Boxing Day 2021: Kumbe Mwanamke akishalewa, usaliti ni nje nje!

DeepPond

JF-Expert Member
Nov 18, 2017
40,460
99,104
Ya Christmas: MWANAMKE Akilewa NI HATARI SANA KWENYE MAHUSIANO.

Heri ya klisi-masi mabibi na mabwana Klisimasi ilikua na hekaheka nyingi Sana hasa hasa sisi wapenzi wa kuhama kiwanja hiki na kuhamia kiwanja kile. Jana ilkua sikU ya boxing day, Kama kawaida kujirusha hapa na pale. Nilikua kiwanja flan cha kujirusha kwelikweli.

Pamegawanyika sehem ya watu wazima Ni uwanja wa wazi miti miti mingi na (live bendi zinapigwa haswa) na sehem nyingine ni ya vijana ukumbini na (disco kubwa linapigwa).

Binafsi Kama mtu mzima nilikaa na sehem ya watu wazima wenzangu na vijana wangu wa kazini. Vinywaji vinatembea, nyama zinachomwa kwelikweli. Ni mwendo wa bandika bandua.

Gafla namuona shemej yangu mmoja Ni Bibi afya pale manispaa bwana ake kaenda kwao Moshi kula sikukuu Yuko kwenye Kati ya 25-29 hivi. {Hawajaoana bado}. Yuko na rafk zake wawili warembo wakaja kutusalimia, Basi tukawaambia wajoin kampani tuendeleze burudani.

Ulabu umeenda mpk KWENYE saa 3 u na Nusu hivi, wale shoga zake wakabeba vinywaji wakarudi zao disco kuendelea kuburudika pamoja wale vijana wangu. (nahisi damu zilishaendana tayar).

Shemeji yangu huyu,

Yeye ni muongeaji sana, akabaki pale anaendelea na sisi kutia stori za hapa na pale. Wadau wakaongezeka KWENYE kilinge tukafikia kama wadau 8 hivi

Kwenye saa 6 hivi kilinge kikaanza kupungua mmoja baada ya mwingine. Tukabaki Kama wanne, jamaa wawili wengine siwafaham ila tulikutana pale pale kwenye kilaji.

Kwenye saa 7 hivi, Ukimya ukaanza kutawala. Nikaanza kuona na shemeji maneno yanatoka kwa kigugumizi akawa Anaongea uku kama anasinzia kdg.

Nikaona sio busara, usiku ushakua mkubwa huu bora niwastue vijana twenzetu. Kufika kule nmetafuta disco zima sijawaona wao Wala wale Mabinti wawili nikajiongeza, nikawa mpole. Nikarudi kwenye meza yangu, nikakuta sio shemej Wala wale vijana wote wameshaondoka.

Basi nikaelekea parking niondoke zangu, Nikiwa najaribu kuwapigia vijana kuwafahamisha kua naondoka zangu gafla nikaona mzozo kwenye taxi barabarani.

Shemej anagombewa na wale vijana wawili aingie kwenye taxi mmojawapo, taxi zilikua mbili. Nikasogea pale. Kufika shemej akakimbilia kwangu viatu kashika mkononi akaniangukia, anasema "Shemejiii Hawa wakaka wanang'ang'ania vitu vyangu"

Nikawaskiliza ule mzozo nikaona jamaa mmoja anang'ang'ania mkoba wake Hataki kuuachia anamlazimisha apande mle. Huyu jamaa mwingine nikaona kashika mtandio wake afu Yuko kimya. Nikajiongeza kua Hawa jamaa wanataka wakamle kimasihara maana wanaona uyu keshalewa tayar.

Ikabidi kunibidi kutumia ubabe. Nikamvuta kuelekea nilikopaki, gafla nikaona jamaa aloshika mkoba anamvuta. Nikaona uyu jamaa asiniletee upuuzi. Nikamuachia mwanamke, afu nikarud kwenye gari nikafungua buti nikachukua rungu langu la mimasai na sime.

