Shem utatapita pale petrol station..

Mwaya; big up!
Wewe ndio mwanaume, tena mwenye msimamo!
Achana na wanaokuzonga. Mi nakukubali mpaka mwisho.
Lina Heri tumbo lililokuzaa, na ana bahati mama wa watoto wako.

Salute!
 
Hapa wala tuctafune maneno,huyu jiran anatia mashaka maana huo msisizo aliounyesha kumfatilia jamaa tangu anatoka mpaka anarudi co bure alikua na lake jambo!hongera zako kaka kwa kumpotezea,kwann acmwite masai amsaidie kutia hiyo luku ebo!
 
Marekebisho mwishoni

Nikazima TV fasta nikaingia
chumbani nikampigia wife simu
nikamwambia nampenda na
kumkiss good night, nikaenda bafuni!
 
Dirty mind tu, yaani wewe ulishawaza unaenda kutongozwa, huyo jirani atakudharau sana kwa kumuhisi yeye ni Mal*ya
kama una nia kweli ya kuikimbia zinaa ungeenda na kuona anachotaka kufanya na hapohapo ungemkanya kwa maneo makali kabisa na sio kukimbia na kujidharirisha
nampongeza mtoa mada,hebu we fikiri amerudi saa mbili na nusu nadhani saa mbili hiyohiyo alimpa masai luku aipeleke...sa4 huyo mama ndo anapiga cm akaingiziwe luku jamani huoni kama huyo mmama alikua anaki2?hivi kweli unamvizia jirani atokapo na aingiapo loo!
 
Ungechukua jopo la majirani kadhaa tu muende kumsaidia jirani yenu kuingiza LUKU na kudumisha ujirani bila hofu ya kuzua tafrani.
 
Mkuu kwa jinsi ilivyo mwisho wa siku lazima utamtafuna Shem.
 
ngoja nimalizie....jamaa alivyoenda akamkuta shem yupo anamsubiri alafu kapiga kitu cha night dress tu....dah shem akamwambia jamaa unajua nilitaka kulala nikaogopa umeme utaisha usiku nikaamua nikuombe uje kunisaidia kuingiza....shem akamwambia mita ipo chumbani.....kufika chumbani shem akasema ngoja amletee stuli maana mita ipo juu jamaa afikii, ikabidi shem ashike stuli ili jamaa asianguke ila shem akaanzia kumkumbatia miguuni mpaka kiuononi alafu uso upo kwenye zakaria mara kanga ya shem ikadondoka....kilichofuata....mnakijua...
 
Ilikua jumamosi asubui natoa gari getini, mara naskia mke wa jirai yangu ananiuliza Shemeji utapita pale Petrol satation?
Kwa sababu nilikua narudi njuma nilikua sijamuona ila yeye alikua kasimama pembeni ya geti kwa nje.
Nikajibu-Oooh za asubui shem...Hapana shemeji nilishaweka jana ila kwani kuna kitu unaitaji... akajibu Ndio shem naitaji Luku.
Nikamwambia haina shida ila mimi nitachelewa kurudi.. akanijibu hamna tatizo bado iko kidogo.
Kwenye mida ya saa mbili na nusu napiga honi ili geti lifunguliwe....mara naona simu inaita, napokea ni shem ananiambia umenipita hapa nyuma..nikamwabia ok ngoja nimpe Masai akuletee luku yako.
Ilipofika kwenye saa nne na nusu ivi bado niko naangalia TV , msg inaingia... ''shem naomba uje uniingizie, mimi nimeshindwa, na baba...... amewapeleka watoto shule Arusha niko mwenyewe, samahani kama nakusumbua''

Nikazima TV fasta nikaingia chumbani nikampigia wife simu nikamwambia nampenda na kumkiss good night,, mke wangu yuko Mbeya alienda kwenye msiba wa bibi yake. Nikazima simu nikasali , nikalala.


