumewe ambaye anauwezo wa kimaisha .... gari mbili za kutembele ajira serikalini.. mkewe amemfungulia mradi wa kuku wa nyama na mayai..kifupi hela ya kubalilisha mboga haipigi chenga... lakini ananiambia shemeji nikopeshe 100,000/= lakini chonde chonde....mume wangu asijue.. iwe siri yetu... jamani ushauri...

mnako elekea atakupa mzigo napo atasema chonde chonde iwe siri
 
Si kila anayekuomba msaada anataka mahusiano kwa nini mnakuwa na positive answers?Inawezekana huyo shemeji yako kweli ana shida na hiyo pesa pengine ana tatizo labda kwa upande wa familia yake na mumewe hayupo katika nafasi ya kumsaidia though kuna magari na anafanya kazi serikalini pamoja na hayo yote siku hazifanani,Kama upo katika nafasi ya kumsaidia tenda wema uende zako usigeuke nyuma na kama kweli una nia ya kumsaidia kwa dhati bile kuexpect return kwanini umshirikishe mumewe,wewe mpe km vigezo na masharti aliyokupa then angalia ustaarabu wako.
 
Si kila anayekuomba msaada anataka mahusiano kwa nini mnakuwa na positive answers?Inawezekana huyo shemeji yako kweli ana shida na hiyo pesa pengine ana tatizo labda kwa upande wa familia yake na mumewe hayupo katika nafasi ya kumsaidia though kuna magari na anafanya kazi serikalini pamoja na hayo yote siku hazifanani,Kama upo katika nafasi ya kumsaidia tenda wema uende zako usigeuke nyuma na kama kweli una nia ya kumsaidia kwa dhati bile kuexpect return kwanini umshirikishe mumewe,wewe mpe km vigezo na masharti aliyokupa then angalia ustaarabu wako.
Asipolipwa jee? Vitu vingine si vya kufanyia majaribio..! Eti unywe sumu halafu uangalia kama utaharisha, utakufa badala ya kuharisha.! Hilo jimama ni la kupigwa chini tu, mambo ya siri na mke wa mtu ya nini?
 
sometimes sisi viumbe huwa tunafikiria visivyo! huenda mama wa watu ana shida iliyomfika shingoni na haoni mtu mwingine wa kumkopa ila huyo shemeji wa kivileee! tuondokane na mentality za kihivyooo!
 
Tuseme za ukweli huyo dada kweli anataka laki moja tuuuuuuu! kama sielewi hivi, aache kuzingua kwanza tumeshachoka kugandiana aende zake saccoss.
 
sometimes sisi viumbe huwa tunafikiria visivyo! huenda mama wa watu ana shida iliyomfika shingoni na haoni mtu mwingine wa kumkopa ila huyo shemeji wa kivileee! tuondokane na mentality za kihivyooo!

hakuna jambo ambalo ni jema utafanya na mke wa mtu alafu eti tufanye iwe siti mme wangu asijue,jamani aya mambo si yakufanyia majaribio ,mke wa mtu si mchezo
 
hakuna jambo ambalo ni jema utafanya na mke wa mtu alafu eti tufanye iwe siti mme wangu asijue,jamani aya mambo si yakufanyia majaribio ,mke wa mtu si mchezo

ni kweli uko right ila mimi nasemea kwa habari ya kutanguliza mentality kwamba labda mke wa mtu anamtega jamaa. ni kweli kuna tatizo...mathalani huyo mke wa mtu asiporejesha pesa na kuanza vituko vingine vya kikubwa! hapo jamaa awe tayari kusamehe hiyo hela endapo asipolipwa. hatari nyingine...itakuwaje endapo mwenye mke akijua kuwa jamaa kamkopesha mkewe hela!
 
Alichosema chenye ujumbe hapo ni 'nataka iwe siri yetu'...
 
Thubutu, yalinikuta hayo mimi, njoo nikupe lecture za bure. Alinifuata mke wa mtu, jamaa mfanya biashara, huwa anasafiri safiri. Mke kaja kunikopa 50,000 nikampa bila hiyana, akaniambia mumewe asijue. baadaye muda wa kulipa ulipofika akawa anasema hajapata bado. Akaanza kuchat na mimi mwishowe akaanza kuniambia kuwa amevutiwa na mimi. Kilichofuata.......... usiniulize.
 
Back
Top Bottom