Nikavua shati nikabaki na vesti TU, tayar kwa Shari kwa maana Hawa vijana nikiwaangalia naona kabisa nawamudu wote kabisa,hawana mbavu za kunisumbua mimi kwa lolote.

Nikamrudia jamaa nikakuta keshamburuza mwanamke na kamuingiza kwenye taxi, Yuko nje kabaki na mzozo na yule aloshika mtandio.

Haraka sana nikambamiza rungu ya bega la kushoto likampeleka chini, akataka kuinuka, nikambamiza ubapa wa sime begani pale pale nilikopiga rungu Mara ya kwanza. Nikaona anataka kuinuka Tena. Nkamuongeza ubapa mwingine wa mgongoni nikamwabia kaa kimya na ukiinuka hapo nakucharanga vipande vipande sasa hivi SITAKI UPUMBAVU. Nikaona Jamaa kawa mpole akatulia anaugulia maumivu.

Nikamwambia Yule aloshika mtandio, "Hebu nipe iyo HARAKA Sana" akanipa mtandio. Nikaenda kwenye taxi kufungua nimtoe mdada, milango imelokiwa. Nikamwambia taxidriver "AISEE fungua HARAKA kabla sijasambaratisha hiki kioo chako na hili rungu"

Akabonyeza rimoti mlango ukafunguka. Nikafungua kumtoa binti. Bahati nzuri Kuna jamaa mmoja mstaarabu Sana alkuepo pale akiamulia ugomvi ule tangu mwanzo akanisaidia kumbeba mdada mpk kwny gari. Nikamwambia uyo jamaa, "AISEE uyu Ni shemej yangu kabisa, nisaidie tumlaze siti ya nyuma nimpeleke kwake"

Basi jamaa Akamlaza siti ya nyuma na akanitakia Safar njema. Nikaondoka nae kuelekea kwake nnapojua anakaa.

Katikati ya safari akadai kabanwa mkojo anataka kukojoa, ikanibidi kusimamisha gari sehem flan Kuna kigiza akakojoe. Ile namuinua kumtoa nje akakojoe, naona tayar siti imeloa afu harufu ya mkojo inanuka, nikajua uyu kashajikojolea tayar pale pale. Nikapotezea kimya.

Nikamtoa nje, akakojoe. Kachuchumaa MDA mrefu, nikamwambia "Shem HARAKA ukojoe tutoke hapa, Kuna patrol MDA huu"

Akajibu, "Apa Sijui Kuna wachawi shem, yaani Mkojo wenyewe ata hauji, Basi twende Shem nitakojoa uko uko nyumbani"

Nikamshika bega Tena kumrudisha kwny gari, Akaanza kulalamika "Shem yaan kina sinta wajinga Sana, wamemwaga pombe kwny gari yako, apa pameloa, yaan Hawa kesho lazima nitawasema. Sio ustaarabu huu."

Nikamjibu, "Sawa Shem" Basi safari ikaendelea mpaka nikamfikisha kwake, Ila maneno mengi Sana Anaongea barabarani ata hayaeleweki. Kufika kwake. Akaanza kunambia alikoficha funguo, Zaid ya sehem 3 ananambia funguo kaacha naangalia sizioni.

Kuna MDA flan mpk nikapata hasira nikataman nimuache pale pale, kuna idea ikanambia ebu nijaribu kupekua kwenye mkoba wake nione.

KWELI kwenye mkoba wake nikakuta funguo Kama bunda 3 hivi. Nikabahatisha nilizoona zinaendana, bahat nzur Moja ikakubali kufungua kitasa.

Nikambeba na kamuingiza ndani nikamuweka kwenye Kochi, akasema nimpeleke chumban akalale. Kumfikisha chumba nikambwaga kitandani kwake, nikamfunika shuka. Akapiga kelele eti yaan joto lote ili nimfunike shuka,nitakua simtakii mema, akaniomba nikamuwashie na feni.

Ikabidi nimfunue shuka na kwenda kumuwashia feni. Basi nikaaga naondoka. Nimefika nje naskia ananiita kwa sauti,
Ikabid kurudi, nauliza unasemaje, anasema "Shem usiondoke kabla sijakojoa, ebu nipeleke choon nikakojoe Ndo uende"

Basi nikamuinua, na kumpeleka chooni. Kisha niuvute mlango nimsubiri akojoe kisha aseme kamaliza ili nimrudishe kitandani. Nikaona kimya, iKabidi nigonge hodi nako kimya. Ikabidi nisukume mlango. Nikakuta kakalia sink na kachapa usingiz.

Nikamwamsha, "Shem ebu kama huna mkojo sema nikurudishe ukalale, hapo choon kwenye kulala kwenye sinki sio salama kwako, Unaweza umia"

Anasimama kwa kujivuta Vita na kusema. "Nivue chupi Shem nikojoe, mi siwezi. Imenibana Sana" (Mda huo Simu yangu ikawa inaita Sana, nikai-mute, ntaichek baadae)

Basi nikachuchumaa nakupitisha mikono katikati ya mapaja yake na kutelemsha chupi yake usawa wa magoti. Nikamwambia "Aya kaa Apo ukojoe Sasa" Kisha nikatoka zangu nje ya choo.

Nikaskia saut ya mkojo akikojoa, baada ya MDA akaniita "Shem nivalishe chupi" Basi nikachuchumaa Tena na kumvalisha chupi yake na nikamkokota na Kumtoa chooni na kumrudisha chumban kwake. Kumfikisha chumban, nikampandisha kitandani alale. Nikaona anakaza miguu.

Nikauliza Nini tatizo. Eti "nivue Hii sketi Shem, mi siwez kulala nivue kwanza iki kisketi kinanibana sana ntashindwa kujigeuza nikilala nimevaa"

Nikasema "sawa" Basi Nika fungua zipu kwa nyuma Nika mvua kisheti nikakiweka kwenye enga yake. Nikawambia, "Sasa, mi naondoka hivyo"

Akasema, "Hamna usindoke Shem, nivue na hiki kiblauzi" Basi nikapanda kitandani niweze kumgeuza kumvua iyo blauzi yake. Nikiwa namvua akawa anasema, "Sasa Shem hivi wee usikiagi joto hili na mashati mashati yako Ayo umebanana hivo" Anaongea uku na yeye akitaka kunivua shati.

Nikazuia mikono yake afu Nikamwambia, "Hamna Shem, ata usjali joto la kawaida Sana hili"

Baada ya kumvua blauz, Nikataka nishuke akanizuia, "Wee unaenda wapi, Hii sidiria unamwachia Nani na joto lote hili. itoe kwanza ndo uondoke"

Nkasema "sawa" Basi nikaanza kufungua kuanzia mgongoni ilikobanwa ili nitoe. Ile ndo namalzia kuitoa, akanibana viganja vyangu kwenye matiti yake uku ananiangukia kwa nyuma ananitizama akisema, "Shem Mungu akubariki Sana, wale vijana kwakweli wangenidhuru"

Nikamjibu uku namtoka "Mungu Ni mwema Ndo maana akanifanya niwepo nikusaidie mpaka umefika kwako" Akasema "Asante Sana Shem"

Nkamwambia "Basi sogea katikat kitandani nikufunike shuka lako mi naondoka usiku umeenda Sana" akasema "Aya, mlango wa seblen rudishia ntakuja kufunga baadae" Nkasema "sawa"

Basi nikarud kuanza safari ya kwenda kwangu, kuchek simu mfukoni missed call za wife Kama 6 hivi na sms akiuliza "Mbona uji, au leo umeamua unalala uko uko? Nifunge milango?" Nikampigia, Nkamwambia "Niko njian nakuja my love, Kuna jamaa angu nlkua nampeleka kwake nje ya mji kidg" Akasema "aya"

Basi ile naweka sim chini, shemej tena uyu anapiga, nikapokea "mejii, mi wananivamia uku. Nakufa mimi" Nikauliza, "KIVIPI tena? imekuaje?". Akasema, "Wanagonga milango na madirishani Sijui wanataka Nini Hawa watu. Nakufa meji nisaidie" Nikamwambia, "Nakuja meji, usipige kelele mi nakuja hapo sahv"