Hongera mkuu, na ulikuwa una kila sababu ya kusali kumshukuru Mungu kwa kukupa ujasiri wa kukataa kwenda kuingiza LUKU, ungeingiza na mengine! Loh!
 
Ningekuona shujaa kama ungeenda, halafu akikwambia mambo mengine tofauti na LUKU umpige mkwara na kumwambia kuwa awe mwaminifu katika ndoa yake. Hapo ungekuwa umetoa fundisho, sasa kwa kuwa hukutoa fundisho lolote, labda kweli tatizo lilkuwa ni LUKU au kama sio LUKU alimpigia jirani mwingine na kupata msaada husika.
 
Ilikua jumamosi asubui natoa gari getini, mara naskia mke wa jirai yangu ananiuliza Shemeji utapita pale Petrol satation?
Kwa sababu nilikua narudi njuma nilikua sijamuona ila yeye alikua kasimama pembeni ya geti kwa nje.
Nikajibu-Oooh za asubui shem...Hapana shemeji nilishaweka jana ila kwani kuna kitu unaitaji... akajibu Ndio shem naitaji Luku.
Nikamwambia haina shida ila mimi nitachelewa kurudi.. akanijibu hamna tatizo bado iko kidogo.
Kwenye mida ya saa mbili na nusu napiga honi ili geti lifunguliwe....mara naona simu inaita, napokea ni shem ananiambia umenipita hapa nyuma..nikamwabia ok ngoja nimpe Masai akuletee luku yako.
Ilipofika kwenye saa nne na nusu ivi bado niko naangalia TV , msg inaingia... ''shem naomba uje uniingizie, mimi nimeshindwa, na baba...... amewapeleka watoto shule Arusha niko mwenyewe, samahani kama nakusumbua''

Nikazima TV fasta nikaingia chumbani nikampigia wife simu nikamwambia nampenda na kumkiss good night,, mke wangu yuko Mbeya alienda kwenye msiba wa bibi yake. Nikazima simu nikasali , nikalala.

Safi sana kAKA, huyo mmama anataka kukuingiza majaribuni hasa baada ya kugundua mkeo kasafiri.
Hatua uliyochukua ni ya kishujaa na inastahili kuigwa na kila mwanaume anayejaribiwa, hongera mkuru.
 
Hapa wala tuctafune maneno,huyu jiran anatia mashaka maana huo msisizo aliounyesha kumfatilia jamaa tangu anatoka mpaka anarudi co bure alikua na lake jambo!hongera zako kaka kwa kumpotezea,kwann acmwite masai amsaidie kutia hiyo luku ebo!
Hasante sana, ingawa ilikua ni ngumu mno..
 
Safi sana kAKA, huyo mmama anataka kukuingiza majaribuni hasa baada ya kugundua mkeo kasafiri.
Hatua uliyochukua ni ya kishujaa na inastahili kuigwa na kila mwanaume anayejaribiwa, hongera mkuru.

Hasante habi.
 
Ningekuona shujaa kama ungeenda, halafu akikwambia mambo mengine tofauti na LUKU umpige mkwara na kumwambia kuwa awe mwaminifu katika ndoa yake. Hapo ungekuwa umetoa fundisho, sasa kwa kuwa hukutoa fundisho lolote, labda kweli tatizo lilkuwa ni LUKU au kama sio LUKU alimpigia jirani mwingine na kupata msaada husika.

Kiongozi unajua ukishakua mtu mzima unakua na uzoefu wa mambo mengi sana... huyu mama hakua na lolote, hapa street kuna vijana wengi tu walinzi na ma house boy ambao angeweza kuwatuma hiyo luku na wakamwekea... kitendo cha mimi kumkubalia tu kununua luku ilikua ni heshima sana.... Mambo kama hayo huitaji kujaribu maana najijua ni rijali siwezi kwenda nikamkuta na chupi alafu nimwache, hivyo ni bora sikwenda kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom