FROZEN HEART
Senior Member
- Sep 8, 2024
- 181
- 248
Amani HAIWEZI kuendelea kuwepo sehemu ambayo hakuna haki.IMAMU wa Msikiti wa Masjid Noor uliopo chini ya BAKWATA Bariadi, Mkoani Simiyu, Sheikh Yakubu Saburia, ameeleza kuwa amani ya nchi haipaswi kuhubiriwa kwa misingi ya itikadi za kisiasa au vyama, bali kama tunu ya kitaifa inayopaswa kulindwa na kila mmoja.
Akizungumza wakati wa swala ya Eidi-al-Adh-ha, Sheikh Saburia amesema Tanzania ina amani, lakini baadhi ya matamshi na mienendo ya kisiasa vinaashiria kutokuwa na dhamira ya kuitunza.
"Sisi tunayo amani, lakini tunaona kwamba haitoshi. Tunaona tunaanza kuichezea hii amani tuliyonayo, kama vile tunataka tufike mahali pa kukimbizana kama ambavyo wanakimbizana mataifa mengine," amesema Sheikh Saburia.
Ndy mana nchi NYINGI alizozitaja shekh hapo zimeingia katika vita Kwasababu ya kutokuwa na haki kati ya serikali na raia. Hatuwezi kuona watu wanapotea kama mbuzi na tukabaki kimya eti Kwa lengo na dhumuni la kuilinda amani. Sasa tutakuwa tunalinda amani au upumbavu na ujinga hapo?
Sheikh kama amekosa hutba za kuhutubia aseme watu tumpatie lakini sio kuwalisha watu pumba kichwani🙌🏿🙌🏿🙌🏿.
Wassalam