Basi nikageuza kurud kwa shemeji, Wazo likanijia, uyu kasema kavamiwa. Sio salama kufika pale na gari wataona mwanga wa gari. Basi nikaiacha mbali kidgo, nikajongea kwa mguu uku nimebeba rungu langu na sime mkononi. Kisha simu nikaweka silent mode

Kufika kwake nikaona Kuna ukimya Sana, nikakaa kwa mbali nione Kama ntaona Kuna kitu kitakatiza. Zaidi ya dkk 10 kimya, ikabd nisogee kukagua mazingira, nikaona bado kimya. Nikaenda kumgongea mlango wa sebleni bado nikaona kimya askiki mtu.

Ikabd nizunguke kwenye dirishani la chumban kwake, nikakuta mbwa wawili wanagombea ndoo ya uchafu. Waliponiona wakakimbia. Nikasogea dirishan nikaskia mtu anakoroma. Nikaita "Shem Shem, nishafika ebu fungua mlango "

Akasema nakuja, Nikarud mlangoni. Ile mlango unafunguliwa, nikaona Yuko uchi Kama alivozaliwa hata chupi hana afu akaniangukia nikamdaka asidondoke kumrudisha ndani.

Akawa hataki anasema wanataka kumuua nimvalishe aondoke. Basi Nikachukua kikoi kilikua pale kwenye kochi nikafunika maana niliona aibu sana kumtizama.

Akazidi kulalamika, Nikamwambia Hamna wachawi bhana hofu yako TU utakua uliskia mbwa walkua wanagombea ndoo ya vyakula vichafu nyuma ya dirisha lako. Akasema "Aya"

Basi Nikamuinua nikamrudisha chumbani kwake na nikamlaza. Nikaskia anakoroma. Nikamuaga nikaondoka zangu kurudi kwangu, Apo tunaenda kwenye mida ya saa 9 usku.

Kufika kwangu nikasingizia pancha Kuna rafki yangu nlkua nampeleka kwake nje ya mji afu sikUa na tairi spea, hivyo nkalazimika kulitoa na kulipeleka likazibwe na kuwekwa tyubu ili niweze kutoka pale.

Wife akanielewa, Ila sasa nikabaki na maswali mengi Sana kichwan Hivi kumbe mwanamke Akilewa anakua vile? Hivi nisingekuja wale vijana si wangembaka uko ambako wangempeleka? Hivi Kama ningekua mtu wa hovyo si ningeshatembea na shemeji yangu kwa Hali ile

Kwakweli nmegundua pombe haifai kunywewa na mwanamke Alie kwenye mahusiano na mtu. Mwanamke akishalewa kukusaliti Ni nje nje


Kiukweli,

TUCHUKUE sana TAHADHALI KUWALINDA TUWAPENDAO. Wanawake wengi pombe zinawapeleka hovyo.

Uzi tayari
 
coffee-steam.gif
 
Duh ulipata kazi nzuri sana siku hiyo,ulii njoooy?kama nakuona vile na hizo pilikapilika na uyo shemeji kama vile namuona alivyolewa na sket yake ilivyokaa upande,afu arufu ya mkojo asubui
Haya mkuu bado mwaka mpya
 
Duh ulipata kazi nzuri sana siku hiyo,ulii njoooy?kama nakuona vile na hizo pilikapilika na uyo shemeji kama vile namuona alivyolewa na sket yake ilivyokaa upande,afu arufu ya mkojo asubui
Haya mkuu bado mwaka mpya
Yaan leo asbh nmeamkia carwash

Kiukweli sikuenjoy chochote maana imenifanya nmeenda kazini na usngz Sana, nmefungua Ofisi saa 2 asbh.
Usingz ulinibana Sana nikajikuta saa 5 narud nyumban kulala mpaka saa 10.

Nmerud ofsin saa 10 mchana mpaka saa 2 usiku nikafunga na kutulia kuandika kisa hiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom